Silaha za Laser: Marekani na mbio za silaha mpya za miale na mionzi (DEW) katika Karne ya 21

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,619
46,259
Silaha za laser "Laser weapons" ndio silaha zinazotegemewa kuwa silaha za viwango vya juu zaidi duniani kuyasaidia majeshi dhidi ya makombora yote katika karne ya 21.

Silaha za laser ni silaha za aina gani?

Silaha za laser ni silaha zitakazokuwa zinatumia nguvu za miale ya laser kuharibu mifumo ya vifaa vya kijeshi kama maroketi, helicopters, ndege, rada, makombora n.k ishindwe kufanya kazi zake, kutembea au ishindwe kulipuka kama ilivyokusidwa kwenye target yake pale miale hiyo ya laser inapoelekezwa katika vifaa hivyo.

Hizi ni silaha mojawapo katika kundi la silaha zinazoitwa Directed Energy Weapons (DEW), nyingine ya silaha katika kundi hili zitakuwa ni za microwaves, particle beams na sound beams.

Jinsi gani silaha za laser zitabadilisha sanaa ya vita?
Ikiwa zitafanikiwa kwa kiwango kikubwa wale watakaokua wanazimiliki watapata faida kubwa katika vita kwa sababu watakuwa wana uwezo wa kuharibu ufanyaji kazi wa silaha, nyenzo na vifaa vingi muhimu vya kijeshi vya kisasa vinavyowasaidia wanajeshi katika mapambano, hii ina maana kitisho cha silaha kama za roketi na makombora kitapunguzwa sana na hivyo matokeo ya vita yataamuliwa zaidi na silaha za karibu kama bunduki na mapambano ya karibu ya moja kwa moja ya wanajeshi katika uwanja wa vita.

Nani anaongoza mbio za kuzipata silaha hizi?

Tangu mwaka 1999 Marekani walizitizama silaha za DEW kama teknolojia ya juu zaidi ya silaha katika karne ya 21 na Pentagon wakaanza kutengewa bajeti ya kufanya utafiti na kuanza kutengeneza silaha za aina hiyo za majaribio madogo madogo.

Baada ya majaribio madogo ya muda mrefu hatimaye Pentagon waliwapa kandarasi ya kutengeneza silaha kubwa makampuni mawili ya silaha ya Boeing na General Atomics Aeronautical Systems(GA-ASI). Majaribio ya kwanza ya silaha kubwa za kilowat 300 za laser yanatarajiwa kufanyika kuanzia mwaka 2022.

Matokeo yoyote ya majaribio hayo utakuwa mwanzo mwingine wa mchuano mkali wa mashindano ya silaha "arm race". Teknolojia inazidi kuwalipa walioamua kufikiri na kutazama mbele ya wakati siku zote.
 
Habari mbaya sana kwa Bwana Mavodka hii,Maana vita ya chini hajiwezi kabisa,Ukraine tu imemkalia kooni mpaka anasajili Mamaluki kutoka Syria.
Mrusi binadamu wa tofauti usikute anayo kama ilivyomkuta mmarekani kwenye hypersonic,marekani kafanya majaribio ya hypersonic yakafeli juzi mrusi kaungurumisha kwa ufanisi mpaka jicho likamtoka.
 
Habari mbaya sana kwa Bwana Mavodka hii,Maana vita ya chini hajiwezi kabisa,Ukraine tu imemkalia kooni mpaka anasajili Mamaluki kutoka Syria.
Javelin kifaa cha begani kiliyabomoa yale mavifaru hadi aibu. Na jamaa alivyo na stock ya makombora hii habari mbaya mno kwake. I can see ndio maana US wala hana time kiviiile na Kiduku na ujuaji wake wa kizamani. Anajua dawa yake imewiva; huenda akawa testing ground ya laser.
 
Javelin kifaa cha begani kiliyabomoa yale mavifaru hadi aibu. Na jamaa alivyo na stock ya makombora hii habari mbaya mno kwake. I can see ndio maana US wala hana time kiviiile na Kiduku na ujuaji wake wa kizamani. Anajua dawa yake imewiva; huenda akawa testing ground ya laser.
Ulimwengu wa sasa teknolojia ndio silaha kuu, mtu kama Kiduku anatesa wananchi bure tu kuwalaza njaa ili atengeneze hayo mavyuma yake ambayo baadae hayatakuwa na kazi.
 
Hypersonic missiles ni missiles za aina gani?
Zinatofautiana vipi na missiles nyingine?
Mrusi binadamu wa tofauti usikute anayo kama ilivyomkuta mmarekani kwenye hypersonic,marekani kafanya majaribio ya hypersonic yakafeli juzi mrusi kaungurumisha kwa ufanisi mpaka jicho likamtoka
 
Javelin kifaa cha begani kiliyabomoa yale mavifaru hadi aibu. Na jamaa alivyo na stock ya makombora hii habari mbaya mno kwake. I can see ndio maana US wala hana time kiviiile na Kiduku na ujuaji wake wa kizamani. Anajua dawa yake imewiva; huenda akawa testing ground ya laser.
Ngoja waje Waumba silaha wa Russia wakupinge na nadharia zao za kusadikika.
 
Mrusi binadamu wa tofauti usikute anayo kama ilivyomkuta mmarekani kwenye hypersonic,marekani kafanya majaribio ya hypersonic yakafeli juzi mrusi kaungurumisha kwa ufanisi mpaka jicho likamtoka
Marekani wanayo Arrow 3 kwa kushirikiana na wayahudi, hii ni teknolojia ya kupoteza makombora hasa ya masafa marefu balltic,

Hata Turkey last year ameingia mkopo wa kuiweka hii tek ktkkulinda anga lake

Na Germany majuzi hapa walikuwa wanafikiria kuikopa hii tek ...ambayo kwa saa ina gharimu USD Trilioni 1
 
Sisi bado tunatafuta magaidi wa kubumba au tumeacha.

Mimi nashauri kwamba tuachane kabisa na somo la sayansi kwa sababu halina kabisa maana yoyote kwetu na tunawapotezea watoto wetu muda bure tu.

Sisi tunasoma hilo somo la sayansi ili iweje. Sayansi ni utafiti na sisi hata siku moja serikali haijawahi kutoa hata senti tano kuwekeza kwenye utafiti kwanza sisi hatuna kitu kinachoitwa utafiti.

Kwa nchi zilizoendelea sayansi wanasoma Block Study kama asilimia 10 tu na zingine 90 wako field watu wanafanya utafiti na matokeo yake ndio hayo tunayoyaona. Sisi tunawangisha watoto vichwa bure tu na sayansi ya maigizo.
 
Screenshot_20220401-162626.jpg
FPNS316XwAw2Rd4.jpg
 
Mrusi anayo tayari. Ni moja ya silaha Sita mpya walizozindua mwaka 2018, fuatilia utajua. Ni moja ya vitu vinavyompa Putin jeuri dhidi ya Marekani. Putin kasisitiza wapo mbele kwa takribani miaka kumi mpaka wapinzani wao wawakute katika eneo hilo.
 
Javelin kifaa cha begani kiliyabomoa yale mavifaru hadi aibu. Na jamaa alivyo na stock ya makombora hii habari mbaya mno kwake. I can see ndio maana US wala hana time kiviiile na Kiduku na ujuaji wake wa kizamani. Anajua dawa yake imewiva; huenda akawa testing ground ya laser.
Hio ni technology ya zamani sana wote wanazo. Russia inaitwa Kornet. Tena ina shabaha ndefu kuliko za USA. Baadhi walitumia Hizbolah wa Lebanon kuharibu vifaru Aina ya merkava vya Israel 2006.
 
Back
Top Bottom