Bome-e
JF-Expert Member
- Jan 3, 2014
- 17,187
- 26,209
Hahahaaaa,wanatafakari watoke vipi!Mkuu,cocochanel dawa imeanza kumuingia,Lizaboni kapotea kabisa
Hahahaaaa,wanatafakari watoke vipi!Mkuu,cocochanel dawa imeanza kumuingia,Lizaboni kapotea kabisa
Hapo kwenye mihemko umemlenga mwenyekiti wako wa chama.Serikali inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za nchi. Sio kwa mihemko ya Wanaharakati uchwara. Mh. Waziri Mkuu ametoa ufafanuzi juu ya suala zima la Makinikia kwa kuwa kuna wajuaji wanapotosha umma na kumwaga sumu iliyojaa chuki dhahiri.
Wenye Chuki na Nchi hii endeleeni na upotoshaji. Ila mwisho wenu ni AIBU.
Naweka akiba ya maneno nikisubiri ripoti ya Pili (2) kutoka TUME ya Rais. Muda utaongea.
Hamjaelewa nini kwa mfano??
Sina Chama...muulize mkeo anatambua!Hapo kwenye mihemko umemlenga mwenyekiti wako wa chama.
Kabisa kabisa.Kiki... Mbona angeweza kupokea report akiwa ofisini kwake labda akishuhudiwa na vice na PM.. Wengine woote tungeshuhudia kupitia TV
Hahahah kama kile kibabu cha Zimbabwe kilivyonyooshwaKutaka kiki kila mahali.Sasa kwa mzungu amebugi!asidhanie hii ni ishu kama ya sukari kutishia wahindi halaf baadae akaufyata.Hawa ni wenye dunia,watamnyoosha!
Mkuu huoni ripoti ya pili itakuwa based on false premises! UnategemeaninTume haijaongelea suala la makontena mangapi yanasafirishwa kwa mwezi. Labda tujadili tu usahihi wa kiwango cha dhahabu kwenye kontena moja hicho ndo tume wameongelea. Tume ya pili ndo ina majibu ya kotena ngapi zimesafirishwa. Nadhani tuna deal na secondary information kwa hiyo there is loss of information hapa katikati.. Tusubiri ripoti zote zitapokuwa available kwenye public..Mimi huwa nashangaa sana kwanini tunapenda ku make judgement kwa information ambayo ni secondary na si primary..Unakuta mtu hasomi ripoti ya kitu fulani anasubiri tu zitto afanye synthesis yake yeye anakuja anachukua secondary information from Zitto au mtu yeyote. Kwa hiyo muda mwingi tunakuwa tunapoteza muda kujadili vitu ambavyo hatujajua ukweli wake kamili...Tuweke akiba ya maneno mpaka pale tutapokuwa wote tumesoma hizo repoti na kuzielewa kisha ndo tuweze kubainisha mapungufu yake..
Yaani "HASIRA" zake zilianza zamani! Nimewahi kusikika akisema MIMI WATALIMIA MENO! Kauli anayoITEKELEZA sasa. Kama Mwalimu wa Kemia wa Advanced Level, anajua kilicho kwenye mchanga wa MADINI. Aliyataja vizuri siku ile. Inaonekana (NIKISOMA KATI YA MISITARI) Kamati ya Profesa ilipata NOTES za Mkuu, na ripoti waliyotoa ilikuwa na "majibu" ya aliyewatuma kabla ya kuanza kazi.
Yah, japo Muhongo simpendi sana kwa sababu ya academic arrogance yake, lakini kwa hili la makinikia hakutendewa haki! Alihukumiwa kwa ripoti yenye uongo mwingi kuliko ukweli!Na amuombe msamaha Prof. Mhongo.
Kukurupuka tuuuuuu!!
T. Lissu alisema nia ya Rais ni nzr but the means is wrong!! CCM wakabisha weeeeeeee
Wabunge hata wakitukanwa na mkuu, makofi kwa kwa kwa! Kujipendekeza kuna shida yakeMkuu,mimi binafsi nimemuona kupitia Star tv akijibu swali hilo na kwakweli kajibu kwa upole sana akionekana wazi kujaribi kuwapoza ACASIA.
Wabunge wa CCM kama kawaida yao makofi yakawa mengi.
Wewe ndo hujaelewa kabisa.. Tatizo UCCM umewakaa akilini, yaani hata wafanyaje wameshaharibu, tulieni tunyolewe Kwa chupa.Unaona kizungu zungu cha nini.
Tatizo mnakuwa na akili za kuambiwa mkuu wa mkoa alikwenda kuhakikisha kuwa utekekezaji wa agizo alilotoa raisi unatekelezwa.
Mbona mnaingia wenge.
Wajinga sana, Akili za Mchanga kubishana na Lissu? Yaani miaka yote wanaambiwa tunaibiwa wanabisha kwa dharau na Kebehi, eti Leo ndio wanajifanya wanauchungu na nchi yetu!! Shenztyp!!!Washaharibu Mkuu, sasa kilichobaki ni kuzuga zuga tu kinamna!
Leo katika kipindi cha bunge cha maswali ya papo kwa hapo amesema kwamba serikali haijawachukulia hatua zozote kampuni yoyote ya madini au mwekezaji kutokana na ripoti ya makinikia.
Kwamba hatua zilizochukuliwa ni za ndani tu haxiwahusu hao wawekezaji. Hivyo wasiwe na wasiwasi na waendelee na shughuli zao kama kawaida. Lengo la serikali ni.kujiridhisha tu kilichopo kwenye makinikia na bado ripoti nyingine inasubiriwa.
Akasema baada ya ripoti hiyo kutoka wstashauriana nini cha kufanya kwa kuwashirikisha wadau wote na kwa haki. Na wala hakutakuwa na tatizo kwani kila kitu kitakwenda vizuri.
Hivyo watu waache kutishana na pia wawekezaji kwenye madini watulie. Jibu hili lilitokana na swali la mbunge wa Tabora mjini aliyetaka kujua kama serikali kwa kuxuia mchanga wa makinikia haioni kwamba inawaogopesha wawekezaji na tunaweza kujikuta tunaingia kwenye mgogoro na nchi wanazotoka wawekezaji hawa hasa endapo ikija kujulikana kwamba kilichosemwa na tume si kweli?
Kiukweli kabisa jibu la Waziri Mkuu limeniacha na kizunguzungu. Ukiacha kwanza kwamba jibu lake lake limeonekana kujaribu kupooza hali ya sintofahamu iliyopo na kwamba kuna uwezekano tume ikawa ilikosea, nimeshangazwa zaidi na aliposema eti hatua zilizochikuliwa ni za ndani tu na makampuni ya madini hayajachukuliwa hatua zozote mpaka sasa na eti waendelee na shughuli zao bila wasiwasi.
Hivi ni kweli WM hakusikia mapendekezo ya Tume ya Rais kwamba Acacia wamekuwa wanatuibia sana? Tena wakashauri makontena ya mchanga yaendelee kushikiliwa mpaka watakapotulipa kodi zetu kwa kile kilichopo kwenye mchanga?
Hakumsikia rais akisema ameyakubali mapendekezo yote ya Tume? Sasa atasemaje eti serikali haijachukulia kampuni yoyote hatua na waendelee tu na shughuli zao kama kawaida?
Je, hajawasikia Acacia wakilalamika kwamba wanapata hasara ya mabilioni kila siku kwa kitendo cha kushikilia mchanga ao muda mrefu?
My take: Nahisi serikali imeshachanganyikiwa kuhusu hili la makinikia ndio maana wanaanza kutoa kauli tata!
Tone ya WM leo na tone ya Magufuli kuhusu hili sakata siku ile ya kukabidhiwa ripoti ni vitu viwili tofauti kabisa.
Naona dalili kwamba somo ambalo limekuwa likitolewa na wadau kuhusu kutokurupuka katika hili limeanza kuwaingia serikali! Kudos kwa serikali kama mmeelewa somo.
Next time mtulize vichwa kwanza kabla ya kukurupuka na maamuzi yanayoweza kuliingiza taifa kwenye hasara kubwa. Tuwape madini, halafu tuwalipe tena fidia ya mabilioni?, No way. Sio kwa kodi zetu. Mngetoa hizo pesa mifukoni mwenu wallah!!
Tatizo Serikali ilishasema inachoamini mpaka kumfukuza yule katibu mkuu aliyesema ukweli sasa leo uje Ikulu useme Rais umekosea? inabidi watengeneze report itakayo mfurahisha mheshimiwa na mpaka akawatukana wasomi wengine kama katibu sasa tutayona maana hata tone zao zimebadilika sisikii tena majambazi.Mkuu Bams una mtazamo kama wangu.
Katika moja ya michango yangu kuhusu hili sakata la makinikia nilielezea mshangao wangu kuwa inawezekana vipi watu wasomi wa kiwango kile wakakosea mahesabu kwa kiwango kikubwa kiasi kile? Hakuna hata mmoja aliyeligundua hilo kabla ya kukabidhi ripoti? Yani wawezaje kumkabidhi Rais kitu chenye makosa ya kiwango kile?
Eti tani 7.8 za dhahabu kwenye makontena 277? Yani around kilo 28 kwa kila container? Tena hiyo iwe ni 50% tu ya wanachozalisha kwa mwezi.
Nafikiri kama wangetumia standard measure ya uzito wa dhahabu ambao ni Wakia au Ounce (oz) labda wangeshtukia makosa yao. Maana tani 7.8 ni kilogramu 7,800 sawa na gramu 7,800,000. Hizi ukizibadili katika troy ounces (1oz = 31.1035g) unapata ounces 250,775. This is too much to be any mine's monthly production....
Hata kwa mwaka hakuna mgodi tulionao hapa wenye uwezo wa kuzalisha kiasi hicho.
Nakubaliana nawe....tume ishitakiwe kwa kumwongopea Rais na wananchi....na hizo Phd zao wafutiwe tu..
Kusema waendelee na shughuli zao, wakati kule ACCASIA wameambiwa wasiendelee na chochote mpaka wapate agizo jipya kutoka kwa rais..hapa ndio hapaeleweki.Hamjaelewa nini kwa mfano??