Simba na Yanga: Jinsi ushabiki wa mikeka ulivyoua ushabiki wa mpira

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,847
18,253
Zamani kabla mikeka haijaingia hapa nchini mashabiki wa mpira walikuwa na ushabiki halisi kwa timu zao pendwa. Nakumbuka mechi kati ya Man United na Arsenal iliyochezwa mwaka 2003. Van Van Nistelrooy alikosa penati dakika za majeruhi. Siku hiyo kulikuwa na mshawasha mkubwa sana miongoni mwa mashabiki wa miamba hii miwili ya soka la England.


View: https://www.youtube.com/watch?v=hhA3wcvrgyY

Tulitazama mpira huo kwenye banda moja la mpira mjini Morogoro karibu na hoteli ya GM. Kulikuwa na mashabiki wengi sana. Banda lilijaa hadi mwenye banda akalazimika kutuhamishia kwenye TV nyingine iliyokuwa uwani. Nako kulijaa pomoni. Mashabiki walikuwa na ari kubwa sana kila mmoja akiitambia timu yake kushinda. Bahati mbaya Man United wakakosa penati dakika za majeruhi, kitendo kiliwasononesha mashabiki wake mpaka leo.

Kwa sasa ushabiki wa mpira umedorora sana. Si kwa sababu nyingine bali ni kwa saabu ususi wa mikeka. Siku hizi ni kawaida shabiki wa Arsenal kuiua timu yake kwenye mkeka na kuipa ushindi timu pinzani. Kitendo hiki huua kabisa ule ushabiki uliomo ndani ya shabiki aliyesuka mkeka na kuamua kuia timu yake. Kwa mujibu wa utafiti nilioufanya hivi karibuni, zaidi ya 90% ya mashabiki wa mpira waasuka mikeka.

Siku moja nilikuwa mahali fulani natazama mpira nikashuhudia shabiki wa Man United anashangilia goli baada ya timu yake kufungwa. Nilishikwa na butwaa nikidhani labda yule shabiki ni mwehu. Kabla sijamaliza kushangaa, nikamuona anaomba kalamu na kuweka tiki kwenye mkeka. Ndipo nilipogutuka kumbe alikuwa anshangilia mkeka sio timu.

Ni kawaida kwa shabiki wa timu A kuonekana anaishangilia timu B ambayo ni mpinzani mkubwa wa timu yake kwa sababu tu timu B ikishinda mkeka wake unapumua. Katika hali kama hii, unadhani msisimko wa kishabiki utatoka wapi?

Mashabiki wengi wa aina hii huwa wanaepuka kwenda kutazama mpira mubashara, hasa pale wanapokuwa wamesuka mikeka na kuziua timu zao au kuzipa ushindi timu pinzani. Badala yake hubakia mafichoni wakifuatilia matokeo kwenye simu au kwa kuwapigia simu mashabiki wanaotazama mpira mubashara. Hii ndio sababu ya mashabiki wengi kushindwa kutazama mpira timu zao zinapocheza. Wanawaza mikeka tu!

Kitendo hiki cha kushabikia mikeka ghairi ya timu kimechangia pakubwa kuharibu ushabiki asilia wa mpira kama ilivyokuwa hapo zamani kabla ya mauzauza ya mikeka kuingia hapa nchini.

Nawasilisha.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Umeongea ukweli mtupu, mimi huwa ninashabikia hela.

Mfano juzi nilimuua Simba dhidi ya Wydad ili nipate hela pamoja na kuipenda mno Simba.
Kabisa. Ushabiki wa mikeka ni jinamizi lililokuja kuua ushabiki na kuondoa kabisa ule utamu wa mpira hasa mtu unapokuwa umeua timu yako kwenye mkeka. Nafsi yako inagawanyika mara 2:

1. Timu yako ikifungwa unajipoza kwa mkeka.
2. Mkeka ukichanika, unajipoza kwa ushindi.

Kwa ujumla hili ni tatizo la dunia nzima sio hapa Tanzania tu.
 
Kabisa. Ushabiki wa mikeka ni jinamizi lililokuja kuua ushabiki na kuondoa kabisa ule utamu wa mpira hasa mtu unapokuwa umeua timu yako kwenye mkeka. Nafsi yako inagawanyika mara 2:

1. Timu yako ikifungwa unajipoza kwa mkeka.
2. Mkeka ukichanika, unajipoza kwa ushindi.

Kwa ujumla hili ni tatizo la dunia nzima sio hapa Tanzania tu.
Mimi siku hizi huwa ninaiombea Yanga ishinde ikiwa inacheza mechi za ligi kuu (NBC).


Nikiwa kwa washabiki uchwara wenzangu ninajifanya kuipondea Yanga, lakini kiukweli ninapenda ishinde ili na mimi mfukoni nipate hela ya kumwagilia moyo.

Sitaki ushabiki wa kufurahia wengine wakipata hela uwanjani halafu mimi nibaki mweupe mfukoni
 
Zamani kabla mikeka haijaingia hapa nchini mashabiki wa mpira walikuwa na ushabiki halisi kwa timu zao pendwa. Nakumbuka mechi kati ya Man United na Arsenal iliyochezwa mwaka 2003. Van Van Nistelrooy alikosa penati dakika za majeruhi. Siku hiyo kulikuwa na mshawasha mkubwa sana miongoni mwa mashabiki wa miamba hii miwili ya soka la England.


View: https://www.youtube.com/watch?v=hhA3wcvrgyY

Tulitazama mpira huo kwenye banda moja la mpira mjini Morogoro karibu na hoteli ya GM. Kulikuwa na mashabiki wengi sana. Banda lilijaa hadi mwenye banda akalazimika kutuhamishia kwenye TV nyingine iliyokuwa uwani. Nako kulijaa pomoni. Mashabiki walikuwa na ari kubwa sana kila mmoja akiitambia timu yake kushinda. Bahati mbaya Man United wakakosa penati dakika za majeruhi, kitendo kiliwasononesha mashabiki wake mpaka leo.

Kwa sasa ushabiki wa mpira umedorora sana. Si kwa sababu nyingine bali ni kwa saabu ususi wa mikeka. Siku hizi ni kawaida shabiki wa Arsenal kuiua timu yake kwenye mkeka na kuipa ushindi timu pinzani. Kitendo hiki huua kabisa ule ushabiki uliomo ndani ya shabiki aliyesuka mkeka na kuamua kuia timu yake. Kwa mujibu wa utafiti nilioufanya hivi karibuni, zaidi ya 90% ya mashabiki wa mpira waasuka mikeka.

Siku moja nilikuwa mahali fulani natazama mpira nikashuhudia shabiki wa Man United anashangilia goli baada ya timu yake kufungwa. Nilishikwa na butwaa nikidhani labda yule shabiki ni mwehu. Kabla sijamaliza kushangaa, nikamuona anaomba kalamu na kuweka tiki kwenye mkeka. Ndipo nilipogutuka kumbe alikuwa anshangilia mkeka sio timu.

Ni kawaida kwa shabiki wa timu A kuonekana anaishangilia timu B ambayo ni mpinzani mkubwa wa timu yake kwa sababu tu timu B ikishinda mkeka wake unapumua. Katika hali kama hii, unadhani msisimko wa kishabiki utatoka wapi?

Mashabiki wengi wa aina hii huwa wanaepuka kwenda kutazama mpira mubashara, hasa pale wanapokuwa wamesuka mikeka na kuziua timu zao au kuzipa ushindi timu pinzani. Badala yake hubakia mafichoni wakifuatilia matokeo kwenye simu au kwa kuwapigia simu mashabiki wanaotazama mpira mubashara. Hii ndio sababu ya mashabiki wengi kushindwa kutazama mpira timu zao zinapocheza. Wanawaza mikeka tu!

Kitendo hiki cha kushabikia mikeka ghairi ya timu kimechangia pakubwa kuharibu ushabiki asilia wa mpira kama ilivyokuwa hapo zamani kabla ya mauzauza ya mikeka kuingia hapa nchini.

Nawasilisha.

Kusema kweli MIKEKA imeharibu sana ile ladha halisi na ushabiki wa mpira kindakindaki. Kazi tunayo.
 
Zamani kabla mikeka haijaingia hapa nchini mashabiki wa mpira walikuwa na ushabiki halisi kwa timu zao pendwa. Nakumbuka mechi kati ya Man United na Arsenal iliyochezwa mwaka 2003. Van Van Nistelrooy alikosa penati dakika za majeruhi. Siku hiyo kulikuwa na mshawasha mkubwa sana miongoni mwa mashabiki wa miamba hii miwili ya soka la England.


View: https://www.youtube.com/watch?v=hhA3wcvrgyY

Tulitazama mpira huo kwenye banda moja la mpira mjini Morogoro karibu na hoteli ya GM. Kulikuwa na mashabiki wengi sana. Banda lilijaa hadi mwenye banda akalazimika kutuhamishia kwenye TV nyingine iliyokuwa uwani. Nako kulijaa pomoni. Mashabiki walikuwa na ari kubwa sana kila mmoja akiitambia timu yake kushinda. Bahati mbaya Man United wakakosa penati dakika za majeruhi, kitendo kiliwasononesha mashabiki wake mpaka leo.

Kwa sasa ushabiki wa mpira umedorora sana. Si kwa sababu nyingine bali ni kwa saabu ususi wa mikeka. Siku hizi ni kawaida shabiki wa Arsenal kuiua timu yake kwenye mkeka na kuipa ushindi timu pinzani. Kitendo hiki huua kabisa ule ushabiki uliomo ndani ya shabiki aliyesuka mkeka na kuamua kuia timu yake. Kwa mujibu wa utafiti nilioufanya hivi karibuni, zaidi ya 90% ya mashabiki wa mpira waasuka mikeka.

Siku moja nilikuwa mahali fulani natazama mpira nikashuhudia shabiki wa Man United anashangilia goli baada ya timu yake kufungwa. Nilishikwa na butwaa nikidhani labda yule shabiki ni mwehu. Kabla sijamaliza kushangaa, nikamuona anaomba kalamu na kuweka tiki kwenye mkeka. Ndipo nilipogutuka kumbe alikuwa anshangilia mkeka sio timu.

Ni kawaida kwa shabiki wa timu A kuonekana anaishangilia timu B ambayo ni mpinzani mkubwa wa timu yake kwa sababu tu timu B ikishinda mkeka wake unapumua. Katika hali kama hii, unadhani msisimko wa kishabiki utatoka wapi?

Mashabiki wengi wa aina hii huwa wanaepuka kwenda kutazama mpira mubashara, hasa pale wanapokuwa wamesuka mikeka na kuziua timu zao au kuzipa ushindi timu pinzani. Badala yake hubakia mafichoni wakifuatilia matokeo kwenye simu au kwa kuwapigia simu mashabiki wanaotazama mpira mubashara. Hii ndio sababu ya mashabiki wengi kushindwa kutazama mpira timu zao zinapocheza. Wanawaza mikeka tu!

Kitendo hiki cha kushabikia mikeka ghairi ya timu kimechangia pakubwa kuharibu ushabiki asilia wa mpira kama ilivyokuwa hapo zamani kabla ya mauzauza ya mikeka kuingia hapa nchini.

Nawasilisha.

Arsenal alipofungwa leo mashabiki wa Man United wamehuzunika kwa sababu mikeka yao imechanika. Jambo hili linaharibu sana utamu wa ushabiki wa mpira.

Hata sasa hivi Yanga wanavyoongoza magoli 4 kwa nunge mashabiki wa Simba wamefurahi kwa kuwa mikeka imesoma. Siku hizi ushabiki wa kweli umeisha; kila mtu amehamia kwenye ushabiki wa mikeka. Inauma sana.
 
Zamani kabla mikeka haijaingia hapa nchini mashabiki wa mpira walikuwa na ushabiki halisi kwa timu zao pendwa. Nakumbuka mechi kati ya Man United na Arsenal iliyochezwa mwaka 2003. Van Van Nistelrooy alikosa penati dakika za majeruhi. Siku hiyo kulikuwa na mshawasha mkubwa sana miongoni mwa mashabiki wa miamba hii miwili ya soka la England.


View: https://www.youtube.com/watch?v=hhA3wcvrgyY

Tulitazama mpira huo kwenye banda moja la mpira mjini Morogoro karibu na hoteli ya GM. Kulikuwa na mashabiki wengi sana. Banda lilijaa hadi mwenye banda akalazimika kutuhamishia kwenye TV nyingine iliyokuwa uwani. Nako kulijaa pomoni. Mashabiki walikuwa na ari kubwa sana kila mmoja akiitambia timu yake kushinda. Bahati mbaya Man United wakakosa penati dakika za majeruhi, kitendo kiliwasononesha mashabiki wake mpaka leo.

Kwa sasa ushabiki wa mpira umedorora sana. Si kwa sababu nyingine bali ni kwa saabu ususi wa mikeka. Siku hizi ni kawaida shabiki wa Arsenal kuiua timu yake kwenye mkeka na kuipa ushindi timu pinzani. Kitendo hiki huua kabisa ule ushabiki uliomo ndani ya shabiki aliyesuka mkeka na kuamua kuia timu yake. Kwa mujibu wa utafiti nilioufanya hivi karibuni, zaidi ya 90% ya mashabiki wa mpira waasuka mikeka.

Siku moja nilikuwa mahali fulani natazama mpira nikashuhudia shabiki wa Man United anashangilia goli baada ya timu yake kufungwa. Nilishikwa na butwaa nikidhani labda yule shabiki ni mwehu. Kabla sijamaliza kushangaa, nikamuona anaomba kalamu na kuweka tiki kwenye mkeka. Ndipo nilipogutuka kumbe alikuwa anshangilia mkeka sio timu.

Ni kawaida kwa shabiki wa timu A kuonekana anaishangilia timu B ambayo ni mpinzani mkubwa wa timu yake kwa sababu tu timu B ikishinda mkeka wake unapumua. Katika hali kama hii, unadhani msisimko wa kishabiki utatoka wapi?

Mashabiki wengi wa aina hii huwa wanaepuka kwenda kutazama mpira mubashara, hasa pale wanapokuwa wamesuka mikeka na kuziua timu zao au kuzipa ushindi timu pinzani. Badala yake hubakia mafichoni wakifuatilia matokeo kwenye simu au kwa kuwapigia simu mashabiki wanaotazama mpira mubashara. Hii ndio sababu ya mashabiki wengi kushindwa kutazama mpira timu zao zinapocheza. Wanawaza mikeka tu!

Kitendo hiki cha kushabikia mikeka ghairi ya timu kimechangia pakubwa kuharibu ushabiki asilia wa mpira kama ilivyokuwa hapo zamani kabla ya mauzauza ya mikeka kuingia hapa nchini.

Nawasilisha.

Mikeka imeondoka na utamu wote wa mpira.
 
Ushabiki maandazi kwa Simba na Yanga umepelekea timu hizi kucheza mpira mdomoni zaidi kuliko uwanjani. Inasikitisha sana.
 
Mimi siku hizi huwa ninaiombea Yanga ishinde ikiwa inacheza mechi za ligi kuu (NBC).


Nikiwa kwa washabiki uchwara wenzangu ninajifanya kuipondea Yanga, lakini kiukweli ninapenda ishinde ili na mimi mfukoni nipate hela ya kumwagilia moyo.

Sitaki ushabiki wa kufurahia wengine wakipata hela uwanjani halafu mimi nibaki mweupe mfukoni
Halafu unatoka nje kwenda kushangilia ukiwa unacheki na mkeka
 
Back
Top Bottom