Siipendi hii tabia

Siipendi hii tabia

Yani mwanaume anaku ask for a date halafu yeye mwenyewe anakwambia chagua any place you want unachagua anakupeleka then anakwambia order anything you want una order zako your food and wine then yeye Ana order maji tu.

Ukimuuliza Kwann anajifanya nimeshiba halafu ukimkaribisha icho chakula anajifanya Ngoja nionje tu mwisho wa siku mnaenda pasu kwa pasu.

Yaani kaniudhi nilivoona anakula sana nikajifanya Mimi nipo kwenye diet nimeshiba, bila aibu kamaliza chote wakati before alisema ameshiba.

Jamani wanaume kujitutumua kwingine hakufai khaaaaaa .

Mtu si bora uwe mkweli tu mimi I can’t afford izo places ntakuelewa kuliko Hii embarrassment.

Nimefuta his number sitaki tena kumuona wala kuwasiliana naye.
😂😂😂😂 mwamba kama mwamba, lakini umezingua kumwacha, mgagagigikoko mwenzangu😂😂😂😂
 
Amefanya vizuri sana,kukutongoza agalimike ,kukulisha agarimike na bado kulitafuta bao agarimike safi hiyo ndo dhana bora 50/50 ameitendea haki ipasavyo coz kipindi anasulubika kubeba zege hukuwepo
 
Ila wewe pia jinga sana. Ulivyoambiwa chagua ungechagua sehemu ya bei rahisi... angalia sasa malengo yako hayajatimia... jamaa kafakamia MSOSI WA NDOTO ZAKO. Halafu wanawake mnaopenda kiswanglish huwa mnakera balaa. Mimi ningekupeleka Holiday Inn lakini ungekunywa maji tu.
Dem alizingua kwa kiasii chake...... Mwanaume akikuulza for date mwache achague eneo.... Hata akikukomalia mwambie wewe nipelk unapoona panafaa sasa yeye kachagua sehem iko expensive ama jamaa hajaikubal

Mm siamn huyo jamaa km Hana sehem nzurii za kwenda sema Dem alkuwa anapimwa tuu kisaikolojia, Men tuko very logic..... Sema kumpima Dem tuu
 
Mmeona jamani jinsi BIDHAA inavyouzwa kwa Ghali?

Hapa MUUZAJI wa BIDHAA amekasirika amekutana na MNUNUAJI ambae anauchungu na Pesa yake.

Ila Muuzaji wa BIDHAA hana CUSTOMER care nzuri alipaswa aitunze hiyo number just incase next time aweze KUVUNA/KUPUNUSA fedha za Mteja.
Kaka huyu manzi mshenzii...... Eti kafuta namba angekaa chini amuulze ata ki utani tuu Ila Mimi hapa naona jamaa Kuna kitu alkuwa anaangalia......
For mine.... Date naenda sehem nayotak mim na sio manzii...... Acha wanione mim katili
 
Nchi kama US ukitoka date na demu basi malipo ni 50-50 mademu wa kibongo akipata Boy friend ndio anaona kama amepata ajira!

Huyo Mwanaume ndio wa level yako,kama ukibahatika ukampata wa level ya juu kidogo basi na yeye atakutema.
Dem njaa huyoo hv mwanaume utoke nyumbn kabisaa unaenda date..... Afu huna ela siamin.... Kweny falsafa apo akili ya mwanaume Kuna kitu iltaka ipate from that gal..... Na inaonekn Dem hisia ndo ziko mbele kulko akili
 
Niliwahi pata kasheshe ya kufa mtu. Nilikuwa bado mgeni mgeni. Profesa wangu alikuja akanikuta nimekaa sina hili wala lile akaniambia SYB let's go grab some lunch. Sasa nikafikiri kuwa kwa vile yeye ndo kaniambia basi atakwenda kulipa bila shaka.

Tumepiga msosi tumemaliza namwona huyoo amekwenda akalipa bili yake huyoo akatoka nje kunisubirisha. Na mfukoni sikuwa hata na wallet. Kikawa kimbembe!

Ndiyo nikajifunza utamaduni wao. Hata binti ukimtoa out anakuja amejiandaa kulipa nusu labda uwe muungwana umkataze. Na hii inasaidia sana mtu kutoagiza wines ghali hizi za $100+ kisa tu kaona kuna mtu anamlipia. Nilipenda sana utamaduni wao huo.

Sisi huku ukimpata mtu limbukeni ambaye hana exposure ukampeleka sehemu ya maana basi anaona leo ndiyo kapata bahati. Ataagiza vitu ghali ambavyo angekuwa yeye ndo analipa asingevigusa.

Ila kama uko vizuri na ukamhakikishia mtu kuwa aagize cho chote, siyo vizuri tena kuja kumgeuka kama jamaa yetu alivyofanya. Na mabinti wenye uzoefu atamwacha kwanza jamaa aagize na yeye atachukua hints kutoka pale. Na kama wamezoeana anaweza tu kuuliza point blank kwamba una uhakika naweza kuagiza cho chote?
Hao watu ukiwa nao lazma akili ikukae Sawa... Ukisahau wallet once iwe bahati mbaya kweli siku nyingine mkitoka anakwambia "Don't forget your wallet honey 😄😄".... Ndalandefu anajua muda wote wallet inatema Tu, ya kwake haihusiki 😂😂
 
Hao watu ukiwa nao lazma akili ikukae Sawa... Ukisahau wallet once iwe bahati mbaya kweli siku nyingine mkitoka anakwambia "Don't forget your wallet honey 😄😄".... Ndalandefu anajua muda wote wallet inatema Tu, ya kwake haihusiki 😂😂
Na wakati mwingine anakutoa yeye na analipa kila kitu. Na anakwambia kabisa kuwa leo huna hata haja ya kubeba wallet. Wako wawazi sana na hakuna surprises. Ukimkataza anakuona kama umemdharau labda kwa vile ni mwanamke...
 
It’s not what you think
Uyu alikua ananitaka tuingie kwenye relationship ila Bado nilikua sijamkubalia
Sasa ndo akaona Sijui akisema choose any place Sijui nini ndo mm ntalainika kumbe kaharibu mwanaume yule asiejiamini
Huyo mwanaume inaonekana hata angekupeleka Hyatt regency na akakulipia kila kitu, bado ungemkatalia Strong and Fearless
 
Na wakati mwingine anakutoa yeye na analipa kila kitu. Na anakwambia kabisa kuwa leo huna hata haja ya kubeba wallet. Wako wawazi sana na hakuna surprises. Ukimkataza anakuona kama umemdharau labda kwa vile ni mwanamke...
Ukiwajulia hawa mbona utadumu nao...muda wowote unahakikisha wallet unayo ingawa unajua pasu kwa pasu ipo sometime unakaza ulipe mwenyewe usiojione MacSelemani 😂..."don't worry, it's ok baby" zitadondoka nyingi sana
 
Mpaka mwanamume akwambie uchague sehemu anajimudu.

Wewe ulikuwa unachunguzwa ni aina gani ya demu

Kwa sababu mwisho wa siku bado alilipa hizo bills

First date imeonyesha wewe ni mwanamke wa aina gani.

Wenzenu wazoefu first date huwa wanakuwa humble hawaombi nauli wala hela ya mafuta ya gari ikiwa ana usafiri hadi anachoagiza sehemu wamekutana
 
Mpaka mwanamume akwambie uchague sehemu anajimudu.

Wewe ulikuwa unachunguzwa ni aina gani ya demu

Kwa sababu mwisho wa siku bado alilipa hizo bills

First date imeonyesha wewe ni mwanamke wa aina gani.

Wenzenu wazoefu first date huwa wanakuwa humble sio kwenye nauli au mafuta ya gari ikiwa ana usafiri hadi anachoagiza sehemu wamekutana
Fact brooh..... Yaan mm nimesema Tena Men tuko very logic no matter how we are? Ila huyo Dem km ulivosema apo mtu haez toka om afu aje ale msosi wako..... Dem hata falsafa ya akili Hana njaa tupu
 
Fact brooh..... Yaan mm nimesema Tena Men tuko very logic no matter how we are? Ila huyo Dem km ulivosema apo mtu haez toka om afu aje ale msosi wako..... Dem hata falsafa ya akili Hana njaa tupu
Umesema vyema

Njaa mkuu ndio shida ya hawa mamanzi.

Hawa ndio wale ukimtoa outing atapiga picha msosi uliomlipia na kupost kwenye mitandao ya kijamii kuwatambia wenzake
 
pole sana.
Mimi mtu akitaka kunitoa out huwa namwambia anipeleke popote tu ili nijionee yeye yupo level zipi au ananichukulia wa hadhi gani.

Akinilazimisha sana nichague nampeleka kwenye machimbo ya kitimoto huko uswazi ndio ashindwe hata kunipiga sound.
 
Akina baba tujitahidi hawa binti zetu tangu wakiwa nyumbani hawajaanza kutafuta wachumba au kuolewa,

tuwapeleke maeneo yenye watafurahia outing ya kifamilia wazoee misosi na vinywaji vizuri kuepusha aibu kama hizi

Njaa zinawasumbua sana dada zetu kuna vitu wanafakamia kwa sababu hawakuwahi kuvipata wakiwa nyumbani kwa wazazi wao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom