Mkuu Molemo, sina tatizo na hili, tatizo langu dogo ni tofauti za uoni vs ukweli halisi!.
Kuna wakati nyumba ikipata mitikisiko, ikapata ufa, dawa ya kuuimarisha ni ama kuziba ufa ili usijenge ukuta, au sometimes ni kuibomoa na kuijenga upya, hivyo in that sense, kuziba na kubomoa zote zikawa ni kujenga!.
Uoni (point of view) ya Wanachadema wengi ni blured vision!, hawaoni kama huko juu kuna matatizo!. Kwa kutoyaina matatizo hayo, mnajiaminisha "manahodha wanaliendesha vizuri jahazi", na watawafikisha salama kwenye "destination 2015!". Sisi ambao hatumo humo ndani ya jahazi, ndio tunauona mwelekeo wa jahazi lenu!, linakwenda mrama, kama hamtakubali sio lazima kubadili manahodha, bali kubadili mwelekeo, ili kufika destination 2015 salama!. Kwa vile kosa ni la manahodha, ambao nao wako ndani ya jahazi, hawaoni kama wanakwenda mrama!, abiria nao hawajui kuwa wanapelekwa mrama!, atakayejitolea kuwa na kadira binafsi, anapotoa tahadhari kuwa "tunakwenda mrama!", "nahodha anatoa amri, atoswe baharini!" na abiria mnashangilia!.
Determinant ya usahihi wa manahodha wenu ni "the end justify the means", sisi wa pembeni tunaona kuwa hamfiki!, mnang'ang'ania mtafika!, tusiendelee kuandikia mate, 2015 itafika, kuna watakao lia na watakao cheka!, atakae lia mwisho ndio atalia sana, na atakae cheka mwisho ndio atakaye cheka sana, japo "kulia na kucheka zote ni kelele!".
Muda huo utakapofika, nitawakumbusha humu humu, tuliwaambia nini!.
Uwezo wa binadamu kufanya mambo pia ni limited kama uwezo wa uongozi!, solution ikiishafikia the point of saturation, inakuwa ni saturated solution, and it can take more than what it can!. Hao uliowataja, wamefanya kazi nzuri, ila wamefikia optimum point ya uwezo wao!, they can do no more than what they did!. Yule daktari wa Mwembe Yanga, tuyliyemtumainia siku zile, siye huyu aliye bize na "honeymoon" isiyoisha, huku aki baby sit kile kichanga kinachomuita "baba babu", kwa ngoma ya 2015 hawezi tena!, labda Kamanda kijana!.
All and all, tunasubiria, tukishuhudia, huku tukiwaeleza wazi!.
Pasco.