Siku ya nne sijampigia mpenzi wangu

Siku ya nne sijampigia mpenzi wangu

Mlanje

Senior Member
Joined
May 16, 2013
Posts
141
Reaction score
77
Wakuu natumaini wote wazima humu ndani,nina mpenzi wangu anasoma chuo kimoja huko mkoani mimi nipo Dar.

Usiku wa tarehe 1 nilimpigia muda wa saa 4 usiku na simu yake muda wote iliita bila kupokelewa,nilimtafuta mara nyingi na baadae nikaamua kulala,ilipofika saa 6 usiku alinitafuta na nilipomwuliza kwanini hakupokea simu alidai alikuwa darasani na aliweka simu silent coz anajiandaa na mitihani ya kumaliza semester.

Nilimkumbusha kuwa tulikubaliana asiweke simu silent na kwanini amevunja makubaliano?.Aliamua kunikatia simu na kuzima kitendo kilichoniudhi sana.Sikujali sana maana sikutaka kumkera kipindi hiki cha mitihani asubuhi nilimpigia hakupokea tena,mchana nilimpigia hakupokea na nikasema akikuta missed calls zangu atanitafuta hakufanya hivyo na mimi niliamua kukaa kimya mpaka sasa.

Kiukweli nampenda sana huyu msichana na leo nimemkumbuka sana ila sitaki kumtafuta maana nitampa kichwa kwa kuruhusu aendelee kufanya makosa zaidi,nishaurini nifanyeje pia samahani kwa kuwachosha kwa maneno mengi na naombeni msitumie matusi kuchangia maana ni vyema tukaheshimiana.
 
Endelea kuuchuna ndio heshima itakuwepo mkuu.... Huyo msichana ameshagundua kuwa unampenda sana ndio maana anakufanyia kiburi... Hata kama umemkumbuka kaa kimya mpaka aanze kukutafuta yeye! Ukimpigia tu ujue atakufanya msukuke wake na atakuendesha kama gari bovu!
 
sidhani kama kungalipo mapenzi apo cha msingi kaa kmya na utafte altenative hapo mda si mrefu itakuwa hstoria! Kupenda si kaz ila kumpata akupendae kaka!
 
Wakati huohuo tafuta kipapuchi kingine cha kukuliwaza
 
tafuta substute yake uone atakavyojirudi kwenye mstari akiogopa kusugua bench !!!!!
 
kuwa na demu anae soma chuo ni kupoteza mda, labda usubiri akimaliza ndio mapenz yata endelea,
watoto wachuo wana mapenzi ya kitoto pia wanapenda sana ngono na mapenzi ya tamthilia (drama)...na kama upo mko tofauti na anao soma ndio kabsaa umeliwa.
 
Endelea kuuchuna ndio heshima itakuwepo mkuu.... Huyo msichana ameshagundua kuwa unampenda sana ndio maana anakufanyia kiburi... Hata kama umemkumbuka kaa kimya mpaka aanze kukutafuta yeye! Ukimpigia tu ujue atakufanya msukuke wake na atakuendesha kama gari bovu!

i like jf bhana,,,,,where pipo dare to talk openly,,,,
hii theory huwa naitumia sana na inafanya kazi
 
Give it time...yeye ndio mkosaji kwahio ukijipeleka kichwakichwa ujue imekula kwako!Atarudi tu kukuomba msamaha!
 
kuwa na demu anae soma chuo ni kupoteza mda, labda usubiri akimaliza ndio mapenz yata endelea,
watoto wachuo wana mapenzi ya kitoto pia wanapenda sana ngono na mapenzi ya tamthilia (drama)...na kama upo mko tofauti na anao soma ndio kabsaa umeliwa.
  • Hili ni tatizo na wengi wao husahau waliko toka, na kuishi masiha ya kuiga zaidi.
 
Endelea kuuchuna ndio heshima itakuwepo mkuu.... Huyo msichana ameshagundua kuwa unampenda sana ndio maana anakufanyia kiburi... Hata kama umemkumbuka kaa kimya mpaka aanze kukutafuta yeye! Ukimpigia tu ujue atakufanya msukuke wake na atakuendesha kama gari bovu!

Na huu ndo ushauri uufanyie kazi!
Km una umhim kwake atakutafuta,ukiona kimya,kashapata mtu huyo!
...na wala usimtafute jikaze kiume,piga kimya!
 
Mkuu fanya hivi pia mwambie afunguke muulize kama amepata mtu akuambie ili msipotezeane muda hili ndio litakalokusaidia zaidi unaweza ukaendelea kukaa kimya kumbe mwenzetu wazidi kuumia ni heri kujua kulikoni ili ufanye mipango mingine!mpigie ongea kwa ukakamavu ukimuuliza vitu hivyo unaweza kujifanya umeuchuna kumbe wazidi kuteseka kupenda ni mchezo hatari sana!
 
Mkuu fanya hivi pia mwambie afunguke muulize kama amepata mtu akuambie ili msipotezeane muda hili ndio litakalokusaidia zaidi unaweza ukaendelea kukaa kimya kumbe mwenzetu wazidi kuumia ni heri kujua kulikoni ili ufanye mipango mingine!mpigie ongea kwa ukakamavu ukimuuliza vitu hivyo unaweza kujifanya umeuchuna kumbe wazidi kuteseka kupenda ni mchezo hatari sana!
Hili ni neno,mwanangu mchana live hawa viumbe wanajisahau sana hicho ni kipimo kama anakupenda kweli au magomashi,kama anakupenda Kweli atakutafuta ukikuta kmya jua wauongo tafuta secretary wake akupoze roho jembe!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom