Siku yangu inavyomalizika kwa bahati

Siku yangu inavyomalizika kwa bahati

Mkuu mpenzi wangu hajui ila anakuja mwezi ujao likizo nitamueleza kila kitu...Mama ndiye alinishauri nimrudishe Dar ili ajifungulie huku hivyo anaweza kua msaada kumueleza Mpenzi wangu maana anajulikana na ni Mwanamke smart sana....anapita humu Jf najua leo akisoma huu uzi atahisi kitu kama kweli amenifuatilia leo.
Kuwa smart na mambo ya hisia za mapenzi ni tofauti. Kila la kheri!
 
Mungu akubariki Sana Sana... Pia akawe Mwamuzi kati yako na Mpenzio kwa Lolote litakalotokea.. Wanao na uzao wako kwa ujumla ukapate kuwa Baraka tele na pia Muwe Baraka kwa Kila Mtu...
 
Mkuu hongera sana kwa kuwa na moyo wa kutoa na kusaidia, ubarikiwe sana,

Lakini sasa, kwa mpenzi wako jitahidi uwe wa kwanza kumweleza kuhusu hili, akijua mwenyewe au akiambiwa na mtu mwingine asie wewe, utapata tabu sana, narudia tena utapata tabu sana,

LA MUHIMU ZAIDI,
Endelea kumsaidia huyo binti na mtoto wake, lakini jaribu kuwa makini nae, pia nashauri ukae mbali kidogo.
Unafahamu, kwa namna ulivyomsaidia bila masharti yeye ndani anatamani kulipa fadhila japo kidogo.
Na kwa hali aliyonayo kitu pekee anaweza kulipa ni ngono. Kama atakuwa karibu na anaweza kushawishika kukutega katika hilo ili kulipa fadhira au hata kutamani kumpindua mpenzi wako akitamani hizo huduma azipate peke yake milele. Na wengi huenda mbali mpaka kutumia ushirikina. Yameshatokea sana. Yakitokea kwako utapata tabu sana.

Usitengeneze mazingira ya kumfanya atamani kulipa fadhila au kumpandisha kihisia au kumtamanisha akaanza kukutazama kwa mtazamo mwingine.
Kuna watu walitoa fadhila zikageuka madhila.
 
Pongezi sana kwako ,mwenyezi mungu akujazie zaidi pale ulipopunguza ,nakuombea heri na mafanikio zaidi wew ni zaidi ya binadamu

Mungu akubariki
 
Muoe huyo binti mlee mtoto wenu
Hongera sana mkuu kwa moyo huo
Naona special bond kati yako na huyo binti
 
Umefanya jambo jema ila kasoro naona kukubali jina lako kutumika. Tumshukuru tu mzungu kwa DNA vinginevyo balaa lake lingekua zito kwa huyo mpenzi wako na pia binadam sio wema kama wewe, unaeza kuja kuta huyo bint siku akajakugeuka kichomi kwa maana alitumia jina lako kwenye kadi ya klinik bila kukupa taarifa huwezi jua motive aliyokua nayo nyuma yake.
 
Mkuu kosa la kwanza hujamuambia mpenzi wako

Kosa la pili mama yako na dada yako wapo karibu na uliyemsaidia na wanafuraha kama ni mwanao wa kumzaa hii hali itamuumiza mpenzi wako japo anaweza asikwambie ila itayumbisha mahusiano yenu.

Wewe ni baba mlezi tu,baba mzazi akiibuka haki zako zitapungua.

Anyway hongera kwa moyo wa kusaidia kinachofata ni mpango wa yeye kujitegemea zaidi(kiuchumi) ili kukupa uhuru wa kulinda penzi lako kwa uliye naye bila kujigawanya
 
Wakuu ndo nimerudi nyumbani....

Naomba nijibu hapa kwa wote.

1.Lengo la kumsaidia huyu binti halikua hisia za mapenzi,na ndo maana anafahamu mimi nina mke(japo ni mchumba ila yeye anajua mke).Hivyo niwaambie humu kama nitalala nae hautakua tena msaada sitakua na tofauti na aliyempa mimba na kuikataa.

2.Hili jambo sikutaka kulifanya siri ndo maana watu wangu wote wa karibu nimewaambia,ila sikumwambia mpenzi wangu kwa sababu yuko mbali na kama unavyojua siwezi semea moyo wake angelipokea vipi.

3.Kuna mdau hapo alisema nimuoe,hilo halitawezekana hata kidogo mimi na mtu niliyenae kwenye mahusiano tuna miaka 9 kwenye uhusiano na muelekeo wetu unaelekea sehemu ya kuhitimisha kwa ndoa...huyu binti niliye nae nakiri hapa hadharani nikimpoteza itanichukua tena miaka 9 kumpata wa aina yake.

4.Najua itamuuma kwa mara ya kwanza lakini narudia tena mwanamke niliye nae ni smart sana ,kuna mambo mazito yalitokea zaidi ya hili na yakapita na tuko imara.

5.Kuhusu ukaribu wa dada na mama ,baada ya kujua kilichotokea ikabidi tu nao watoe sapoti na ukweli mama yangu ameguswa zaidi pengine kuliko mimi....hivyo hata ikitokea mchumba ataelewa vibaya ataelewesha na kama atakataa kuamini(japo naamini atakubali) nadhani hilo litabaki tatizo lake na si langu.

6.kuhusu umiliki wa mtoto,,nakili wazi sio wangu nimejitolea tu hivyo hata akitokea baba yake huko baadae mimi sina tatizo la msingi mimi nimetimiza wajibu wangu.


Nb:
Mtoto ni mzuri na ana afya tele...atakaa kwa dada kwa mwezi wote na baada ya hapo atarudi kwao makambako na huduma nitatoa akiwa huko...wakuu kwenye kila kitu hakikosi mapungufu lakini wakati nakutana nae pengine nisingefanya msaada wowote angeweza hata kuondoa uhai wake,,

Yote kwa yote nashukur sana kwa pongezi zenu na pia waliokosoa na kunishauri nimepokea na nakili kama binadamu hakuna kilichokosa upungufu namo nimeyapokea yote na kwenye uhitaji wa kurekebisha nitarekebisha.

Bado napokea majina.
 
Back
Top Bottom