Siku hizi undugu ni ‘overrated’

Hii nayo inasikitisha yaani wewe uliyetoka kimaisha kushirikiana na ndugu zako unaona kama wanakurudisha nyuma??🤣

Aliyekuwa bado na maisha magumu matuamaini yake yako kwa ndugu zake wenye nafuu ya maisha. Hata ungekuwa wewe imungekuwa katika nafasi hiyo.
Kiukweli ndugu wengine ni wavivu. Au wamefanya maamuzi mabaya ya maisha kama kuzembea shuleni au kuchezea fursa. Mfano aliamua kuzaa watoto 7 na hana uwezo au Alipata hela ya maana akaichezea kwa starehe. Mimi nimepambana na kufanya maamuzi ya ku-sacrifice hadi nikatoboa. Halafu wao wale dezo.

Mimi namshukuru Mungu lakini pia nilipambana sana. Na hakuna ndugu aliyenisaidia zaidi ya mama mzazi. Baba alifariki nikiwa mdogo. Kwa hio nao wapambane tu na hali zao.
 
Bado kuna ndugu hasa wa Baba na Mama mmoja wanasaidiana sana kwenye shida na raha.
 
I thank God bado tuna ishi kijamaa na ndugu zangu tuna saidiana kwa yaliyo ndani ya uwezo
 
Ndugu mliokulia nyumba 1 au eneo moja, mara nyingi mna vitu vya kushea, memories.
Nakumbuka zamani wengi walikuwa wanatokea kijiji kimoja, watu wameoleana, bond ilikuwa strong!
Siku hizi mfumo wa maisha watu wamezaliwa maeneo tofauti, wamesoma maeneo tofauti, wakaajiriwa maeneo tofauti, wakaoa maeneo tofauti..huo ukaribu wa undugu utaupataje??

Lazima popote ulipo hata ugenini uwe na jirani, rafiki na watu wa karibu..uko U.S. mfano au Nanjilinjili, kwenu asili Bukoba, ukipata tatizo hadi mtu wa Bukoba akusaidie ni ngumu.

Ndugu tutazidi kutakutana kwenye misiba na harusi..

Undugu siyo kufanana bali kufaana!

Everyday is Saturday.......................... :cool:
 
Hao wazungu unaosema sijui ni wazungu wa wapi. Wacha kujificha kwa wazungu kwa kuwa wanandugu zako wana roho za kutu. Nina marafiki zangu wamekuja kuwekeza miradi ya hotel. Jamaa alipofika mahali fedha ikamuishia alinambia ana kaka yake mtoto wa baba yake mdogo atamuazima kama dolar elfu 30 hivi amalizie mradi wake. Binafsi nimeweza kukaa na watu hawa wanapendana mno.

Tazama wahindi walivyo na upendo wao kwa wao. Yaani unaenda kwa familia ya muhindi unakuta nyumba ya vyumba vitano kuna ishi humo mtu kama 50 hivi. Wote ni ndugu na mwenye kipato( mhindi mwenye duka lake kariakoo) ni mmoja tu. Na anawalea wote na kuwatunza.

Twende kwa Warabu sasa. Yaanu haw ani noma. Mmoja akikosa mtaji wanamchangia na yeye anafanya biashara. Yaani hukuti kuna boya kwenye familia. Hata kama hakusoma lakini utakuta ana japo banda la spare za pikipiki.

Huku kwa waafrika sasa. Duuh ndio kama hayo. Ambayo na weww unayaendeleza kwa kisingizio kilekile.

Huwezi ukafananisha maisha ya Mwafrika na za wazungu, waarabu, wahindi nk. bila kuongelea generational wealth (kizazi kurithi mali na pesa toka kwa mababu/mabibi) na Black Tax.

1591045832477.png


Huyo mwenye uwezo wa kumpa mwenzake dola elfu 30,000 unafikiri ni mtu anaetegemea mshahara wa kazi ya kawaida?? Minimum wage ya huko marekani kwa mfano ni chini ya dola $8 kwa saa na bado hajakatwa taxes. Hawa watu pia hawalipii shule mpaka labda chuo au kama wanatake mtoto aende private school. Huku kwetu ni kuanzia primary.

Huko marekani kwa mfano, watu weusi walikuwa hawaruhusiwi kumiliki mali/ardhi, kwahiyo tunaona matokeo yake sasa bado wanajitahidi kujinyanyua kutoka kwenye umaskini. Hapa Afrika kwa mfano kama Babu alikuwa mkulima ana wake wawili, kila mke akazaa watoto 8 kipindi hicho kilikuwa kitu cha kawaida; watoto wanazaliwa wengi , wanaenda kulima, maisha yanaendelea. Hakuna cha shule wala nini, kama ni shule mradi ujue kusoma na kuandika. Sasa maisha yakabadilika, na kwasababu first born kaenda shule, ndugu zake woooote 15 wanamuangalia wawasaidie, na hapo hapo kuna wazee wengine wanne wakutunza wakizeeka. Hii ndio tunaita Black Tax. Kipato chako kinarudi kusaidia wengine, mambo yako unashindwa kuyafanyia kazi sababu umeelemewa na majukumu .

Kwahiyo sidhani kwamba undugu ni overrated, bali tumegundua kuwa ukitaka kuishi maisha mazuri bila kuelemewa, inabidi kuwa selective, saidia ndugu zako . Jamaa watasaidiana na ndugu zao, kila mtu apambane na hali yake.
 
Huwezi ukafananisha maisha ya Mwafrika na za wazungu, waarabu, wahindi nk. bila kuongelea generational wealth (kizazi kurithi mali na pesa toka kwa mababu/mabibi) na Black Tax.

View attachment 1466161

Huyo mwenye uwezo wa kumpa mwenzake dola elfu 30,000 unafikiri ni mtu anaetegemea mshahara wa kazi ya kawaida?? Minimum wage ya huko marekani kwa mfano ni chini ya dola $8 kwa saa na bado hajakatwa taxes. Hawa watu pia hawalipii shule mpaka labda chuo au kama wanatake mtoto aende private school. Huku kwetu ni kuanzia primary.

Huko marekani kwa mfano, watu weusi walikuwa hawaruhusiwi kumiliki mali/ardhi, kwahiyo tunaona matokeo yake sasa bado wanajitahidi kujinyanyua kutoka kwenye umaskini. Hapa Afrika kwa mfano kama Babu alikuwa mkulima ana wake wawili, kila mke akazaa watoto 8 kipindi hicho kilikuwa kitu cha kawaida; watoto wanazaliwa wengi , wanaenda kulima, maisha yanaendelea. Hakuna cha shule wala nini, kama ni shule mradi ujue kusoma na kuandika. Sasa maisha yakabadilika, na kwasababu first born kaenda shule, ndugu zake woooote 15 wanamuangalia wawasaidie, na hapo hapo kuna wazee wengine wanne wakutunza wakizeeka. Hii ndio tunaita Black Tax. Kipato chako kinarudi kusaidia wengine, mambo yako unashindwa kuyafanyia kazi sababu umeelemewa na majukumu .

Kwahiyo sidhani kwamba undugu ni overrated, bali tumegundua kuwa ukitaka kuishi maisha mazuri bila kuelemewa, inabidi kuwa selective, saidia ndugu zako . Jamaa watasaidiana na ndugu zao, kila mtu apambane na hali yake.
Na haiji wealth ya kuja kurithisha jamaa zako badae haiji hivi hivi lazima kuwe na coorperation. Inaanza taratibu lakini kwa mawazo haya tunayoona ya umimi bado hatutafika popote. Hata hao wanaopeana dola elfu 30 usizani waliziokota chini wamehangaikia pia.
 
Huwezi ukafananisha maisha ya Mwafrika na za wazungu, waarabu, wahindi nk. bila kuongelea generational wealth (kizazi kurithi mali na pesa toka kwa mababu/mabibi) na Black Tax.

View attachment 1466161

Huyo mwenye uwezo wa kumpa mwenzake dola elfu 30,000 unafikiri ni mtu anaetegemea mshahara wa kazi ya kawaida?? Minimum wage ya huko marekani kwa mfano ni chini ya dola $8 kwa saa na bado hajakatwa taxes. Hawa watu pia hawalipii shule mpaka labda chuo au kama wanatake mtoto aende private school. Huku kwetu ni kuanzia primary.

Huko marekani kwa mfano, watu weusi walikuwa hawaruhusiwi kumiliki mali/ardhi, kwahiyo tunaona matokeo yake sasa bado wanajitahidi kujinyanyua kutoka kwenye umaskini. Hapa Afrika kwa mfano kama Babu alikuwa mkulima ana wake wawili, kila mke akazaa watoto 8 kipindi hicho kilikuwa kitu cha kawaida; watoto wanazaliwa wengi , wanaenda kulima, maisha yanaendelea. Hakuna cha shule wala nini, kama ni shule mradi ujue kusoma na kuandika. Sasa maisha yakabadilika, na kwasababu first born kaenda shule, ndugu zake woooote 15 wanamuangalia wawasaidie, na hapo hapo kuna wazee wengine wanne wakutunza wakizeeka. Hii ndio tunaita Black Tax. Kipato chako kinarudi kusaidia wengine, mambo yako unashindwa kuyafanyia kazi sababu umeelemewa na majukumu .

Kwahiyo sidhani kwamba undugu ni overrated, bali tumegundua kuwa ukitaka kuishi maisha mazuri bila kuelemewa, inabidi kuwa selective, saidia ndugu zako . Jamaa watasaidiana na ndugu zao, kila mtu apambane na hali yake.
Hapo kwenye kuzaa sana bila mpango naungana na wewe kwa 100%. Imechangia umaskini na utegemezi usio wa lazima. Baba mwenye kipato cha mfano laki nne kwa mwezi na yuko kijijini au mkoani kwenye maisha nafuu. Anaweza kuweka akiba kila mwezi na kukuza mtaji au mali. Lakini kutokana unakuta ana wake wawili na watoto nane hiyo laki nne si kitu si lolote. Anatarajia watoto wakue ndio wasaidiane kulisha na kusomesha wenzao. Umaskini unarudi pale pale generatio after generation. Inakuwa vicious cycle.
 
Ndugu mliokulia nyumba 1 au eneo moja, mara nyingi mna vitu vya kushea, memories.
Nakumbuka zamani wengi walikuwa wanatokea kijiji kimoja, watu wameoleana, bond ilikuwa strong!
Siku hizi mfumo wa maisha watu wamezaliwa maeneo tofauti, wamesoma maeneo tofauti, wakaajiriwa maeneo tofauti, wakaoa maeneo tofauti..huo ukaribu wa undugu utaupataje??

Lazima popote ulipo hata ugenini uwe na jirani, rafiki na watu wa karibu..uko U.S. mfano au Nanjilinjili, kwenu asili Bukoba, ukipata tatizo hadi mtu wa Bukoba akusaidie ni ngumu.

Ndugu tutazidi kutakutana kwenye misiba na harusi..

Undugu siyo kufanana bali kufaana!

Everyday is Saturday.......................... :cool:
Point
 
inategemea bhana. malezi yanachangia. kuna watu wanakuzwa kushirikiana yani hadi kuwaona ni furaha sana. ila mtazamo wa mtu hutokana na njia zipi alipitia katika makuzi na ni vipi aliaminishwa. familia zenye mshikamano bila unafiki zipo nyingi tu ni vile hatu/hawapostiani.
 
M
Mimi mbona ndugu yangu ndo aliyeninyanyua pale nilipojua mimi ni mgeni sana hapa duniani. Au kisa tupo wachache tu (3)!

Hao ndugu zenu inabidi mkapime DNA, labda bi'mkubwa alimpiga changa la macho mzee. Ndugu yako ni yule mliyetoka naye tumbo moja tu.
May be mpo wachache ndo maana mnathaminiana sana ktk nyakati hizi,kwangu mimi yote aliyoorodhesha mtoa mada yanaakisi maisha yangu na ndugu zangu.
Sikatai kwamba ktk kunikuza ndugu wamenisaidia ile uko home sembe inapikwa na unakaa chini unakipiga cha ugali ila baada tu ya umri fulan unachiwa kila kitu upambane kivyako hata msaada wa kimawazo ama kifedha unapotea mwisho wa siku unakutana na marafiki wanakupiga kampani ya kutosha mpaka unatoboa hapo ndipo uhasama unapoanzi na ndugu,na ni pale tu kila mtu anapozingatia mafanikio ya familia yake binafsi.
Kwangu rafiki ana mchango mkubwa sana ktk mafanikio yangu.
 
Walichobakiza ndugu wa sasa ni kunafikiana na kuchekana, inasikitisha sana.
Sure,unapofeli ktk mambo yako utachekwa na kusemwa vibaya kinyama utadhani hata msaada walikupatia na kama walikupa msaada ukajisahau kuto fadhira basi utasimangwa mpaka ukajuta kwanini walikusaidia.
 
watz tumekul
Tambua:

Siku hizi sio kama zamani ambapo undugu ulikuwa na thamani, damu ilikuwa nzito kuliko maji.

Siku hizi unaweza ukawa na braza hapa mjini msionane miaka miwili na msipigiane simu.

Siku hizi kila mtu ana time zake tu wanaita 'kuendana na kasi ya mheshimiwa'

Siku hizi rafiki na mchepuko wana nafasi kubwa kuliko ndugu.

Zamani matatizo ya ndugu yako ni matatizo yako lakini sikuizi kila mtu 'anapambana na hali yake'Undugu uliobaki ni mke, mume na watoto.

Lakini Kaka, Dada, Mjomba, Shangazi, Binamu imeshapitwa na wakati.

Maisha sasa hivi kila mtu yuko bize na maisha yake kutafuta vya kwake tu.

In short teknolojia ilileta ustaarabu na ndiyo inayouondoa.
ia mifumo ya kijamaa
na hili alileta baba wa taifa..
sasa mzoee ya ulimwengu..umekuta wenzetu kenya wanalalamika..kule ni kazi kazii tu,,undugu mpaka uwe na ishu..sio mambo ya kutembeleana sijui kuwekeana kambi..njoo ukiwa na ishu..
ukitaka uwe na ukaribu kama rafiki au mchepuko njoo tupeane deal..sio kuja kumaliza mpunga kwangu afu huna ishu na hapo juu umesema maisha yanaenda kasi,,nawew changamka shwaiiin...
 
NDUGU NI YULE ALIYEKO MAISHANI MWAKO SIKU ZOTE BILA KUJALI MNA SHARE BABA AU MAMA AU DAMU.

my testimony:
Kwa mama yangu nilizaliwa first born.mama akaolewa na mume mwingine kisha mm nikapelekwa kwa ma mkubwa na baadae baba akanichukua nikiwa mdogo bado sijaanza hata class 1 nikalelewa na mama wa kufikia (i love this woman to death) pamoja na ndugu zangu nilowakuta hapo home tume share baba..
Baadae mama huko alipoolewa akazaa mtoto wa kike (mdogo angu) baadae akafariki 1998 nikiwa std 4.
Baadae mume wa mama akahamia kwao bukoba baada ya mama kufarik na ukawa ndio mwisho wa kumskia dogo alikua na months tu.Hata mwaka hakua amefika.

Nimekuja kuanza kumskia 2015 kuwa ameolewa arusha.Nikafunga safar mpaka huko nikamtafuta nikampata kwakua nilipata namba yake ya cm.Nikamuona ashakua kua mtu mzima.Ana mwanae tayar na mume

Tukawa tunawasilianA but kwakwel honestly SI FEEL ule uzito wa undugu baina yetu licha ya ku share tumbo 1.
Ofcz najitahid kuwasiliana nae lakin unaona kabisa una struggle ku make it happen.Na jins anavyonichukulia mm kama kaka yake ni tofaut kabisaa na anavyowa treat kaka zake aliolelewa nao japo hawazaliwa tumbo moja ila wame share baba (mama mama alipoolewa huko alikuta mumewe ana mtoto wa kiume tayar makamo yangu though kanizid kidogo).Yko close nao zaid kuliko mm

Lakin mimi pia i feel the same. hawa ndugu zangu tulio share baba na kukua pamoj ndio haswa nawaona ndugu kwel kwel.
 
Sahihi kabisa mimi binafsi bado najuta hadi leo kwa kuwa ilipita fursa sikuweza kumsaidi mdogo wangu wa kike. Alimaliza form four wakati huo mimi niko chuo na nilikuwa nasomesha wagmdogi zangu wengine wengi hivi kama watano hivi. Wakati huo kipato changu kilikuwa kidogo. Nilimweleza kuwa anisubirie kama mwaka hivi ili hali yangu ikiwa nzuri nitampeleka shule. Dogo wangu wa kike akanisikiliza akaendea kumsaidia mama kulima huko kijijini.

At the end miaka miwili ikapita mambo yangu bado tight na huku nina mzigo mwingine wa madogo. Mwisho wa siku mdogo wangu yule akapata mchumba. Akaniambia kaka nimesubiri sana msaada wako lakini naona bado naomba uniruhusu nieolewe. Basi nikamruhusu kwa uchungu sana. Hadi leo ana watoto watatu . Furaha yangu ilikuwa nimsomeshe apate maisha mazuri kwenye maisha yake.

Watu wanaona Ulaya ndugu wana maisha mazuri wanadhani yalijitengeneza. Hapana wanainuana. Undugu ni kusaidiana.kutokana na Choyo ya waafrika sasa wanasingizia Ulaya ya wazungu eti hakuna undugu ili wawatenge ndugu zao.

Wazungu wanapendana mno.
Hii imenitoa chozi...hali yake uko alikoolewa vip?
 
Back
Top Bottom