Sokwe Mjanja
JF-Expert Member
- Jul 16, 2009
- 575
- 298
Kaka kubali unampenda sana huyu dada na ni wewe ndio unahangaika sasa, usisikilize maneno ya watu nakukanya, watu wapo kwenye computer zao wanakwambia endelea kuuchuna wakati wewe unaumia, wenzako wako na wapenzi wao poa tu! By the way mbona inawezekana wewe ndio umeshamwagwa hapo kaka, kwa mazingira hayo wala usilete ukidume hapo, yeye ndio hapokei simu zako na wala hakutafuti, hayo ya kusema utampa kichwa zaidi au ukimtafuta ataendelea kufanya makosa zaidi yanatoka wapi ndugu yangu, hakikisha kwanza bado ni wako ndio useme haya. Ni kama alikuwa anakutafutia sababu tu huyo na ameshakata kamba huyo kaka.