Siku hizi undugu ni ‘overrated’

Siku hizi undugu ni ‘overrated’

Mcqueenen

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2019
Posts
7,316
Reaction score
12,768
Tambua:

Siku hizi sio kama zamani ambapo undugu ulikuwa na thamani, damu ilikuwa nzito kuliko maji.

Siku hizi unaweza ukawa na braza hapa mjini msionane miaka miwili na msipigiane simu.

Siku hizi kila mtu ana time zake tu wanaita 'kuendana na kasi ya mheshimiwa'

Siku hizi rafiki na mchepuko wana nafasi kubwa kuliko ndugu.

Zamani matatizo ya ndugu yako ni matatizo yako lakini sikuizi kila mtu 'anapambana na hali yake'Undugu uliobaki ni mke, mume na watoto.

Lakini Kaka, Dada, Mjomba, Shangazi, Binamu imeshapitwa na wakati.

Maisha sasa hivi kila mtu yuko bize na maisha yake kutafuta vya kwake tu.

In short teknolojia ilileta ustaarabu na ndiyo inayouondoa.
 
Tusisingizi teknolojia, tatizo ni sisi wenyewe.

Hebu jiulize wewe binafsi ni jambo gani linalo kuzuia kumthamini ndugu yako?

Kumjulia hali ndugu yako hata kwa kumpigia simu?

Kumtembelea ndugu yako?

Kama kila mmoja atajiuliza yeye binafsi tutagundua tatizo ni sisi wenyewe.
 
Mimi mbona ndugu yangu ndo aliyeninyanyua pale nilipojua mimi ni mgeni sana hapa duniani. Au kisa tupo wachache tu (3)!

Hao ndugu zenu inabidi mkapime DNA, labda bi'mkubwa alimpiga changa la macho mzee. Ndugu yako ni yule mliyetoka naye tumbo moja tu.
 
Njaa inauma... chunga usichinje nyau... Ukisha fikisha 18 yrs wewe ni sovereigh state ni free jiongeze acha kutegemea ndugu nayeye ana yake acha lawama...ujamaa umeisha long sasa hivi kila mtu anajiangalia mwenyewe
 
kwahyo wazungu wana maswala ya kiukoo kama huku?
Yani mara kikao cha ukoo etc.
Misiba ya watu 300+??? Wanayo?

Ninaamini US mtoto anaweza akazaliwa mpaka akafa ndugu anaowajua wasizidi 10
Hata hao ndugu kumi hana pa kuwatoa...Unakuta mama mtu ana kaka yake tu..Baba mtu naye ana dada yake tu..So dogo tofauti na wazazi anakuwa anajua Uncle, Aunt, grandma na grandpa.

Kama hao Uncle na Aunt nao wanafamilia tuseme hata ya watu watatu, jumla wanakuwa 11. Ndo idadi ya watu huo ukoo...Hao wanaweza hata kutana jioni ,wakala dinner,wakajuana vema mchezo ukaisha.

Sasa huku kwetu si kuna koo zina watu karibu mia!!! Kujuana msibani hakuepukiki....Au kutembea wote ilhali nyie ni ndugu
 
Ujamaa na undugu ni chanzo kikubwa cha umaskini wetu, ukipata kinafasi kidogo utanyonyolewa hadi ujute... ukikaza tu utasemwa balaa.
Yaani acha kabisa mpango wangu mwakani nibaki na wanangu wawili tu ndugu tupa kule! kwanza wanafiki watupu unawasaidia halafu wanakusemanga! big up nyote mnaoishi na watoto wenu tu! Nuclear family ndugu kulostishana tu.
 
Back
Top Bottom