Siipendi hii tabia

Siipendi hii tabia

Nchi kama US ukitoka date na demu basi malipo ni 50-50 mademu wa kibongo akipata Boy friend ndio anaona kama amepata ajira!

Huyo Mwanaume ndio wa level yako,kama ukibahatika ukampata wa level ya juu kidogo basi na yeye atakutema.
Niliwahi pata kasheshe ya kufa mtu. Nilikuwa bado mgeni mgeni. Profesa wangu alikuja akanikuta nimekaa sina hili wala lile akaniambia Shimba let's go grab some lunch. Sasa nikafikiri kuwa kwa vile yeye ndo kaniambia basi atakwenda kulipa bila shaka.

Tumepiga msosi tumemaliza namwona huyoo amekwenda akalipa bili yake huyoo akatoka nje kunisubirisha. Na mfukoni sikuwa hata na wallet. Kikawa kimbembe!

Ndiyo nikajifunza utamaduni wao. Hata binti ukimtoa out anakuja amejiandaa kulipa nusu labda uwe muungwana umkataze. Na hii inasaidia sana mtu kutoagiza wines ghali hizi za $100+ kisa tu kaona kuna mtu anamlipia. Nilipenda sana utamaduni wao huo.

Sisi huku ukimpata mtu limbukeni ambaye hana exposure ukampeleka sehemu ya maana basi anaona leo ndiyo kapata bahati. Ataagiza vitu ghali ambavyo angekuwa yeye ndo analipa asingevigusa.

Ila kama uko vizuri na ukamhakikishia mtu kuwa aagize cho chote, siyo vizuri tena kuja kumgeuka kama jamaa yetu alivyofanya. Na mabinti wenye uzoefu atamwacha kwanza jamaa aagize na yeye atachukua hints kutoka pale. Na kama wamezoeana anaweza tu kuuliza point blank kwamba una uhakika naweza kuagiza cho chote?
 
Mwanaume kama huyo futa namba hakufai kabisa.

Hajiamini, hana uwezo wa kuishi na wewe.pia hongera we ni mwanamke unayejielewa.

Next few wks nitakuja na series ya kuwafunda wanaume jinsi ya kuandaa mtoko wenye mafanikio kwa Mwanamke unayekutana naye kwa mara ya kwanza

Tutajadiliana vifungu vifuatavyo

1. Jinsi ya kupanga kukutana
2. Namna ya kujiandaa kukutana
3. Namna ya kuvaa siku hiyo( hakuna haja ya gharama za nguo)
4. Jinsi ya kutembea
5. Tabia na mienendo za kuwa nazo au ,a kuepuka unapokuwa n mwanamke kwa mara ya kwanza.

Ktk uzi wa Mwanadada huyu ametaja mambo mazito ambayo braza kakosea sana na imepelekea Mwanadada kumuona ni mtu wa hovyo na hafai kuwa Mwanaume wake.

Stay tuned.

Kwakweli coz wanaume nao wanahitaji kitchen party
 
Wewe ndo wale wale hamna cha kuchangia zaidi ya kutoa pussy na mwanaume akiomba mtoko huwa mnafanya kama kukomoa ivi kwann usinge chagua sehem nzuri ya bei rahisi? Kwanza jamaa angekuona una akili sana hata mshikaj huko alipo na yeye atakuwa amefuta na namba yako kabisa!


Nilimuombaga dem mmoja mtoko akakubali nikampa location tutakapo kwenda akasema mbona mbali sana gari yake haina mafuta nikamwambia usijali nitakutumia hela ya wese akasema poa nilichokifanya nikasema ngoja nione huyu ni mwanamke wa aina gani nilimtumia 30k nikamwambia weka mafuta hiyo akajibu sasa 30k itatosha mafuta gani na gari yake ina engine kubwa asee hapo hapo nikasema basi baki huko ulipo mimi nitakufata nilivyokata simu tu nikafuta na namba stupid kabisa! Yani 30k ya mafuta yeye anaona ni ndogo mbona hakuwa nayo sasa
She was a Gold Digger
 
Ila wewe pia jinga sana. Ulivyoambiwa chagua ungechagua sehemu ya bei rahisi... angalia sasa malengo yako hayajatimia... jamaa kafakamia MSOSI WA NDOTO ZAKO. Halafu wanawake mnaopenda kiswanglish huwa mnakera balaa. Mimi ningekupeleka Holiday Inn lakini ungekunywa maji tu.

Ata ww ungeambiwa chagua any place I bet ungechagua hata Hyatt
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom