...sikwambii.....

...sikwambii.....

Kaunga

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2010
Posts
12,529
Reaction score
13,502
Sikwambii jinsi ya kuwa mama wa kiafrika, kwani tayari wewe ni mama tena Mwafrika
Sikwambii jinsi ya kulea mwanao, kwani kila mtoto ni unique
Sikwambii jinsi ya kutunza nyumba yako, kwani sijui kilichopo nyumbani mwako
Sikwambii jinsi ya kuishi maisha yako kwani Mungu KAKUAMINI na kukukabidhi maisha yako.

Sikwambii jinsi ya kuishi na mumeo, kwani huyo si mume wangu
Sikwambii jinsi ya kumwandalia chakula, kwani sijui mapendeleo yake
Sikwambii jinsi ya kuwa naye faragha, kwani ni ya wawili ya faraghani
Sikwambii jinsi ya kuishi maisha yako, kwani Mungu KAKUAMINI na kukukabidhi maisha yako.

Sikwambii ukashop wapi, kwani sijui mahitaji yako
Sikwambii uanze na kipi, kwani sijui uwezo wala matamanio yako
Sikwambii wahitaji nini, kwani mimi si mmiliki wa maisha yako
Sikwambii uishi vipi, kwani Mungu KAKUAMINI na kukukabidhi maisha yako.

Sikwambii; sio kwasababu sitaki, bali kwakuwa SIJUI
Sikwambii; sio kwasababu mchoyo, bali kwakuwa sitaki KUKUPOTOSHA
Sikwambii; sio kwasababu sijali, bali kwakuwa si MNAFIKI
Sikwambii kwakuwa naamini UNAJUA kwani Mungu KAKUAMINI na kukukabidhi maisha yako.

.....Love you all and wishing you prosperity 2013 all the way to 3013.....
 
Sasa huo si uchoyo wa kutokuambiana????
Happy new year Kaunga na wadau wote mtaocoment hapa wishing all of you a prosperity 2013
 
Last edited by a moderator:
Sasa huo si uchoyo wa kutokuambiana????
Happy new year Kaunga na wadau wote mtaocoment hapa wishing all of you a prosperity 2013

Hahaha, sio uchoyo amu; nimesema sitaki kukupotosha, kwani nikikwambia nitakupa uzoefu wangu uliojaa mistakes na madudu kibao!

The same to you dear.
 
Last edited by a moderator:
niambie jinsi ya kuishi na mume wangu, kwani huyo ni mume wako pia
niambie jinsi ya kumwandalia chakula, kwani wajua mapendeleo yake
niambie jinsi ya kuwa naye faragha, kwani ulishawai kuwa nae
niambie Kaunga niambie.kwani mwenzio nitaumbuka
 
Last edited by a moderator:
niambie jinsi ya kuishi na mume wangu, kwani huyo ni mume wako pia
niambie jinsi ya kumwandalia chakula, kwani wajua mapendeleo yake
niambie jinsi ya kuwa naye faragha, kwani ulishawai kuwa nae
niambie Kaunga niambie.kwani mwenzio nitaumbuka

yaani huu ujumbe ungeutoa live, pangechimbika!
Kaunga, sikujua wifi ni malenga. Afadhali utuletee gene hiyo manake we are hopeless kwenye hii fani.
 
Last edited by a moderator:
yaani huu ujumbe ungeutoa live, pangechimbika!
Kaunga, sikujua wifi ni malenga. Afadhali utuletee gene hiyo manake we are hopeless kwenye hii fani.
ahaa pachimbike nini tena? wanasema ni wako akiwa kwako akitoka nje si wako madameee!
 
Nice one mkuu. Ukipigwa msasa utakuwa mzuri zaidi.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
niambie jinsi ya kuishi na mume wangu, kwani huyo ni mume wako pia
niambie jinsi ya kumwandalia chakula, kwani wajua mapendeleo yake
niambie jinsi ya kuwa naye faragha, kwani ulishawai kuwa nae
niambie Kaunga niambie.kwani mwenzio nitaumbuka

Amenishinda huyo mume, ndio maana nikakwachia.
Kazidisha ugumegume, kila chakula adandia.
Ya chumbani tena usiombe, hadi kanichefua.
Bora tumia wako ufundi, huenda mkaendana!
 
Last edited by a moderator:
yaani huu ujumbe ungeutoa live, pangechimbika!
Kaunga, sikujua wifi ni malenga. Afadhali utuletee gene hiyo manake we are hopeless kwenye hii fani.

Halafu muache, nimemuona haishi kwa profile ya my Eiyer. Usis sio kwenye mume! LOL

Honestly, najaribu tu. Happy New Year ma Wii.
 
Last edited by a moderator:
Nice one mkuu. Ukipigwa msasa utakuwa mzuri zaidi.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Thanks, niambie basi niboreshe wapi.
Lkn ujumbe umeupata? Trust in yourself this 2013, coz Mungu kaku-trust with your life!
 
Asante Kaunga. 2013 I'll believe in myself! Happy New Year!
 
Last edited by a moderator:
Halafu muache, nimemuona haishi kwa profile ya my Eiyer. Usis sio kwenye mume! LOL

Honestly, najaribu tu. Happy New Year ma Wii.
kaka Eiyer sina wasiwasi nae. Muache ajigonge weeh akimaliza hana kucha za dole gumba. Relax, if you love something let it go. If it comes back, make sure unakuwa haupo.
 
Last edited by a moderator:
Thanks, niambie basi niboreshe wapi.
Lkn ujumbe umeupata? Trust in yourself this 2013, coz Mungu kaku-trust with your life!

Ujumbe nimeupata mkuu. I will trust in myself 2013 because God has trusted me with my life.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Asante Kaunga. 2013 I'll believe in myself! Happy New Year!

Thanks hny,
God believes in you does it matter if l don't. That is a way to go girl; you are the best n in control no matter what the rest of us say!
 
Last edited by a moderator:
kaka Eiyer sina wasiwasi nae. Muache ajigonge weeh akimaliza hana kucha za dole gumba. Relax, if you love something let it go. If it comes back, make sure unakuwa haupo.

.....If it comes back, make sure unakuwa haupo...... Amen!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom