Sijawaelewa Airtel na bure yao ya WTF!

Mchumia Rungu

JF-Expert Member
Apr 26, 2013
1,434
821
Katika ulimwengu wa leo sijaona kitolewacho bure na kama kipo basi wapo waliokilipia. Hii ya Airtel na bure ya WTF naona kama ni zaidi ya wizi! Kabla huduma yao hii haijaja, kila nilipoweka kwa mfano sh. 500/= na kujiunga na kifurushi cha siku, walinipa dk 13 za kupiga mitandao yote, SMS 300 na 125M kwaajili ya mtandao wa internet.

Baada ya kuja huduma hii ya bure WTF, zile 125M kwaajili ya mtandao hazikai utakuta zimeisha ndani ya muda mfupi na kisha huduma yao inayoitwa ya bure ya WTF haipatikani tena! Hapa nafikiri kuna kawizi wanafanya ila wamekosea setting zao. Na nisilogwe nikaunga (tethering) katika computer, hizo mega byte 125 zit aishi kwa speed ya ajabu wakati awali nilikuwa nafanyia kazi kwa muda wa kutosha kabisa.

Tafadhali wadau tufahamishane kwa walioina huduma hii msaada. Natamani kufuta setting za Airtel internet lakini sijui nianze wapi. Simu ninayoitumia ni HUAWEI Y300. Sitaki kuuhama network huyu, Airtel. Nimeanza nanyi ndg zangu hapa JF lakini pia kama sitapata ufumbuzi nitawaendea wahusika ofisini kwao.

Natanguliza shukrani kwa majibu yote yatakayo kuja.
 
Wameitafsiri hapa JF, lakini kwa mujibu wa Airtel hiyo inasimama badala ya WhatsApp, Twitter na Facebook.

Duh aisee sawa asante nadhani ungeiweka wazi ndani ya bandiko lako, wengine tuko far na tv/radio za tz mkuu. TIA (thanks in advance)
 
mkuu Mchumia Rungu hebu niambie how effective hii kitu tethering ipo!!inafanyaje kazi shule kiduch kiongozi
 
Last edited by a moderator:
Duh aisee sawa asante nadhani ungeiweka wazi ndani ya bandiko lako, wengine tuko far na tv/radio za tz mkuu. TIA (thanks in advance)

Si unajua ukishakasirishwa na jambo, matokeo yake ni kudhani kuwa bila ya shaka wako na wenzako ambao wamekutwa na lililokuta! Hivyo unajimwga kihasirahasira ukijua mkishakutana na wenzako utaeleweka na ama mtalia pamoja au kufarijiana kwa lililowakuta. Kumbe habari unayotoa ina kazi zaidi ya ile unayodhamiria. Mfano hapa tayari najitambua kuwa bandiko langu linatoa pia tahadhari kwa waliotaka kuingia Airtel kama nilivyoingia. Asante pia kwa ushauri wako.
 
mkuu Mchumia Rungu hebu niambie how effective hii kitu tethering ipo!!inafanyaje kazi shule kiduch kiongozi

Mkuu inategemea ni simu gani unaitumia lakini sasa hivi simu nyingi zina mfumo huo. Badala ya kutumia modem unaweka simu yako katika mfumo huo wa tethering kisha unaunga na computer yako kama wireless. Wakati unaendelea kutumia internet kwenye computer yako, simu yako itafanya kazi kama kawaida bila kuathiri chochote katika kazi zako za computer. Kimsingi ni huduma nzuri na sasa hivi wengi wanaitumia na wamesahau modem.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu inategemea ni simu gani unaitumia lakini sasa hivi simu nyingi zina mfumo huo. Badala ya kutumia modem unaweka simu yako katika mfumo huo wa tethering kisha unaunga na computer yako kama wireless. Wakati unaendelea kutumia internet kwenye computer yako, simu yako itafanya kazi kama kawaida bila kuathiri chochote katika kazi zako za computer. Kimsingi ni huduma nzuri na sasa hivi wengi wanaitumia na wamesahau modem.
nikiangalia hapa simu yangu naona hivi:
USB tethering
PORTABLE WI-FI HOTSPOT
SET UP WI-FI HOTSPOT

HELP
je katika hizo nina anzia wapi hii kitu yangu ni xperia E

 
nikiangalia hapa simu yangu naona hivi:
USB tethering
PORTABLE WI-FI HOTSPOT
SET UP WI-FI HOTSPOT

HELP
je katika hizo nina anzia wapi hii kitu yangu ni xperia E


Mkuu nafikiri anzia hapo kwenye "SET UP WI-FI HOTSPOT"
 
Ni kweli kabisa..!! kuna wizi unaendelea hapa..!!

Hakika wizi upo. Kama mpaka Jumatatu sitapata ufumbuzi, kazi yangu ya kwanza ni kufika katika ofisi zao na kama hakitaeleweka basi siku hiyo ndiyo itakuwa siku yangu ya mwisho kutumia mtao huo. Na baada ya hapo kazi yangu itakuwa kuhamasisha (kuwakomboa) watu waachane na mtandao huo.
 
Bure ni ghali.. Usitegemee kitu cha bure kuwa Effective na Effeciency...

Pole sana..
 
Mkuu nafikiri anzia hapo kwenye "SET UP WI-FI HOTSPOT"
mkuu nashukuru nimefanikiwa kwa karibu asilimia 96!laptop inaconnect vizuri kwenye wi-fi ya simu na network strength inaonekana ni excellent ila nikifungua kitu inagoma kwenye internet hakifungui!je kuna kitu naweza kufanya zaidi?
 
mkuu nashukuru nimefanikiwa kwa karibu asilimia 96!laptop inaconnect vizuri kwenye wi-fi ya simu na network strength inaonekana ni excellent ila nikifungua kitu inagoma kwenye internet hakifungui!je kuna kitu naweza kufanya zaidi?

Hapo Mkuu nafikiri uangalie setting zako kwenye computer yako na hiyo nafikiri watu wa IT wanaweza kusaidia maana niliona jamaa mwingine alikuwa na tatizo kama hilo lakini baadae akafanikiwa. Au la keep trying mwisho mambo yanaweza kuwa sawa.
 
Bure ni ghali.. Usitegemee kitu cha bure kuwa Effective na Effeciency...

Pole sana..

Asante sana Mkuu! Hapa kinachoumiza ni udanganyifu unaofanyika. Na kama nilivyosema ulimwengu wa leo hakuna bure na kama ipo basi wako walioilipia unayodhani ni bure. Kinachosikitisha ni zile megabyte 125 kupotea ghafla ili hali mwanza nilikuwa nazitumia kwa muda mrefu!
 
Hii mitandao ni full kizungumkuti, bora mimi natumia nokia tochi sipati adha hizo za internet sijui WTF,,,,,,,,
 
Hakika wizi upo. Kama mpaka Jumatatu sitapata ufumbuzi, kazi yangu ya kwanza ni kufika katika ofisi zao na kama hakitaeleweka basi siku hiyo ndiyo itakuwa siku yangu ya mwisho kutumia mtao huo. Na baada ya hapo kazi yangu itakuwa kuhamasisha (kuwakomboa) watu waachane na mtandao huo.
Utahamia mtandao gani wakati yote ina matatizo yanayofanana?
 
Back
Top Bottom