Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,454
- 32,980
SIKU SHEIKH ROCKET ALIPOPIGA ADHANA MBILI MOJA KIBLA MASJID BADAWY NA NYINGINE NDANI SOKO MJINGA KISUTU
Sikupata kujua wala kuwaza kwa bali kuwa rafiki yangu mmoja alikuwa rafiki wa Sheikh Rocket tena rafiki yake wa kukaa, kuzungumza, kutembeleana nyumbani na kula pamoja.
Huyu sahib wangu ni Mhandisi wa sifa na kajenga majumba ya yanayopamba jiji la Dar es Salaam.
Amemfahamu Sheikh Rocket Masjid Badawy yeye bado kijana mdogo.
Huyu sahib wangu wa miaka mingi toka udogoni yeye kanipa mengi ya Sheikh Rocket lakini kwa sasa napenda niliweke hili moja hadharani sote tufaidi nami sitatia mkono wangu nitakiweka In Shaa Allah kisa hiki kama alivyoniandikia:
''Siku moja, enzi za Msikiti wa Badawiy ukitazamana na soko la Kisutu, aliadhini adhana kwa ajili ya swala ya Adhuhuri msikitini.
Alipomaliza akaenda kusimama katikati sokoni Kisutu akaadhini.
Alipomaliza akawaambia watu wa sokoni: " Msishangae, nimekuja kujivua dhima, msije mkasema hamkusikia nilipoadhini msikitini.
Maana nyinyi wengine hapa hizi nyanya, vitunguu, maboga nk. ndiyo miungu yenu.
Kama si hivyo twendeni tukaswali."
Inasemekana kuna baadhi walimfuata na wakadumu na swala.
Sikupata kujua wala kuwaza kwa bali kuwa rafiki yangu mmoja alikuwa rafiki wa Sheikh Rocket tena rafiki yake wa kukaa, kuzungumza, kutembeleana nyumbani na kula pamoja.
Huyu sahib wangu ni Mhandisi wa sifa na kajenga majumba ya yanayopamba jiji la Dar es Salaam.
Amemfahamu Sheikh Rocket Masjid Badawy yeye bado kijana mdogo.
Huyu sahib wangu wa miaka mingi toka udogoni yeye kanipa mengi ya Sheikh Rocket lakini kwa sasa napenda niliweke hili moja hadharani sote tufaidi nami sitatia mkono wangu nitakiweka In Shaa Allah kisa hiki kama alivyoniandikia:
''Siku moja, enzi za Msikiti wa Badawiy ukitazamana na soko la Kisutu, aliadhini adhana kwa ajili ya swala ya Adhuhuri msikitini.
Alipomaliza akaenda kusimama katikati sokoni Kisutu akaadhini.
Alipomaliza akawaambia watu wa sokoni: " Msishangae, nimekuja kujivua dhima, msije mkasema hamkusikia nilipoadhini msikitini.
Maana nyinyi wengine hapa hizi nyanya, vitunguu, maboga nk. ndiyo miungu yenu.
Kama si hivyo twendeni tukaswali."
Inasemekana kuna baadhi walimfuata na wakadumu na swala.