Kikao gani kiliridhia? kumbuka hizi pesa si za Chadema na kuna utaratibu rasmi uliowekwa na serikali na chama husika kukubali kuufuata kwa mujiibu wa sheria ya usajili wa vyama vya siasa.
Hivi unafikiri ingewezekana vipi yeye kwenda tu benk na kuchukua hela na kuondoka nayo bila kuridhiwa na viongozi wenzake? Kama alifanya hivyo, wewe umejuaje kwamba kuna hela alichukua? Si ndiyo hivyo vikao ambavyo na akina Shonza walihudhuria na hatimaye kutoa siri nje ya chama?
Pili ukiniambia zile siyo fedha za chadema nitakushangaa sana. Maana zile fedha ni za serikali pale zinapokuwa serikalini, na zinapokuwa mikononi mwa CHADEMA wanachadema wana utaratibu wao wa kuzipangia bajeti zikiwemo hizo program za M4C na kadharika. Lakini zaidi ya hote, hadi hivi sasa, hakuna ushahidi wa wazi kwamba Dr. Slaa alikopa hizo pesa, na kama kweli alikopa hakuna hata mmoja mwenye ushahidi dhahiri kwamba zilikuwa ni za ruzuku.
Lakini mwisho wa yote, kama alikopa ina maana zitarudishwa? Sasa tatizo ni nini? Mbona wabunge wakifika bungeni wanakopeshana magari ya milioni 200 hadi 300, itakuwaje ajabu kwa katibu wa chama naye kukopa pale ambapo panamhusu kwa ajili ya kutatua matatizo yanayomkabili? Hakuna hata mmoja kati yetu aliyeweza kueleza ni mazingira gani yaliyopeleka Dr Slaa kukopeshwa hizo hela kama kweli alikopeshwa. sasa tunapata wapi huo ujasiri wa kulalamika na kumshambulia wakati hatujui basis ya huo mkopo? Ni kwa vipi basi hatuwashambulii wabunge wetu ambao tumewachagua kwenda kuwa wasemaji wetu bungeni, badala yake wanafika huko na kukopeshana mapesa na kudai nyongeza za posho na mishahara kutoka kwenye hela ya serikali.
Mwisho nataka nikukumbushe kwamba CCM ndiyo wenye ruzuku kubwa kuliko vyama vyote nchini, unaweza kutuambia ni kazi gani wanafanyia hiyo hela? Hawana mikutano ya hadhara au operations kama zila za CHADEMA kama Sangara na M4C inayoendelea sasa. Je wanazipeleka wapi hela zao? Mabilioni kwa mabilioni? CCM wamepora viwanja, ofisi na rasilimali mbalimbali za wananchi na kuziita zao, na zinawaingizia kipato hadi hivi sasa eg uwanja wa Kirumba-Mwanza. Kumbi za mikutano kimwaga, jengo la vijana CCM Dar, ofisi zake zote, ambazo kimsingi zilijengwa kwa gharama ya wananchi wote wakati wa chama kimoja, na sasa zinatumiwa na CCM. Je wana nini wanachowafanyia wananchi kutokana na kuwa na mali zote hizo ambazo kimsingi ni za wananchi wote? Ni kwanini milioni 140 za Dr. Slaa ziwaume hivyo ilihali hamhusiki nazo? Fanyeni mambo yenu, tuacheni na chadema tufanye mambo yetu.
CC.
Nape Nnauye