Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

Kama mungu angeihesabu sabato ni ya kupumzika tungeshaakufa wote maana we jiulize akipumzika mungu kuna atakaye baki kweli
Hiyo ni akili yako

Mimi nimeandika alichosema Mungu na kukiandika kwa "chanda cha kidole chake"... mwenyewe


Amri ya nne (kutoka 20 :8-11)
 
Ni sawa hiyo uliyo nukuru ni Biblia takatifu tafsiri ya kiswahili cha zamani.... Hiyo iliyoandikwa majina ya siku ni Biblia takatifu tafsiri ya kiswahili cha kisasa
Kiswahili gani cha zamani ambapo hakukuwa na neno jumapili, jumatatu hadi jumamosi!? Je unajua hadi Biblia kutafsiriwa kwa lugha ya kiswahili haya maneno ya jumapili hadi jumamosi tayari yalikuwa yanatumiwa kwenye lugha ya kiswahili!? Je hiyo Biblia ya habari njema ilitafsiriwa mwaka gani ambapo majina ya siku yalianza kutumika kwenye lugha ya kiswahili!?
 
Kiswahili gani cha zamani ambapo hakukuwa na neno jumapili, jumatatu hadi jumamosi!? Je unajua hadi Biblia kutafsiriwa kwa lugha ya kiswahili haya maneno ya jumapili hadi jumamosi tayari yalikuwa yanatumiwa kwenye lugha ya kiswahili!? Je hiyo Biblia ya habari njema ilitafsiriwa mwaka gani ambapo majina ya siku yalianza kutumika kwenye lugha ya kiswahili!?
Hayo ni maswali ya kijinga...

Unamaanisha hiyo biblia haipo au kama unadhani waliyoiandika wameikosea waulize maana inatumiwa sana na wakatoliki

Usiulize kila kitu hivyo unaonyesha uvivu wa kutafiti mambo

Tafuta huko then rudi na concrete evidence kwamba.. "hiyo biblia haipo"
 
Mi nataka niwaulize tu wasabato wa humu ndani jambo hili

Kwa kutumia maadhimisho ya ijumaa kuu na pasaka mnapata uhakika kua sabato ni jumamosi... Je, hii inamaanisha maadhimisho haya ni sahihi? Kama ni sahihi kwa nini hamuadhimishi pamoja na sisi maadhimisho hayo japo kwa namna yenu (maana kwenu sisi ni wapagani), na kama so sahihi mnayatumiaje kama rejea zenu?
 
Hayo ni maswali ya kijinga...
Huenda ni kweli maswali ya kijinga ndo maana yanataka elimu ya kuelimisha ili huu ujinga utoweke, kwa hiyo haya maswali ya kijinga yanahitaji elimu please naomba ujibu
Unamaanisha hiyo biblia haipo au kama unadhani waliyoiandika wameikosea waulize maana inatumiwa sana na wakatoliki

Usiulize kila kitu hivyo unaonyesha uvivu wa kutafiti mambo

Tafuta huko then rudi na concrete evidence kwamba.. "hiyo biblia haipo"
Kwa hiyo ninyi wasabato mnatumia Biblia ya wakatoriki!? Si ndo maana yake!? Kama ni sawa basi ninyi nyote mmebaka Biblia kwa kisingizio cha lugha ya kiswahili kwa kuingiza maneno yenu na kisha kuleta upotoshaji juu ya uwepo wa siku za jumapili hadi jumamosi kwenye Biblia
 
Naomba usome marko 2:27
Angalia yesu anakujibu vyema kwamba mwanadamu hakufanyika kwa ajili ya sabato
Nadhani kuna kitu yesu alikiona ambacho kinawasumbua wengi
Kwasababu yesu alisema pia
Yeye hakuja kuitangua torati
Ila kuitimiliza
Yesu aliikuta sabato
Lakini palikuwa na mapungufu
Na asingalikuja yesu sabato
Ingaliendelea
 
Mateso ya yesu yalianza ijumaa siku ya tatu akafufuka hiyo siku ndio tunaikumbuka ni siku ya ukombozi wetu aliouahidi mungu
 
KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"
Hahahaha!!!! umechukulia ushaid kwa nakanisa ambayo huwa mnayaponda.......Kama tukifuata cku za kidunia basi SABATO ni siku ya IJUMAA..........kwa kuwa Biblia haijataja siku so kila mtu ana SABATO YAKE ilimlad tu ufanye kazi siku sita na siku ya saba upumzike(Ufanye sala kwa Muumba wako)
 
Naomba usome marko 2:27
Angalia yesu anakujibu vyema kwamba mwanadamu hakufanyika kwa ajili ya sabato
Nadhani kuna kitu yesu alikiona ambacho kinawasumbua wengi
Kwasababu yesu alisema pia
Yeye hakuja kuitangua torati
Ila kuitimiliza
Yesu aliikuta sabato
Lakini palikuwa na mapungufu
Na asingalikuja yesu sabato
Ingaliendelea
Kwa hiyo akaifuta?

Mbona wewe mwenyewe umesema kuwa.. hakuja kutangua TORATI?

... wanadamu hawakufanyika kwa ajili ya Sabato... Maana yake ni.. "Sabato haikupaswa kuwa mzigo kama wayahudi walivyoichukulia".. Sisi tunatunza Sabato yenye maboresho ya Yesu

Yesu ni kielelezo cha usabato wetu
 
Ni jambo lisilo na shaka kuwa sabato ni siku ya jumamosi ila chenye shaka ktk ulimwengu wa leo wa kiimani ni kwamba waitii amri hii ya Mungu ama wasiitii,,,

Dunia ya leo hamna wa kupinga kuwa sabato ni jumamosi ila watu wanachomiss ni kutambua kuwa sabato ni amri na utaratibu wa Mungu uliowekwa toka bustani eden na baadae kukumbushiwa pale mlimani Sinai kutoka 20:8 na baadae utaratibu huu ukaendelea kudumishwa na Yesu hata na mitume na kanisa la awali baada ya Yesu kupaa pia ni biblia hiyo hiyo inatuarifu kupitia kwa nabii Isaya 66:23 kuwa hadi kule mbinguni ibada itakuwa siku ya sabato

Watu hawafanyi ibada kwa kutii maagizo ya Mungu ila wanatii taratibu za wanadamu ambazo si salama kwao kufanya ibada isiyo na utii maana kabla ya ujio wa Yesu kutakuwa na makundi mawili moja linalofanya kwa utii kwa Mungu na jingine kwa kuongeza uchakachuzi na hapo kutakuwa na kundi lenye chapa ya mnyama yaani lisilo na utii kwa Mungu na jingine lenye muhuri wa Mungu kama tu ilivyokuwa kwa kaini na Abel, wote walitoa sadaka ila utii na unyenyekevu ukaleta tofauti
N napinga.....Sabato ni siku ya saba na si jumamosi............!
 
Huenda ni kweli maswali ya kijinga ndo maana yanataka elimu ya kuelimisha ili huu ujinga utoweke, kwa hiyo haya maswali ya kijinga yanahitaji elimu please naomba ujibu

Kwa hiyo ninyi wasabato mnatumia Biblia ya wakatoriki!? Si ndo maana yake!? Kama ni sawa basi ninyi nyote mmebaka Biblia kwa kisingizio cha lugha ya kiswahili kwa kuingiza maneno yenu na kisha kuleta upotoshaji juu ya uwepo wa siku za jumapili hadi jumamosi kwenye Biblia
Nijibu swali hili kwanza ili tuendelee

Je umewahi kusikia kitu kinaitwa.. "literature review"..?
 
Hilo hata wao wanajua ni vile tu wanashupaza shingo maana hata jumapili wanayoabudu wanasema ndiyo siku Yesu aliyofufuka na maandiko yanasema siku aliyofufuka ilikuwa siku ya kwanza sasa ukihesabu toka hiyo jumapili siku ya kwanza jumamosi itakuwa ya saba

Lakini watakataa watasema hiyo ilikuwa ya wayahudi lakini ni uongo maana pale Edeni ilipoanzishwa hapakuwa na wayahudi wowote Lakini kwa maneno ya Yesu mwenyewe anasema

MK. :2:27
Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato.

Sabato ni kwa ajili ya mwanadamu na sote tu wanadamu kwa hiyo ni ya kila mmoja mtanzania, mkenya, muarabu, mhindi, na wote duniani hapa na siyo wayahudi pekee

Kwa hiyo ukiikataa uikatae kwa sababu zako binafsi lakini biblia maandiko ya haki yanasema sabato ni kwa ajili ya wanadamu
Mod.... tumevamiwa huku......Udini unataka kuingia JF
 
N napinga.....Sabato ni siku ya saba na si jumamosi............!
Hata mimi nakubaliana na wewe kuwa Sabato ni siku ya saba

Je hiyo siku ya saba inaitwaje katika KALENDA yetu ya ulimwengu wa leo?

Unaruhusiwa hata ku "Google" au kumuuliza "Padree wako"
 
Nijibu swali hili kwanza ili tuendelee

Je umewahi kusikia kitu kinaitwa.. "literature review"..?
Mkuu, masuala ya literature review yanaingiaje kwenye Biblia!? Kuanzia mwanzo wa thread yako umejitanabahisha kutumia Biblia, kama unataka tuingie kwenye literature review anzisha thread nyingine inayohusu literature review nitakuja kuchangia we fanya kunitag tu, vinginevyo kama umeshindwa kujibu maswali yangu unaweza kukausha tu sio ya lazima sana
 
Ndugu soma waebrania 10:1-4 katika sabato yaliandamana na hayo kuitii sabato haikuwakamilisha ndio maana ukisoma yohana 4:24 haisomeki kwamba wamwabuo baba katika sabato aa bali wamwabuduo ktk roho na kweli
 
Mkuu, masuala ya literature review yanaingiaje kwenye Biblia!? Kuanzia mwanzo wa thread yako umejitanabahisha kutumia Biblia, kama unataka tuingie kwenye literature review anzisha thread nyingine inayohusu literature review nitakuja kuchangia we fanya kunitag tu, vinginevyo kama umeshindwa kujibu maswali yangu unaweza kukausha tu sio ya lazima sana
Kwa hiyo kumbe hayo maandiko yanayotumika humu kusapoti hoja siyo literature review?

Nilikuuliza swali hilo ili nikuulize tena kwamba..

Hivi nikitumia maandiko ya bibiana inayotumiwa na wakatoliki lazima niwe naitumia pia?

Au je inaondoa facts kwamba hiyo biblia inakubaliana na hoja kwamba siku ya saba ni juma ni Jumamosi?
 
Ndugu soma waebrania 10:1-4 katika sabato yaliandamana na hayo kuitii sabato haikuwakamilisha ndio maana ukisoma yohana 4:24 haisomeki kwamba wamwabuo baba katika sabato aa bali wamwabuduo ktk roho na kweli
Swali moja kwako ambalo nilikuuliza hapo juu na haujalijibu

Je Amri ya nne (kutoka 20 :8-11) ilifutwa?
 
Back
Top Bottom