GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,721
- 109,155
Na kama ni takwa la kiufundi mwambieni huyo aliyeamua hivi kuwa hii ni hatari na itatugharimu kimatokeo.
Ningewaelewa Simba S.C. (hasa kiufundi) kama wangeenda Angola siku tatu kabla ila hii ya kwenda siku moja kabla ya mechi (yaani Jumamosi na kucheza Jumapili) ni hatari kimchezo (kimaandalizi), na hapa wala GENTAMYCINE nisimung'unye maneno kuwa tumefanya kosa kubwa sana.
Hivi kweli ndani ya siku moja huko Angola wachezaji wa Simba S.C. watazoea hali ya hewa, mazingira kiujumla na kuzoea uwanja ili kuweza kujiandaa vyema kisaikolojia kwa mchezo husika wa siku ya Jumapili? Hii ni kujiua kiufundi kwa Simba S.C. na tutake tusitake ni lazima itatugharimu katika utendaji wetu uwanjani siku ya mtanange (mechi).
Nilikuwa mbishi kuamini kuwa sasa Simba S.C. kuna ukata (bajeti hafifu) na pia mwekezaji Mo Dewji ni kama vile amesusa na kajiweka kando, ila kwa hili la kwenda nchini Angola Jumamosi na mechi Jumapili naamini rasmi kuwa mzigo ndani ya Simba S.C. umekata na wala tusitake kudanganyana juu ya hili.
Ukiwa umecheza mpira, ni mtu wa mpira au ni mdau (mchambuzi na mwaimu) wa mpira utanielewa vyema GENTAMYCINE kwa hiki nilichokiandika hapa, ila ukiwa ni "Ngala ngala' kamwe hutonielewa na utabaki kunishangaa tu.
Kazi ipo tu Jumapili kwa Waangola!
Ningewaelewa Simba S.C. (hasa kiufundi) kama wangeenda Angola siku tatu kabla ila hii ya kwenda siku moja kabla ya mechi (yaani Jumamosi na kucheza Jumapili) ni hatari kimchezo (kimaandalizi), na hapa wala GENTAMYCINE nisimung'unye maneno kuwa tumefanya kosa kubwa sana.
Hivi kweli ndani ya siku moja huko Angola wachezaji wa Simba S.C. watazoea hali ya hewa, mazingira kiujumla na kuzoea uwanja ili kuweza kujiandaa vyema kisaikolojia kwa mchezo husika wa siku ya Jumapili? Hii ni kujiua kiufundi kwa Simba S.C. na tutake tusitake ni lazima itatugharimu katika utendaji wetu uwanjani siku ya mtanange (mechi).
Nilikuwa mbishi kuamini kuwa sasa Simba S.C. kuna ukata (bajeti hafifu) na pia mwekezaji Mo Dewji ni kama vile amesusa na kajiweka kando, ila kwa hili la kwenda nchini Angola Jumamosi na mechi Jumapili naamini rasmi kuwa mzigo ndani ya Simba S.C. umekata na wala tusitake kudanganyana juu ya hili.
Ukiwa umecheza mpira, ni mtu wa mpira au ni mdau (mchambuzi na mwaimu) wa mpira utanielewa vyema GENTAMYCINE kwa hiki nilichokiandika hapa, ila ukiwa ni "Ngala ngala' kamwe hutonielewa na utabaki kunishangaa tu.
Kazi ipo tu Jumapili kwa Waangola!