Sifa za blacksheep na namna ya kuishi nao

Sifa za blacksheep na namna ya kuishi nao

Think2

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2025
Posts
2,193
Reaction score
3,957
Sifa za "Black Sheep" (mwana kondoo mweusi) katika familia/kundi:

1. Hutofautiana na wengine – Ana mtazamo, tabia, au maisha yasiyoendana na ya familia/kundi.
2. Mwenye maamuzi huru – Hufuata njia yake bila kujali matarajio ya wengine.
3. Huonekana kama muasi – Anaweza kukaidi mila, dini, au mfumo wa familia.
4. Hutengwa au kubezwa – Mara nyingi huonekana kama “msumbufu” au chanzo cha aibu.
5. Anaweza kuwa mbunifu au mkomavu kuliko wengine – Ingawa hukosolewa, mara nyingine yeye ndiye mwenye fikra pana au uelewa wa mapema.

Namna ya kuishi na "Black Sheep":

1. Kuwa na uvumilivu – Tambua kuwa tofauti si kosa.
2. Mpe nafasi ya kujieleza – Msikilize bila kumhukumu.
3. Usimlazimishe kuwa kama wengine – Heshimu uchaguzi wake.
4. Muonyeshe upendo wa kweli – Hata kama hampendani kimtazamo, upendo hujenga daraja.
5. Jifunze kutoka kwake – Tofauti zake zinaweza kuwa na faida au funzo kwa familia.
6. Epuka kumsema vibaya – Badala yake, msaidie au muelewe kwa undani.
 
Vile vijamaa ambavyo unakuta familia nzima mmesoma vizuri na mkapata hela ila vyenyewe shule vimekimbia na bado havina ajira wala hela ila full ujuaji na kufuatana majumbani kuombana hela kwa jina la sister na brother wangu au shemeji
Akifeli kimaisha anakuwa "black sheep", akifaulu anakuwa "golden goose" wa kupigwa mizinga na kila mtu
 
Vile vijamaa ambavyo unakuta familia nzima mmesoma vizuri na mkapata hela ila vyenyewe shule vimekimbia na bado havina ajira wala hela ila full ujuaji na kufuatana majumbani kuombana hela kwa jina la sister na brother wangu au shemeji
Hapana. Umekosea. Muda mwingine blacksheep hua anatengwa tu, kwa kosa ambalo halina maana, sifa uza blacksheep umezitoa vizuri sana. Lakini haya maelezo umejamba kwenye maji mkuu. Sio blacksheep wote omba omba, na sio kila omba omba ni bkacksheep.
 
Hapana. Umekosea. Muda mwingine blacksheep hua anatengwa tu, kwa kosa ambalo halina maana, sifa uza blacksheep umezitoa vizuri sana. Lakini haya maelezo umejamba kwenye maji mkuu. Sio blacksheep wote omba omba, na sio kila omba omba ni bkacksheep.
Tafadhali nakuheshimu sana jamaa yangu na nitapenda tuendelee kuwa marafiki ila mpaka pale utakapokubali kuedit neno kujamba katika maelezo yako ili unikosoe kwa staha mimi kama mtu mzima ,mwenye elimu kubwa na kazi nzuri ila blacksheep wa familia yetu .
Natamani tuendelee kuwa marafiki hivyo sitegemei kama utakataaa kuedit hilo neno "KUJAMBA " katika maelezo yako mazuri .
Ahsante
 
Vile vijamaa ambavyo unakuta familia nzima mmesoma vizuri na mkapata hela ila vyenyewe shule vimekimbia na bado havina ajira wala hela ila full ujuaji na kufuatana majumbani kuombana hela kwa jina la sister na brother wangu au shemeji
Black sheep sio lazima awe ba sifa hizo.

Black sheep ni mtu aliyechagua njia zake tofauti na kile kilichowekwa kama “ukawaida “
 
Tafadhali nakuheshimu sana jamaa yangu na nitapenda tuendelee kuwa marafiki ila mpaka pale utakapokubali kuedit neno kujamba katika maelezo yako ili unikosoe kwa staha mimi kama mtu mzima ,mwenye elimu kubwa na kazi nzuri ila blacksheep wa familia yetu .
Natamani tuendelee kuwa marafiki hivyo sitegemei kama utakataaa kuedit hilo neno "KUJAMBA " katika maelezo yako mazuri .
Ahsante
Dahhh!!!! Nimecheka sana. sasa mtu mzima, mwenye elimu kubwa na kazi nzuri. Mbona hilo neno umelirudia mara mbili mkuu?? Hiyo ni ishara kwamba halina tatizo lolote, its a figure of speech.

Kama imekukera ndo basi tena. Sibadili chochote. Tumie hiyo elimu kubwa kuelewa that figure of speech.
 
Akifeli kimaisha anakuwa "black sheep", akifaulu anakuwa "golden goose" wa kupigwa mizinga na kila mtu
Sijamaanisha hivyo
Hapana. Umekosea. Muda mwingine blacksheep hua anatengwa tu, kwa kosa ambalo halina maana, sifa uza blacksheep umezitoa vizuri sana. Lakini haya maelezo umejamba kwenye maji mkuu. Sio blacksheep wote omba omba, na sio kila omba omba ni bkacksheep.
Kujamba kwenye maji tena 😂
 
Uzi mzuri sana huu endeleenj kutirilika ma-black sheep
 
Back
Top Bottom