Sifa kumi za mpenzi wa kweli

Sifa kumi za mpenzi wa kweli

Herbalist Dr MziziMkavu

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,073
Reaction score
34,844
Mpenzi msomaji wangu, ni wakati mwingine ambao tunakutana katika uwanja huu wa maisha na mapenzi, kwa lengo la kujifunza namna ya kuwa wapenzi bora na kuepukana na tatizo la kuachana ambako kumekuwa fasheni siku hizi.

Vijana wengi ambao wanapendana leo mapenzi yao hayadumu kiasi cha kubatishwa jina la utamu wa bazoka. Lakini yote hii inatokana na ukweli kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.

Ipo zana potofu kwamba kumfundisha motto mapenzi ni kumharibu, jambo ambalo si kweli bali inategemea mtoto huyo anafundishwa nini na kwa wakati gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa mapenzi hawayajui, matokeo yake wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa bumbumbu na hivyo kuteshwa na changamoto za mepenzi.

Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu. Sifa hizo hizi zifuatazo.

1. Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.


2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri .
4. Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuacha mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa nyuma na kukuacha bila msaada .

6.Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7.Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine

8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.

9. Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe.

 
wengine hawavulii kwa lolote lile, hujamfikiria kesha toa hitaji lake. anajua uwezo anataka juu uwezo huo. mapenzi jama?
 
Kwa hizo sifa ulizozitaja, napata picha mapenzi ya kweli sasa yamekuwa adimu sana..!!
 
tatizo kubwa ni kwamba moyo wa m2 ni kichaka, waweza kumpenda m2 yeye akawa anafanya usanii, ukishagundua hilo ina maana nafasi ya kuwaamini wapenzi inakuwa tayari ina doa kubwa sana, akitokea m2 mwingine wa kukupenda itakubidi nawe umfanyie usanii kwa kuwa yalishakukuta ya kuigiza.
 
Hapa penye ukweli uongo lazima ujitenge, MziziMkavu mpenzi wako wa kweli ana sifa ngapi hapa?
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom