Sifikirii kama kuna ulazima wa kuendesha zoezi la sensa ya watu na makazi katika kipindi hiki cha mdororo wa uchumi

Katika mambo ambayo mataifa mengi yanapigana nayo kwa sasa ni kunusuru uchumi wao na kuachana na matumizi yasiyo ya lazima. Uchumi wa mataifa mengi umeathiriwa na mlipuko wa COVID 19 hali iliyopelekea hatua kadhaa za kubana matumizi kufaatwa.

Mwakani taifa letu litafanya zoezi la sensa kwa maana kwamba mabilini ya fedha yatatumika. Miongoni mwa mambo na maswali ya kujiuliza JE NI KWELI KUNA ULAZIMA WA KUENDESHA SENSA KWA DUNIA NA HALI YA SASA?

Nchi hii haijui kama kina mama wajawazito wanapoteza maisha kwa ukosefu wa huduma za afya karibu? PELEKA PESA UKAJENGE MIUNDOMBINU YA AFYA, nchi hii haijui watoto wanakaa chini? Wanasomea chini ya miti? PELEKA PESA HIZO UKAWEKE MIUNDOMBINU YA ELIMU.
Naunga mkono hoja, kwa hali ilivyo hatuhitaji Sensa kwa sasa, labda hadi 2030, serikali ingeshughulikia uchumi wa watu wake na maendeleo mbali mbali, idadi ya watu haina maana kwa sasa. Tuna mambo makubwa ya kitaifa kushughulikia haraka, idadi ya watu haina umuhimu hivyo kwa sasa.
 
Mleta mada huelewi Nini kuhusu sensa,huwezi kuendesha nchi bila ya kuwa na takwimu,labda tutumi njia mbadara ya kuendesha sensa,tunawezi kutumia watendeji wa kata wakatupa takwimu za mahitaji ya msingi.ila sensa lazima ifanyike.
Kujenga barabara kunahitaji kujua idadi ya watu?
Kuajiri waalimu na madaktari inahitaji kujua idadi ya watu?
Kusambaza maji vijijini kunahitaji kujua idadi ya watu?
Miaka yote wanajua idadi ya watu mbona huduma za afya ni mbovu?
Mzungu ndio anajua kutumia sensa kuandaa mipango ya maendeleo ya baadae,
Tanzania hatuna plani zozote za baadae,
 
Back
Top Bottom