Simba imeyaheshimisha mashindano ya Kombe la Mapinduzi

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,898
Wakati kuna katimu kanajifanya kana "besi" la kusema mashindano ya kombe la mapinduzi hayana maana na kwamba yana gundu, Simba haikusikia kelele za vyura hao na badala yake imeyapa mashindano ya Kombe la Mapinduzi heshima inayostahili. Ukiacha kombe itakalobeba leo na zawadi za pesa, nadhani klabu ya Simba inastahili tuzo maalumu kutoka SMZ.

Ushauri wangu kwa SMZ na Kamati ya mashindano, kabla ya mashindano yajayo wakae chini na uongozi wa Simba ili waone ni jinsi gani wanaweza kuyafanya mashindano haya yakawa bora zaidi. Simba ina ushawishi wa kuvutia timu kubwa zije kushiriki na kuachana na hawa viroboto wanaodhani bila wao mambo hayawezi kwenda.

Ukipata jumla ya timu 8, tatu za Z'bar na zinazobaki kutoka kanda tofauti za Africa, wacheze makundi mawili, ondoa robo fainali itapunguza uchovu wa mechi kuwa nyingi ndani ya muda mfupi. Hadi fainali, timu zitakuwa zimecheza mechi 5 tu. Mashindano haya yanaweza kusaidia timu kuboresha vikosi vyao kipindi cha likizo fupi ila bila kukamiana.

Wale wanaoona mashindano haya hayana maana wawekwe pembeni kwanza hadi watakapojitambua.
 
Tafuta Moja ya sababu iliyofanya mashindano ya muungano yavunjike, ukipata sababu uje uandike porojozako.
Nakudokezea: Yanga walipogomea na ndipo yalivunjika.
Kwasasa Simba zaidi ya mapinduzi cup Hana kikombe anacho gombea, ni vizuri apambane kwa nguvu zote ikiwa pamoja na makosa ya kibinadamu ili atwae kikombe icho, akikosa ameumia.
 
Tafuta Moja ya sababu iliyofanya mashindano ya muungano yavunjike, ukipata sababu uje uandike porojozako.
Nakudokezea: Yanga walipogomea na ndipo yalivunjika.
Kwasasa Simba zaidi ya mapinduzi cup Hana kikombe anacho gombea, ni vizuri apambane kwa nguvu zote ikiwa pamoja na makosa ya kibinadamu ili atwae kikombe icho, akikosa ameumia.
susa.gif
 
JApo hujaitaja timu mlengwa ila kuna kitu kimenijia ngoja nikiandike. Hakuna anayeweza kuleta jeuri kwa Yanga. Kwa TZ hii bila kuwepo yanga kwenye shughuli za michezo hakuna kitakachonoga. Kama unabisha kamuulize Mangungu na Jaribu tena.
Kwamba bila yanga😁,,,sasa nyie mna nini cha muhim vyura
 
JApo hujaitaja timu mlengwa ila kuna kitu kimenijia ngoja nikiandike. Hakuna anayeweza kuleta jeuri kwa Yanga. Kwa TZ hii bila kuwepo yanga kwenye shughuli za michezo hakuna kitakachonoga. Kama unabisha kamuulize Mangungu na Jaribu tena.
MAUMI FC?
ambao hata huko duniani haina lolote?hebu tutolee huu ushubwada ulioutype hapa
 
Wakati kuna katimu kanajifanya kana "besi" la kusema mashindano ya kombe la mapinduzi hayana maana na kwamba yana gundu, Simba haikusikia kelele za vyura hao na badala yake imeyapa mashindano ya Kombe la Mapinduzi heshima inayostahili. Ukiacha kombe itakalobeba leo na zawadi za pesa, nadhani klabu ya Simba inastahili tuzo maalumu kutoka SMZ.

Ushauri wangu kwa SMZ na Kamati ya mashindano, kabla ya mashindano yajayo wakae chini na uongozi wa Simba ili waone ni jinsi gani wanaweza kuyafanya mashindano haya yakawa bora zaidi. Simba ina ushawishi wa kuvutia timu kubwa zije kushiriki na kuachana na hawa viroboto wanaodhani bila wao mambo hayawezi kwenda.

Ukipata jumla ya timu 8, tatu za Z'bar na zinazobaki kutoka kanda tofauti za Africa, wacheze makundi mawili, ondoa robo fainali itapunguza uchovu wa mechi kuwa nyingi ndani ya muda mfupi. Hadi fainali, timu zitakuwa zimecheza mechi 5 tu. Mashindano haya yanaweza kusaidia timu kuboresha vikosi vyao kipindi cha likizo fupi ila bila kukamiana.

Wale wanaoona mashindano haya hayana maana wawekwe pembeni kwanza hadi watakapojitambua.
Mh
 
"Simba haikusikia kelele za vyura hao na badala yake imeyapa mashindano ya Kombe la Mapinduzi heshima inayostahili. Ukiacha kombe itakalobeba leo na zawadi za pesa, nadhani klabu ya Simba inastahili tuzo maalumu kutoka SMZ."

Haya ni maneno ya mkolofive mmoja aliyeongea kwa kuchanganyikiwa kwa kipigo cha goli tano.

Haya kachukueni hilo kombe, unadhani kila siku utafanikiwa kwa dhurma?
 
Back
Top Bottom