Simiyu: “Dr. Mwigulu ni Magufuli mtupu”

Simiyu: “Dr. Mwigulu ni Magufuli mtupu”

Spadino

New Member
Joined
Mar 17, 2026
Posts
4
Reaction score
30
file_000000008bec820ea6df26ff11b8a69f.png


Ziara ya Mhe. Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba Mkoani Simiyu imekonga mioyo ya wana-Simiyu. Katika mazungumzo na wananchi mbalimbali, wengi wameeleza kuvutiwa na namna Waziri Mkuu anavyokemea uzembe na wizi, pamoja na kusisitiza hatua za kubana matumizi ili fedha hizo zielekezwe katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande mwingine, wananchi hao wamesema utatuzi wa kero za wananchi papo kwa papo umesaidia wanyonge kupata haki zao. Kwa mtazamo wao, wameuita huo ni “Umagufuli mtu.”

Mmoja wa wananchi hao ananukuliwa akisema:

“Tumepata Magufuli mpya hapa. Haya tunayoyaona mbele ya macho yetu yanatukumbusha ule uongozi wa kusimamia haki na kukemea uzembe. Ona Maswa, wanyonge wamepata haki yao. Ona Bariadi na Itilima, tumeshuhudia kwa macho yetu.

Kuna baadhi ya watendaji ambao wamekuwa wakiwadhulumu wananchi na kuwanyima haki zao kwa makusudi. Lakini Waziri Mkuu anapofika, anawasikiliza wananchi, anachukua hatua na kutatua kero zao papo kwa papo. Huu ndio umagufuli wenyewe.

Sisi wananchi tumeona kwa macho yetu. Tumepata Magufuli mpya hapa. Huyu ni kiongozi anayesimama upande wa wanyonge na kutetea haki zao. Huyu ndiye Mtetezi wa Wanyonge.”

Tunajua haya ambayo tumeanza kuyasikia kwamba magenge yenye nguvu hayamtaki Waziri Mkuu na yanapambana kuhakikisha anaondoshwa au kumdhibiti kuelekea 2030. Tuseme tu, sisi wanyonge tutamwombea kwa Mungu.

Huyu ndiye Mtetezi wa Wanyonge.
 
Unajua Mwigulu ni mfugaji, na maisha ya kusikiliza na kusaidia watu yamekuwa sehemu ya maisha yake. Nilikuwa nikizungumza na Mnyiramba mmoja akanieleza kwamba zamani, pale nyumbani kwa Mwigulu Misigiri, kulikuwa na watu wengi wenye shida binafsi waliokuwa wakifika kutafuta msaada—wakidaiwa kufika zaidi ya watu 1,000 kwa siku—na kwamba alikuwa akiwapatia muda wa kuwasikiliza.

Hii inaonyesha kwamba tabia ya kusikiliza wananchi na kushughulikia changamoto zao haikuanza alipokuwa Waziri Mkuu. Tofauti ni kwamba wakati huo hakukuwa na kamera na mitandao ya kijamii iliyokuwa ikirekodi na kusambaza kila tukio kama ilivyo sasa. Leo, akiwa Waziri Mkuu, matukio mengi ya namna hiyo yanaonekana hadharani kupitia mitandao na vyombo vya habari.

Kwa hiyo, jambo la kujiuliza si kama tabia hiyo imeanza kwa sababu yuko kwenye nafasi kubwa, bali kama ni sehemu ya mwenendo ambao amekuwa nao kwa muda mrefu. Kama simulizi hizi za watu zinaweza kuthibitishwa, zinaweza kutumika kueleza tofauti kati ya tabia ya muda mrefu ya mtu na mwenendo unaotokana na nafasi anayoshikilia sasa.
 
Madelu kataa hizi sifa za kijinga wanakuweka kwenye spotlight uonekane ni threat 2030 wakule kichwa mapema.
 
Huyu ni muigizaji tu hana lolote, halafu yupo vizuri kwenye maigizo hana aibu kabisa akiwa anafanya maigizo.
Magufuli vyote alivyofanya ndivyo alivyokua toka akiwa waziri katika wizara mbalimbali , haigizi bali alikua vile ndio maana hata kabla hajawa raisi kwenye kampeni watu walikua wanasema kama tunaenda kuchagua dikteta kutokana na hulka na misimamo yake isiyoyumbishwa akiamua kitu huwezi kumrekebisha hata kama anakosea.

Huyu mwigulu ni muigizaji tu na haya yote anayafanya mawazo yote yapo kwenye uraisi na wala sio kusikiliza wananchi
 
Huyu ni muigizaji tu hana lolote, halafu yupo vizuri kwenye maigizo hana aibu kabisa akiwa anafanya maigizo.
Magufuli vyote alivyofanya ndivyo alivyokua toka akiwa waziri katika wizara mbalimbali , haigizi bali alikua vile ndio maana hata kabla hajawa raisi kwenye kampeni watu walikua wanasema kama tunaenda kuchagua dikteta kutokana na hulka na misimamo yake isiyoyumbishwa akiamua kitu huwezi kumrekebisha hata kama anakosea.

Huyu mwigulu ni muigizaji tu na haya yote anayafanya mawazo yote yapo kwenye uraisi na wala sio kusikiliza wananchi
Umeanza kumjua Mwigulu lini?
 
Umeanza kumjua Mwigulu lini?
Nimemjua toka kipindi Cha kashfa za mabomu ,kumwagia watu tindikali, kujiandika kwenye mawe kuwa ni raisi ajaye .
Huyu Bila kupepesa macho ni uwezo mdogo sana na hana hoja wala utumishi wa maana wowote ule .
Tapeli asiyekua na mvuto wowote na kingine zaidi Bado ana fikra za ujima huko anaamini kuvaa mabendera ndio uzalendo.
Mwambie uzalendo unapimwa kwa matendo sio skafu na mashati yenye bendera ya Tanzania
 
Nimemjua toka kipindi Cha kashfa za mabomu ,kumwagia watu tindikali, kujiandika kwenye mawe kuwa ni raisi ajaye .
Huyu Bila kupepesa macho ni uwezo mdogo sana na hana hoja wala utumishi wa maana wowote ule .
Tapeli asiyekua na mvuto wowote na kingine zaidi Bado ana fikra za ujima huko anaamini kuvaa mabendera ndio uzalendo.
Mwambie uzalendo unapimwa kwa matendo sio skafu na mashati yenye bendera ya Tanzania
Kuna uwezekano mkubwa hii ni chuki binafsi
 
Mtoa thread unakuja na ID tofauti kwenye uzi mmoja. unaandika thread na ku comment mwenyewe post no. 4.

Mwigulu ni fala mmoja mzuri sana, muigizaji mahiri, fisadi la karne. Wanyiramba si watu wa kupewa madaraka makubwa. Speaking frm experience, natokea kijiji kimoja na huyo muhuni mwigulu.
 
Et magufuri mtupu!!

Ivi jamaa magufuri unamjua kweli wewe? Au unadhani kipindi magufuri rais sisi tulikuwa watoto wadogo?
 
View attachment 3672626

Ziara ya Mhe. Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba Mkoani Simiyu imekonga mioyo ya wana-Simiyu. Katika mazungumzo na wananchi mbalimbali, wengi wameeleza kuvutiwa na namna Waziri Mkuu anavyokemea uzembe na wizi, pamoja na kusisitiza hatua za kubana matumizi ili fedha hizo zielekezwe katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande mwingine, wananchi hao wamesema utatuzi wa kero za wananchi papo kwa papo umesaidia wanyonge kupata haki zao. Kwa mtazamo wao, wameuita huo ni “Umagufuli mtu.”

Mmoja wa wananchi hao ananukuliwa akisema:

“Tumepata Magufuli mpya hapa. Haya tunayoyaona mbele ya macho yetu yanatukumbusha ule uongozi wa kusimamia haki na kukemea uzembe. Ona Maswa, wanyonge wamepata haki yao. Ona Bariadi na Itilima, tumeshuhudia kwa macho yetu.

Kuna baadhi ya watendaji ambao wamekuwa wakiwadhulumu wananchi na kuwanyima haki zao kwa makusudi. Lakini Waziri Mkuu anapofika, anawasikiliza wananchi, anachukua hatua na kutatua kero zao papo kwa papo. Huu ndio umagufuli wenyewe.

Sisi wananchi tumeona kwa macho yetu. Tumepata Magufuli mpya hapa. Huyu ni kiongozi anayesimama upande wa wanyonge na kutetea haki zao. Huyu ndiye Mtetezi wa Wanyonge.”

Tunajua haya ambayo tumeanza kuyasikia kwamba magenge yenye nguvu hayamtaki Waziri Mkuu na yanapambana kuhakikisha anaondoshwa au kumdhibiti kuelekea 2030. Tuseme tu, sisi wanyonge tutamwombea kwa Mungu.

Huyu ndiye Mtetezi wa Wanyonge.
Yaani ni kama yule mshambuliaji hatari wa simba Ibrahim Doumbia! Na yeye ni Osimhen mtupu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom