Siku za Hussein Bashe ndani ya CCM zinahesabika!

Siku za Hussein Bashe ndani ya CCM zinahesabika!

Ukweli ni jambo zuri sana kulisema, lakini uzalendo ni kitu bora zaidi kuliko kitu chochote kile.

Hussein Bashe wewe uko ndani ya CCM na ajabu wewe unaongoza kwa kuiponda CCM kuliko hata ambavyo unaviponda vyama vya upinzani. Katika siasa tabia kama hii haikubaliki hata kidogo.

Wana CCM tumekuwa tukikufuatilia kwa karibu sana, na matamko yako, yanaonesha wazi kabisa wewe siyo mzalendo kwa chama chako kilichokulea mpaka kukufikisha hapo ulipofika.

Inawezekana madai yako yakawa na ukweli ama la; lakini namna unavyoyawasilisha na mahali unapoyawasilisha siyo sahihi hata kidogo. Sidhani kama Mwenyekiti ataendelea kukuvumilia. Mimi nikiwa kama mwanachama wa CCM nimekerwa sana na matamshi yako unayoyatoa bungeni. Acha kutafuta cheap publicity!

Bashe wewe ni msaliti, tena inaonekana unatumiwa na CHADEMA sababu ulikuwa swahiba wa Lowassa. You are a traitor! You are a mole and you have to be removed!

Nakushauri Mwenyekiti wangu mpendwa na Rais wetu, ndugu John Pombe Magufuli, muondoe haraka sana huyu kijana ndani ya chama chetu sababu sasa ameshaota MAPEMBE. Bashe ni hatari sana kwa mustakabali wa chama chetu (CCM).

Hakuna chama chochote kile cha siasa hapa Tanzania ambacho kingemvumilia mwanachama kama BASHE! Mifano ipo mingi sana.

Mbaya zaidi anayoyaongea Bashe bungeni hayana faida yoyote ile kwa wananchi wa jimbo lake! Kazi yako Bashe ni kuwawakilisha wapiga kura wa NZEGA na siyo kupigana na CCM na serikali yake!

Mheshimiwa Rais; naomba uunde kamati maalumu ndani ya CCM kwa ajili ya kumchunguza huyu bwana mdogo. Anakoelekea siko kabisa na hatufai tena ndani ya chama chetu.

Mimi nina uhakika wa 90% hata kama tukimfukuza uanachama huyu msaliti BASHE, jimbo la NZEGA bado tutalichukua. Wakati ni sasa!

By Son of Gamba.
Mpuuzi wewe usiwajaze watu woga wa kiliberali
 
Huenda ukawa unamuona si mfia chama, lkn sie tunamuona ni mzalendo kwa nchi yake.
Wana siasa wanajua sana kucheza na akili za wapiga kura. Juma Nkamia aliwahi kusema siongei na mbwa isipokuwa mwenye mbwa.....

Bashe ndio mwanzilishi wa move iliyoshindwa 2012 kumpunguzia madaraka Mwenyekiti. Ingefanikiwa ingemneemesha nani?

Naangalia siasa kwa mshangao sana
 
Sasa wewe son of Gamba hebu sema. BASHE ni mbunge halafu hutaki aongelee issues bungeni eti akaongelee kwenye vikao vya chama unadhani akili yako ipo sawa? Moja ya kazi za bunge ni kuisimamia Serikali je unadhani kuisimamia kwenye nini? Mbona nyie ccm mnajiona mnahaki miliki ya nchi. Yaani hujisikii aibu kumpangia cha kuongea kijana mwenzako tena aliyepewa ridhaa na wananchi?

Haya kwani anayoikosoa serikali je? Anaionea au ni kweli? Watu hawatekwi? Hawauawi? Sasa ww unapuuza haya la muhimu kwako chama?? Ndo maana kuna mtu amekuita ww muumiani mnyonya damu
 
Haijalishi kupoteza jimbo. Hivi madaktari wakikuambia mkono wako una kansa na ili hiyo kansa isisambae mwilini ni lazima huo mkono ukatwe. Wewe utaamua nini?

Sisi kama wanaCCM tuko tayari kuindoa kansa BASHE, hata kama tutapoteza jimbo.
Kweli mmenyweshwa maji ya bendera kama wenzeu washabiki wa Lowasa. Ni hatari kweli kwa hii nchi kuendelea na tabia kama hizi. Mtu akisema ukweli anaitwa msaliti, tuliyaona haya kwa Zitto Kabwe sasa yamerudi kwa Bashe na na CCM. Kweli tuna njia ndefu
 
Katika kumvua mwanachama uanachama wake, MWENYEKITI ndiye mwenye kauli ya mwisho.

Mnavunja mpaka katiba ya chama chenu wenyewe.. Hebu lete kifungu kinachosema Mwenyekiti ndio mwenye kauli ya mwisho kwenye kumvua uanachama mwanachama, na sio either kamati kuu au mkutano mkuu wa chama..
 
Unamfungulia kesi nani kama polisi hao ndio wametumika kukutisha/kukunyamazisha? Polisi wamepewa namba ngapi na mrejesho ni upi?
Na ni wapi pameandikwa polisi wakifanya uchunguzi mtu mwingine haruhusiwi kuzungumza au unamaanisha jambo likiwa mahakamani?
Kwako wewe maendeleo yanakwamishwa na wabunge kusema kuna hatari ya utekaji usiokuwa wa kawaida unaendelea? Na mbunge mzuri ni yule anayesifia serikali tu ika akikosoa anapoteza muda.
Hakuna mtu wa kuikwamisha serikali kama kweli imeamua kwenda mbele, wabunge hawa wameshiriki kupitisha bajeti zote bila kuzipinga japo hazitekelezeki. Sasa nini kimeikwamisha serikali kwenda mbele?

Kwahiyo, wewe unaposikiliza mambo haya ya kuichafua serikali ya raisi John Magufuli kwamba inateka na kutisha raia wake unakubaliana nayo?
 
Ukweli ni jambo zuri sana kulisema, lakini uzalendo ni kitu bora zaidi kuliko kitu chochote kile.

Hussein Bashe wewe uko ndani ya CCM na ajabu wewe unaongoza kwa kuiponda CCM kuliko hata ambavyo unaviponda vyama vya upinzani. Katika siasa tabia kama hii haikubaliki hata kidogo.

Wana CCM tumekuwa tukikufuatilia kwa karibu sana, na matamko yako, yanaonesha wazi kabisa wewe siyo mzalendo kwa chama chako kilichokulea mpaka kukufikisha hapo ulipofika.

Inawezekana madai yako yakawa na ukweli ama la; lakini namna unavyoyawasilisha na mahali unapoyawasilisha siyo sahihi hata kidogo. Sidhani kama Mwenyekiti ataendelea kukuvumilia. Mimi nikiwa kama mwanachama wa CCM nimekerwa sana na matamshi yako unayoyatoa bungeni. Acha kutafuta cheap publicity!

Bashe wewe ni msaliti, tena inaonekana unatumiwa na CHADEMA sababu ulikuwa swahiba wa Lowassa. You are a traitor! You are a mole and you have to be removed!

Nakushauri Mwenyekiti wangu mpendwa na Rais wetu, ndugu John Pombe Magufuli, muondoe haraka sana huyu kijana ndani ya chama chetu sababu sasa ameshaota MAPEMBE. Bashe ni hatari sana kwa mustakabali wa chama chetu (CCM).

Hakuna chama chochote kile cha siasa hapa Tanzania ambacho kingemvumilia mwanachama kama BASHE! Mifano ipo mingi sana.

Mbaya zaidi anayoyaongea Bashe bungeni hayana faida yoyote ile kwa wananchi wa jimbo lake! Kazi yako Bashe ni kuwawakilisha wapiga kura wa NZEGA na siyo kupigana na CCM na serikali yake!

Mheshimiwa Rais; naomba uunde kamati maalumu ndani ya CCM kwa ajili ya kumchunguza huyu bwana mdogo. Anakoelekea siko kabisa na hatufai tena ndani ya chama chetu.

Mimi nina uhakika wa 90% hata kama tukimfukuza uanachama huyu msaliti BASHE, jimbo la NZEGA bado tutalichukua. Wakati ni sasa!

By Son of Gamba.
BASHE NI MSALITI NDANI CCM. THE EARLIER THEY KICK HIM OUT THE BETTER !
 
Ni bora kuwa UKAWA kuliko kuwa CCM punguani na zuzu fata upepo.
 
Mzalendo wa Chama na mzalendo kwa nchi yake bila kujali chama yupi bora Bashe anaitendea haki Elimu yake ni mda wa kupitisha Rasimu ya walioba mgombea binafsi vyama vinatukwamisha
 
Tawi lake lianze mkakati wa kuchukuwa kadi yao kwa sababu watakazoona zinafaa kwa mujibu wa katiba ya ccm.
Kama hawana sababu wamvumilie na wawe wamejfunza. Vinginevyo aendelee kupambana na wababe wake mpaka ataacha tu kama alivyoacha ulimboka. Torture Works said Dolnad Trump
 
Kweli mmenyweshwa maji ya bendera kama wenzeu washabiki wa Lowasa. Ni hatari kweli kwa hii nchi kuendelea na tabia kama hizi. Mtu akisema ukweli anaitwa msaliti, tuliyaona haya kwa Zitto Kabwe sasa yamerudi kwa Bashe na na CCM. Kweli tuna njia ndefu
Hatumkatazi Bashe kukikosoa chama, lakini anapaswa kupima kile anachokiongea nini impact yake? Yeye kama mbunge amekuwa akijikita zaidi sana kwa wapinzani jambo ambalo siyo zuri kwa mustakabali wa chama chetu.

Kama alitishiwa kwanini asiwasilishe malalamiko yake kwa waziri wa mambo ya ndani ambaye yupo naye kila siku hapo bungeni? Kulikuwa na ulazima gani wa yeye kuropoka bungeni kama akina Zito Kabwe?
 
Back
Top Bottom