Simba mnatolewa kwenye mstari na Ushabiki wa kijinga

May Day

JF-Expert Member
May 18, 2018
6,162
8,820
Kumezuka mtindo wa baadhi ya Mashabiki kujiona kwamba wao ndio Mashabiki wenye haki au bora au kindakindaki sana kuliko Mashabiki wengine.

Kila jambo wao wanataka kuliongelea hata kama hawana chochote wanachofahamu kuhusina nalo.

Ni ushabiki gani huu wa kushindwa kukubali timu kupoteza au kutoka suluhu?, hivi hizo timu nyingine kwani hazijiandai kushindana, kwani hao Makocha wengine hawafundishi hizo timu zao kwamba basi wakikutana na Timu yako tu basi wanapaswa kupoteza?

Ni sawa huenda kufungwa na Mtani kunanyong'onyeza lakini ndio iwe nongwa? Hawa Namungo si ndio waliwasumbua hata Yanga na nusura tu watoke suluhu, na si waliwapiga Azam 3 na ubora wao wote, sasa Simba kupata droo vipi iwe nongwa?.

Ingekuwa ni Timu inayopaswa kushinda tu wakati wote kuna haja gani basi ya kuwa na ligi?.

Nadhani udhaifu mkubwa kabisa kuliko wote ni hii ya kuonekana kukosa umoja pindi tu timu inapopoteza, kuliko hata kupoteza kwenyewe ndani ya uwanja.

Hiki ni kipindi cha Simba kuwa makini sana maana ndio kipindi ambacho Mamluki wanapenyeza ajenda zao na ikiwezekana kuitoa kabisaTimu kwenye Reli.

Furaha ya Simba ni Yanga kupoteza, na furaha ya Yanga ni Simba kupoteza, na tusisahau kwamba si kupoteza uwanjani tu, bali pia hata ikiwezekana kuipoteza timu.

Chondechonde Wana Simba, kuna Watu wapo kazini wanachochea kuni kwa bidii, hawalali, tusiwe kama Mazuzu mnachonganishwa nanyi mnavurugana kweli.
 
Hii imeonesha simba ni team ya watoto, yan game moja tu watu wote wametoka kwa reli kabisa
Ni Mamluki hao, Shabiki wa kweli hana akili hizo.

Mfano hili la kuwatuhumu Wachezaji kabisani ajenda iliyopenyezwa na maadui, na Simba tunapokea tuna na kwenda nalo kama dodoki linavyofyonza kila kitu.
 
Kumezuka mtindo wa baadhi ya Mashabiki kujiona kwamba wao ndio Mashabiki wenye haki au bora au kindakindaki sana kuliko Mashabiki wengine.

Kila jambo wao wanataka kuliongelea hata kama hawana chochote wanachofahamu kuhusina nalo.

Ni ushabiki gani huu wa kushindwa kukubali timu kupoteza au kutoka suluhu?, hivi hizo timu nyingine kwani hazijiandai kushindana, kwani hao Makocha wengine hawafundishi hizo timu zao kwamba basi wakikutana na Timu yako tu basi wanapaswa kupoteza?

Ni sawa huenda kufungwa na Mtani kunanyong'onyeza lakini ndio iwe nongwa? Hawa Namungo si ndio waliwasumbua hata Yanga na nusura tu watoke suluhu, na si waliwapiga Azam 3 na ubora wao wote, sasa Simba kupata droo vipi iwe nongwa?.

Ingekuwa ni Timu inayopaswa kushinda tu wakati wote kuna haja gani basi ya kuwa na ligi?.

Nadhani udhaifu mkubwa kabisa kuliko wote ni hii ya kuonekana kukosa umoja pindi tu timu inapopoteza, kuliko hata kupoteza kwenyewe ndani ya uwanja.

Hiki ni kipindi cha Simba kuwa makini sana maana ndio kipindi ambacho Mamluki wanapenyeza ajenda zao na ikiwezekana kuitoa kabisaTimu kwenye Reli.

Furaha ya Simba ni Yanga kupoteza, na furaha ya Yanga ni Simba kupoteza, na tusisahau kwamba si kupoteza uwanjani tu, bali pia hata ikiwezekana kuipoteza timu.

Chondechonde Wana Simba, kuna Watu wapo kazini wanachochea kuni kwa bidii, hawalali, tusiwe kama Mazuzu mnachonganishwa nanyi mnavurugana kweli.
Inategemea. Kupigwa 5 kunakotokana na kukabia macho huo ni uzembe mkuu. Wachezaji wote wakijitoa kwa moyo kama anavyofanya Kibu D hata wakipigwa 10 ni Sawa Tu.
 
Kule kwa wenzenu kuna watu wawili wenye akili wanaongoza wengine, ila huko kwenu wote ni mbumbumbu
Sio wote tuombe radhi, ila kuna Wachache wanaosumbua wengine..tupo wenye akili na kujua maana ya kushindana.
 
Inategemea. Kupigwa 5 kunakotokana na kukabia macho huo ni uzembe mkuu. Wachezaji wote wakijitoa kwa moyo kama anavyofanya Kibu D hata wakipigwa 10 ni Sawa Tu.
Labda kila Mtu ana namna yake ya kutathmini mechi. Ila kwangu naona tulizidiwa mbinu tu na mechi ikawa mzigo mzito kwa Wachezaji, tutawalaumu Wachezaji bure bila ya sababu.
 
Labda kila Mtyu ana namna yake ya kutathmini mechi. Ila kwangu naona tulizidiwa mbinu tu na mechi ikawa mzigo mzito kwa Wachezaji, tutawalaumu Wachezaji bure bila ya sababu.
Aina ya wachezaji wa Yanga kuwaacha wachezee mpira vile unachokitafuta lazima ukipate. Unawakabia macho akina Pacome unategemea nini?. Mbona kwenye mechi ya Simba 2-0 Yanga,Simba walikaba wapita njia wote hadi vichochoro vyote. Manula akawa anasoma gazeti tu. Walishindwa vipi kufanya hivyo tena?.
 
Back
Top Bottom