Sijamwelewa Waziri Mkuu ujue?

Duh!!!

Unaniita kwenye uzi ambao mtu anadai hajaelewa kabla hajajibiwa kajijibu anayotaka kujijibu na kujidanganya kwa kupindisha....shaaaaaa

Mimi napita sipendi udaku, alichoongea Mh. Majaliwa leo sioni utofauti na kinachoendelea.

Tabu wananchi wengi hamna subira na kupenda udaku wa kuchafua ya serikali yetu safiiii ya awamu ya Tano inayoongozwa na mpendwa Rais wetu Mh. Magufuli.

Hapa kazi tu

Nakuona unavyoyumba yumba huna pa kushika, eti serikali yetu safi ndiyo umepata pa kuegemea, awamu hii mtapata mateso sana
 
Nakuona unavyoyumba yumba huna pa kushika, eti serikali yetu safi ndiyo umepata pa kuegemea, awamu hii mtapata mateso sana

Hakuna mateso ni nyie hamoendi kusikia mazuri yake, mnapindisha tu kudanganyana.

Subirini ripoti ya pili

Hapa kazi tu
 
Mkuu Bams una mtazamo kama wangu.
Katika moja ya michango yangu kuhusu hili sakata la makinikia nilielezea mshangao wangu kuwa inawezekana vipi watu wasomi wa kiwango kile wakakosea mahesabu kwa kiwango kikubwa kiasi kile? Hakuna hata mmoja aliyeligundua hilo kabla ya kukabidhi ripoti? Yani wawezaje kumkabidhi Rais kitu chenye makosa ya kiwango kile?
Eti tani 7.8 za dhahabu kwenye makontena 277? Yani around kilo 28 kwa kila container? Tena hiyo iwe ni 50% tu ya wanachozalisha kwa mwezi.
Nafikiri kama wangetumia standard measure ya uzito wa dhahabu ambao ni Wakia au Ounce (oz) labda wangeshtukia makosa yao. Maana tani 7.8 ni kilogramu 7,800 sawa na gramu 7,800,000. Hizi ukizibadili katika troy ounces (1oz = 31.1035g) unapata ounces 250,775. This is too much to be any mine's monthly production....
Hata kwa mwaka hakuna mgodi tulionao hapa wenye uwezo wa kuzalisha kiasi hicho.
Nakubaliana nawe....tume ishitakiwe kwa kumwongopea Rais na wananchi....na hizo Phd zao wafutiwe tu..
Mimi nadhani adhabu sahihi kwao ni kunyongwa. Walipika hizo data makusudi ili kuumiza Maafisa wa serikali waliohukumiwa kuwa eti wameitia serikali hasara kubwa. Dawa hapa wasindikize hayo makontena hadi kwenye smelter yakachambuliwe tuone tutapata hayo madini waliyoyasema kwenye taarifa yao. Yasipotoka wanyongwe
 
  • Thanks
Reactions: GSL
Eeeeeeh

Unatamani niwe ivyoooo, ulitaka nitumie maneno machafu ndio uelewe I guess!!! Sio zangu hizo
Umeelewa sana ila unajifanya mbumbumbu!Kwani day 1 JPM alitukana???Umepooza kama PM alivyopooza!
 
Wamefyata!!! Haya sasa wale mliyokuwa mnashangilia mkurupuko wa Magu kwa kujifanya wazalendo, endeleeni kutoa povu. Watu wakitoa ushauri mnasema wamenunuliwa. Kweli Ccm ni laana.
 
Unajua nlikua najiuliza sana mbona km WM ameongea kwa upole sana kana kwamba sio ishu hot ambayo inasumbua nchi kwa sasa.
 
Umeelewa sana ila unajifanya mbumbumbu!Kwani day 1 JPM alitukana???Umepooza kama PM alivyopooza!

Unajitahidi na kugonga wamba tu hapa kwa Cocochanel

Wewe fata mkumbo wa mleta mada ufurahi huku ukiendelea kuisoka namba na kusaga meno.
 
Mzuka ulimpanda vibaya mpaka akajikuta anatukana!
Yaani "HASIRA" zake zilianza zamani! Nimewahi kusikika akisema MIMI WATALIMIA MENO! Kauli anayoITEKELEZA sasa. Kama Mwalimu wa Kemia wa Advanced Level, anajua kilicho kwenye mchanga wa MADINI. Aliyataja vizuri siku ile. Inaonekana (NIKISOMA KATI YA MISITARI) Kamati ya Profesa ilipata NOTES za Mkuu, na ripoti waliyotoa ilikuwa na "majibu" ya aliyewatuma kabla ya kuanza kazi.
 
Unasema watamnyoosha kama vile aikuhusu wewe wapuuzi kweli nyie labda kama nyie siyo watanzania kisa uchama wenu wa kipuuzi kabisa,ingekuwa ni amri yangu ningewafolenisha pale Taifa niwachape viboko nfufjqbveeiqb.
Unamaanisha JPM, Kikwete na Mkapa?!
 
Leo katika kipindi cha bunge cha maswali ya papo kwa hapo amesema kwamba serikali haijawachukulia hatua zozote kampuni yoyote ya madini au mwekezaji kutokana na ripoti ya makinikia.

Kwamba hatua zilizochukuliwa ni za ndani tu haxiwahusu hao wawekezaji. Hivyo wasiwe na wasiwasi na waendelee na shughuli zao kama kawaida. Lengo la serikali ni.kujiridhisha tu kilichopo kwenye makinikia na bado ripoti nyingine inasubiriwa.

Akasema baada ya ripoti hiyo kutoka wstashauriana nini cha kufanya kwa kuwashirikisha wadau wote na kwa haki. Na wala hakutakuwa na tatizo kwani kila kitu kitakwenda vizuri.



Hivyo watu waache kutishana na pia wawekezaji kwenye madini watulie. Jibu hili lilitokana na swali la mbunge wa Tabora mjini aliyetaka kujua kama serikali kwa kuxuia mchanga wa makinikia haioni kwamba inawaogopesha wawekezaji na tunaweza kujikuta tunaingia kwenye mgogoro na nchi wanazotoka wawekezaji hawa hasa endapo ikija kujulikana kwamba kilichosemwa na tume si kweli?

Kiukweli kabisa jibu la Waziri Mkuu limeniacha na kizunguzungu. Ukiacha kwanza kwamba jibu lake lake limeonekana kujaribu kupooza hali ya sintofahamu iliyopo na kwamba kuna uwezekano tume ikawa ilikosea, nimeshangazwa zaidi na aliposema eti hatua zilizochikuliwa ni za ndani tu na makampuni ya madini hayajachukuliwa hatua zozote mpaka sasa na eti waendelee na shughuli zao bila wasiwasi.

Hivi ni kweli WM hakusikia mapendekezo ya Tume ya Rais kwamba Acacia wamekuwa wanatuibia sana? Tena wakashauri makontena ya mchanga yaendelee kushikiliwa mpaka watakapotulipa kodi zetu kwa kile kilichopo kwenye mchanga?

Hakumsikia rais akisema ameyakubali mapendekezo yote ya Tume? Sasa atasemaje eti serikali haijachukulia kampuni yoyote hatua na waendelee tu na shughuli zao kama kawaida?

Je, hajawasikia Acacia wakilalamika kwamba wanapata hasara ya mabilioni kila siku kwa kitendo cha kushikilia mchanga ao muda mrefu?

My take: Nahisi serikali imeshachanganyikiwa kuhusu hili la makinikia ndio maana wanaanza kutoa kauli tata!

Tone ya WM leo na tone ya Magufuli kuhusu hili sakata siku ile ya kukabidhiwa ripoti ni vitu viwili tofauti kabisa.

Naona dalili kwamba somo ambalo limekuwa likitolewa na wadau kuhusu kutokurupuka katika hili limeanza kuwaingia serikali! Kudos kwa serikali kama mmeelewa somo.

Next time mtulize vichwa kwanza kabla ya kukurupuka na maamuzi yanayoweza kuliingiza taifa kwenye hasara kubwa. Tuwape madini, halafu tuwalipe tena fidia ya mabilioni?, No way. Sio kwa kodi zetu. Mngetoa hizo pesa mifukoni mwenu wallah!!

Kuelewa unaelewa au unautoa ufahamu kusudi? Kunamwekezaji aliyeadhibiwa?
 
Unasema watamnyoosha kama vile aikuhusu wewe wapuuzi kweli nyie labda kama nyie siyo watanzania kisa uchama wenu wa kipuuzi kabisa,ingekuwa ni amri yangu ningewafolenisha pale Taifa niwachape viboko nfufjqbveeiqb.
Acha kutukana watu.
Nani kawatuma mkafanye ujinga wenu kule?
Mnataka tuwapigie makofi kwa kututia hasara???
Pelekeni woga na kujipendekeza mbali na sisi.
 
Duh!!!

Unaniita kwenye uzi ambao mtu anadai hajaelewa kabla hajajibiwa kajijibu anayotaka kujijibu na kujidanganya kwa kupindisha....shaaaaaa

Mimi napita sipendi udaku, alichoongea Mh. Majaliwa leo sioni utofauti na kinachoendelea.

Tabu wananchi wengi hamna subira na kupenda udaku wa kuchafua ya serikali yetu safiiii ya awamu ya Tano inayoongozwa na mpendwa Rais wetu Mh. Magufuli.

Hapa kazi tu
Juzi fisiemu mkakata viuno kusheherekea hewa,
leo sijui mtaficha wapi sura zenu
 
Serikali inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za nchi. Sio kwa mihemko ya Wanaharakati uchwara. Mh. Waziri Mkuu ametoa ufafanuzi juu ya suala zima la Makinikia kwa kuwa kuna wajuaji wanapotosha umma na kumwaga sumu iliyojaa chuki dhahiri.

Wenye Chuki na Nchi hii endeleeni na upotoshaji. Ila mwisho wenu ni AIBU.
Naweka akiba ya maneno nikisubiri ripoti ya Pili (2) kutoka TUME ya Rais. Muda utaongea.
 
Back
Top Bottom