mcshonde
Member
- Jul 15, 2022
- 66
- 154
Kutoka nchini Zambia, mwanaume mmoja amerudi nyumbani kwake na kumfumania mke wake wa ndoa akiwa chumbani na mwanaume mwingine. Mwanamke huyo ambaye ni mjamzito alikuwa akivunja amri ya sita na mwanaume anayedaiwa kuwa ni mchungaji (kutokana na picha zake zilizosambaa zikimwonyesha akiwa madhabahuni).
Katika chumba hicho, mume wa mtu akapigwa na kitu kingine kizito baada ya kuona mazingira ya kiganga yaliyokuwa yanaendelea; tunguli, vibuyu, mishumaa na unga unga ukionekana chumbani humo. Hata hivyo haijajulikana mwisho wake umekuwaje lakini wengi wameshtushwa na namna "ibada" hiyo ilivyojumuishwa na ngono.
Tukio hili linanirudisha nyuma sana, maelfu ya miaka kabla Yesu hajazaliwa. Huko mashariki ya kati, mwanamke aitwaye Yezebeli mke wa mfalme Ahabu. Malkia huyu alishiriki vyema kuisambaza dini ya mungu baali ambapo waliabudu kwa aina nyingi ikiwemo kufanya ngono (ritual sex).
Ingawa natambua uwepo wa aina ya madhehebu haya "rituals" sikujua uhalisia wake kwa mazingira yetu.
Katika chumba hicho, mume wa mtu akapigwa na kitu kingine kizito baada ya kuona mazingira ya kiganga yaliyokuwa yanaendelea; tunguli, vibuyu, mishumaa na unga unga ukionekana chumbani humo. Hata hivyo haijajulikana mwisho wake umekuwaje lakini wengi wameshtushwa na namna "ibada" hiyo ilivyojumuishwa na ngono.
Tukio hili linanirudisha nyuma sana, maelfu ya miaka kabla Yesu hajazaliwa. Huko mashariki ya kati, mwanamke aitwaye Yezebeli mke wa mfalme Ahabu. Malkia huyu alishiriki vyema kuisambaza dini ya mungu baali ambapo waliabudu kwa aina nyingi ikiwemo kufanya ngono (ritual sex).
Ingawa natambua uwepo wa aina ya madhehebu haya "rituals" sikujua uhalisia wake kwa mazingira yetu.