DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Akiwakilisha kundi la Wabunge walio wachache bungeni katika msiba wa Hayati Edwin Mtei, Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHAUMMA, Sigrada Mligo, amesema busara na hekima za Mzee Mtei ni nguzo muhimu ambazo wanasiasa wanapaswa kujifunza.
“Mimi binafsi huwa natamani nipate hata robo tu ya busara za huyu mzee, nikiziangalia hata theluthi za busara za mheshimiwa Mbowe niwe nazo, lakini nimeshindwa.
Sisi kama wabunge tulio wachache bungeni, tunamuahidi kwenda kupigania demokrasia ya kweli katika nchi hii, kwenda kuhakikisha nchi hii inarudi kwenye kuheshimiana, tunajadili jambo la kitaifa kwa pamoja.
Ameendelea kusema, "Wanyonge wanatakiwa kuungana kupambana na wenye nguvu, nashangaa sana pale tunapoona wanyonge wanafinyana wenyewe.”
“Mimi binafsi huwa natamani nipate hata robo tu ya busara za huyu mzee, nikiziangalia hata theluthi za busara za mheshimiwa Mbowe niwe nazo, lakini nimeshindwa.
Sisi kama wabunge tulio wachache bungeni, tunamuahidi kwenda kupigania demokrasia ya kweli katika nchi hii, kwenda kuhakikisha nchi hii inarudi kwenye kuheshimiana, tunajadili jambo la kitaifa kwa pamoja.
Ameendelea kusema, "Wanyonge wanatakiwa kuungana kupambana na wenye nguvu, nashangaa sana pale tunapoona wanyonge wanafinyana wenyewe.”