Simba wamtenga mwenzao aliyefanyiwa upasuaji

Simba wamtenga mwenzao aliyefanyiwa upasuaji

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
8,273
Reaction score
25,297


Arusha. Simba aliyefanyiwa upasuaji Novemba 8 mwaka huu baada ya kuugua ugonjwa wa henia na matatizo ya misuli ya tumbo hatimaye ametengwa na wenzake.

Sababu za kutengwa kwa Simba huyo anayeishi katika hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha zimedaiwa kwamba ni kutokana na harufu ya dawa alizopewa baada ya kufanyiwa upasuaji.

Pia sababu nyingine ya kutengwa kwa Simba huyo ni baada ya viungo vyake vya ndani ya tumbo kuwa nje tofauti na ilivyo kawaida.

Mtaalamu wa Tiba Afya ya Wanyama Pori kutoka mamlaka ya hifadhi ya Ngorogoro Dk Atanas Nyaki amesema jaribio la kumrejesha simba huyo porini limeshindikana na kulazimu ahifadhiwe sehemu maalumu kwa usalama wake ili kuepuka hatari inayoweza kumpata.

“Tumetumia dawa zenye harufu kali inawafanya wenzake kusikia tofauti na walivyomzoea ndio sababu ya kumtenga,” amesema Dk Atanasi

Amesema pamoja na kufanyiwa upasuaji huo ambao ulikuwa mkubwa na si rahisi bado ataendelea kuwa na uvimbe ambao hautamuathiri na yuko chini ya uangalizi wa hali ya juu.

Aidha amesema wao kama madaktari wamejihakikishia kwamba anaweza kuchanganyika na wenzake ingawa wamemkataa hivyo wamejitahidi kuokoa maisha yake kwani wenzake walikuwa wakitaka kumuua.

Ameongeza kwamba Simba huyo anajengewa banda lake kama ilivyofanyika kwa Faru Fausta, na sasa wanasubiri uamuzi wa Serikali kujua wapi watampeleka kwani mnyama huyo ni mali ya Serikali.


Mwananchi
 
Hahaaaa simba alikua anaumwa "ngiri" wenzake wamemtenga........
 
[emoji85] [emoji85] [emoji85]
Kwa wataalam wa wanyama waende kuwatibu binadamu[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Umemjibu kikubwa, congs..nchi hii kila kitu watu wanatia siasa,ni mara ngapi tumesikia mnyama huyu mzuri anahitaji upasuaji wa lazima? Ni nadra sana..pongezi zangu ziende TANAPA hizi ndio habari zenye kutia faraja sana.
 
Ecology ....huyo simba mgonjwa wasingemtibu

wangemuacha aliwe na fisi huo ndio utaratibu

wa porini ....binadamu anaanza kuingilia eco system???
Binadamu tunaingilia sana utaratibu wa asili, kuna mahali huko america waliamua kuua mbweha wakidhani kuwatowesha itawaacha salama, lakini matokeo yake miaka 15 baadae eneo likaanza kuwa jangwa, mto ukakauka, kumne uwepo wa wale mbweha ulisaidia kufanya eneo lishamiri kwa kuwa kuna wanyama wengine(jina nimelisahau) wanazaliana sana na wanakula majani hivyo mbweha walikua wanaweka uwiano na kufanya eneo lishamiri na kupendeza, baada ya study kadhaa wakagundua hilo hivyo wameamua kuanza kuzalisha mbweha maeneo hayo.
 
sku hizi wanyama wanathamani kuliko hata binadamu.......haya ngoja nayeye atengewe kitita.
Wanthaminiwa kiasi kwamba hadi binaadam wanaamua kwenda kupanga foleni kutibiwa kwenye meli ya mchina.
 
Chamsingi tu wasije sema kaundiwa kamati na kutengewa 100s million
 
kwanini wahangaike na simba ambaye faida yake si direct waachane na mama wajawazito kule mwananyamala, vipaumbele buana
Huyo simba kuna watu wanalipa madolari kuja kumuona na kumpiga picha kuna ubaya akitibiwa ili aendelee kuleta mpunga ambao utajenga hospitali na shule na ajira na kadhalika na kadhalika au we unaoje ndugu?
 
Sa ivi ni kutengeneza mrija wako wa kuingiza hela na iwapo utaulizwa uwe na uthibitisho tu.
 
Ecology ....huyo simba mgonjwa wasingemtibu

wangemuacha aliwe na fisi huo ndio utaratibu

wa porini ....binadamu anaanza kuingilia eco system???
Sasa mkuu, ukiongelea ecology, basi na binadamu wasitibiwe ili ku balance nature.
 
Huyu walitakiwa wamuache tu apambane na hali yake ndiyo Nature inavyotaka
 
Back
Top Bottom