Siasa za CHADEMA kama za CCM

Siasa za CHADEMA kama za CCM

NATAKA nionyeshwe tofauti ya CCM na CHADEMA kwenye mambo makubwa wanayoshutumiana. Kama chadema wanasema CCM ni chama cha watoto wa wakubwa kubebwa basi na CHADEMA wasiwepo!

Nisichotaka ni kuaminishwa kwamba kuna chama cha watakatifu kinaongozwa na watu wasio kosea wala wasio na rekodi mbaya za maisha yao ya nyuma wakati tunajua kwamba siyo kweli. Nyerere alishawahi kusema "Hatuhitaji malaika kuja kutuongoza" na hili ndilo ninalolipigania kwamba CHADEMA kisifanywe ni chama cha malaika chama ambacho watu wake wakikosea basi nchi nzima isujudu kutubu makosa yao.

njaa yako sasa inakuondolea utu wako.
 
njaa yako sasa inakuondolea utu wako.
Njaa yangu kubwa ni kuona mabadilko ya kweli. kama CCM wakizomewa kwa kufanya madudu tunashangilia, nataka na CHADEMA wakifanya madudu nao pia wazomewe! Kama ni njaa ya tumbo tu mzee nakula na kusaza, kwa hilo mungu wangu wa mbinguni ahimidiwe!
 
Njaa yangu kubwa ni kuona mabadilko ya kweli. kama CCM wakizomewa kwa kufanya madudu tunashangilia, nataka na CHADEMA wakifanya madudu nao pia wazomewe! Kama ni njaa ya tumbo tu mzee nakula na kusaza, kwa hilo mungu wangu wa mbinguni ahimidiwe!

chadema haihitaji ushauri wa kipuuzi kama huu.Wewe ni Magamba na ndio maana unajaribu kupima upepo hapa jamvini.Hakuna mpigania haki mwenye mawazo mfu kama haya.Mbona huwashauri washirika wenu Cuf ambao viongozi wake robo tatu ni wapemba?
 
cdm magwanda,ccm magamba.hivyo vua gamba vaa gwanda!kuna tofauti kubwa sana kati siasa za kukumbatia mafisadi,makundi na proopaganda zinafanywa na ccm,dm harakati zidi kupinga unyonge,umaskini,ufisadfi,ukkiukwakaji wa hakiza binadamu na upuuzi mwingine unaoufahamu.ccm akili zenu na upeo wenun sawa cuf,afp,chausta,updp,na ncccr.hamna mabacho mn chokifanya ambacho kinaweza kuwafananisha na chadema na serikali yenu inao wabagua watoto wa maskini ktk elimu kama mikopo,
 
cdm magwanda,ccm magamba.hivyo vua gamba vaa gwanda!kuna tofauti kubwa sana kati siasa za kukumbatia mafisadi,makundi na proopaganda zinafanywa na ccm,dm harakati zidi kupinga unyonge,umaskini,ufisadfi,ukkiukwakaji wa hakiza binadamu na upuuzi mwingine unaoufahamu.ccm akili zenu na upeo wenun sawa cuf,afp,chausta,updp,na ncccr.hamna mabacho mn chokifanya ambacho kinaweza kuwafananisha na chadema na serikali yenu inao wabagua watoto wa maskini ktk elimu kama mikopo,

Ninachokataa ni ile falsafa ya kiyahudi kwamba "neno jema haliwezi kutoka Samaria". Kupagawa kwenu na imani ya kile mnachokiamini kwamba ndiyo sheria na Kanuni (world order) ya kimaumbile ya ulimwengu ndiko ninakokupinga. Nakumbuka zogo lililotokea wakati Zitto alipotaka kugombea uenyekiti wa taifa.

Kila mtu aliaminishwa kwamba Zitto katumwa na Rostam Aziz kugombea ili aisambaratishe CHADEMA. Hivi kila mtu mwenye mawazo tofauti na nyie ni lazima awe ni mwanachama wa CCM au katumwa na mafisadi? Ina maana demokrasia ya CDM ni kukubali kila kitu bila ya kutafakari au kuwa na mawazo mbadala?
 
chadema haihitaji ushauri wa kipuuzi kama huu.Wewe ni Magamba na ndio maana unajaribu kupima upepo hapa jamvini.Hakuna mpigania haki mwenye mawazo mfu kama haya.Mbona huwashauri washirika wenu Cuf ambao viongozi wake robo tatu ni wapemba?
Kwa hiyo "Upemba' wa CUF ni hatari bali 'undugu' wa CHADEMA ni ukamanda!!
 
Kwa hiyo "Upemba' wa CUF ni hatari bali 'undugu' wa CHADEMA ni ukamanda!!

wewe umesema upemba wa Cuf ni hatari.Mimi sijasema.Ninachoweza kukushauri mind your Magamba party business.Thats it!
 
wewe umesema upemba wa Cuf ni hatari.Mimi sijasema.Ninachoweza kukushauri mind your Magamba party business.Thats it!
Tafsiri ya maneno yako ndivyo yanavyoonyesha kwamba upemba wa CUF ni hatari. Kwa taarifa yako chama cha siasa ni Public Property hakina mwenyewe ndiyo maana hakuna kufunga milango ya kujiunga wala masharti ya kibaguzi. CHADEMA ni Public property wanachama na wasio wanachama wana haki ya kukikosoa.

Mimi si mwana CCM lakini naongozwa na CCM. Kwa hiyo CCM wakikataa kukosolewa na mimi utakuwa ni ujinga wao na CDM kwa sababu wanataka kuniongoza ni lazima niwakosoe kwa aina nipendayo. Vyama vya siasa ni watumishi wa Umma na ni umma ndiyo wenye haki ya kivikosoa vyama vya siasa na vyama vya siasa havina haki ya kuukosoa Umma.
 
Bado hujuaeleweka mkuu, katika dunia wote tuna mahusiano,kwanza wote ni BINADAMU,pili tumezaliwa na binadamu so labda utupe ushahidi wa wazi kuwa kuna upendeleo katika kupata nafasi fulani, ikiwa mtu katimiza vigezo na masharti kuna kosa gani?ieleweke kwamba kumpendelea mtu kutokana na unasaba ni jambo lisilofaa na huenda na ndivyo ilivyo huzorotesha maendeleo ya sehem husika hebu tupe ushahidi kuwa kuna upendeleo halaf HATUA ZICHUKULIWE

Huelewi nini? Anasikitishwa na dynasty iliyoko huko CDM ambayo haina tofauti na ile ya CCM tunayoitolea mimacho na kutoka mapovu tunapoijadili. Sasa unaomba ushahidi gani zaidi wakati umeambiwa kila kitu:

1. Dr. Slaa /Rose Kamili
2. Ndesamburo/Lucy Owenya/Grace Kiwelu
3. Tundu Lissu/Christina Lissu
4. Zito Kabwe/Muhonga Ruhwanya
5. Anna Komu/Anthony Komu (siyo mke na mume)
6. Edwin Mtei/Freeman Mbowe
 
Aliyekuwa diwani wa kata ya kaloleni kupitia CHADEMA inasemekana anatafutwa na Polisi kwa tuhumu za kumtapeli mwekezaji mwenza kwenye biashara yao ya utalii. Charles David Mpanda (Rasta) anadaiwa kumtapeli Margaret Lema kiasi cha Dola 16,400 kutoka kwenye akaunti yao ya pamoja.

Hili jambo limenifanya nifikirie upya siasa za bongo. Margaret ni Mdogo wake God bless Lema Mbunge wa Arusha Mjini kwa maana nyingine yale yanayotokea CCM kwa watu wa ukoo mmoja kumiliki chama yanatokea na CHADEMA pia. Mbowe kaoa mtoto wa Edwin Mtei Muasisi wa CHADEMA, Lucy Owenya mbunge wa viti maalum ni mtoto wa Philimon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini.

Ukikutana na Rose Kamili Mbunge wa viti maalum ujue ni mzazi mwenzie Dr. Wilbroad Slaa pia ujue kwamba ukikutana na Christina LIssu ni Mdogo wake na Tundu Lissu, na Moulida au Anna Komu Mbunge Viti maalum ni Mke wa mkuu wa Idara ya fedha Makao Makuu CHADEMA, Anthony Komu. Hawa ni wale wanaohusiana kimapenzi na kiukoo hatujui wale wanaohusiana kimaslahi kama vile kibiashara wako wangapi na kwenye ngazi zipi. Lakini jambo hili kwa sababu limetokea CDM basi litatetewa weeee hadi mijasho itukauke.

Aliyekuwa mkuu wa upelelezi Kanda Maalum ya Dar es salaam Abdalah Zombe alidai kwamba Godbless Lema alikuwa ni mwizi wa magari. Sijaona mcharuko mkubwa angalau wa kumshinikiza Zombe aseme anavyojua wizi wa magari wa Lema wala wa kumshinikiza Lema kueleza historia yake ya nyuma kabla hajawa Mbunge inahusiana vipi na wizi wa magari. Wote tuko kimyaa kwa sababu ni mtoto wa nyumbani. Rage kuonyesha Bastola ilikuwa nongwa lakini la Lema ni "Uzushi' wa magamba.
kwenye red highlight nadhani panajieleza panyewe. Ila ninavyojua kwa chadema hamna tofauti na ccm. Na ndo maana hata juzi na wao walikuwa wakiiba kura kule igunga. kwani zilikutwa kura nyingi zimetikiwa kwa mgombea wa chadema.
chadema na ccm wote ni many'ang'au, ila kwa viwango tofauti. ila hiki kiny'ang'au kidogo kinakua kwa kasi ya ajabu, du! muda si mrefu kitakuwa linyany'ang'au likubwa kama hili la zamani. EWE MUNGU TUEPUSHIE MBALI NA MANY'ANG'AU HAYA. AMEEN!
 
Tafsiri ya maneno yako ndivyo yanavyoonyesha kwamba upemba wa CUF ni hatari. Kwa taarifa yako chama cha siasa ni Public Property hakina mwenyewe ndiyo maana hakuna kufunga milango ya kujiunga wala masharti ya kibaguzi. CHADEMA ni Public property wanachama na wasio wanachama wana haki ya kukikosoa.

Mimi si mwana CCM lakini naongozwa na CCM. Kwa hiyo CCM wakikataa kukosolewa na mimi utakuwa ni ujinga wao na CDM kwa sababu wanataka kuniongoza ni lazima niwakosoe kwa aina nipendayo. Vyama vya siasa ni watumishi wa Umma na ni umma ndiyo wenye haki ya kivikosoa vyama vya siasa na vyama vya siasa havina haki ya kuukosoa Umma.

ni kweli ukosoaji unaruhusiwa lakini si kwa unafiki kama ufanyavyo.Wewe unaleta ubaguzi wa kikabila kwa maslahi ya chama chako Magamba.Unataka kusema ndugu yako akiwa mwanachama na kiongozi basi huruhusiwi kushiriki harakati eti itaonekana undugu? Mnafiki ni aheri ya mchawi.Mlitumia uongo huu mwaka jana Watanzania wakawajibu kwa kuiongezea chadema wabunge kutoka 5 hadi 48.Igunga mkatumia propaganda hizohizo wanaIgunga wakawajibu kwa kuwapa kura chadema kutoka kura sifuri hadi elf 23.Hamchoki tu? Tafuteni propaganda nyingine hii imeshindwa.
 
chadema haihitaji ushauri wa kipuuzi kama huu.Wewe ni Magamba na ndio maana unajaribu kupima upepo hapa jamvini.Hakuna mpigania haki mwenye mawazo mfu kama haya.Mbona huwashauri washirika wenu ("Cuf ambao viongozi wake robo tatu ni wapemba")?
kama CDM tu viongozi wake robo tatu ni Wachagga
 
Mtoto wa kiume sio vizuri kumsifia mwanaume mwezengu! Unatupa wasiwasi kama uwa anakupa pesa sisi hatufahamu

mwambie kazi unayofanya hapa ni kubwa akupe walau buku 3 kwa siku
 
ni kweli ukosoaji unaruhusiwa lakini si kwa unafiki kama ufanyavyo.

Sielewi ni kwa nini unafikiri ukosoaji wangu ni wa kinafiki wakati kila kitu nimeweka adharani.

Wewe unaleta ubaguzi wa kikabila kwa maslahi ya chama chako Magamba.

Kama utaonyesha kwenye post yoyote nimetaja kabila lolote basi nihukumu,lakini kama utashindwa kuonyesha basi wewe ni MZUSHI

Unataka kusema ndugu yako akiwa mwanachama na kiongozi basi huruhusiwi kushiriki harakati eti itaonekana undugu?
Sijakataa kuwa ndugu yako akiwa mwanasiasa na wewe usiwe mwanasiasa. Julius alikuwa mwanasiasa na Joseph Nyerere naye alikuwa ni mwanasiasa. sioni tatizo katika hilo. Hoja yangu ni kwani nini hayo yakitokea CCM inakuwa ni nongwa kwa CDM ni baraka?

Mnafiki ni aheri ya mchawi.
Hata mimi nakusihi wewe usiwe mnafiki kwani hata dini zinakataa wanafiki.

Mlitumia uongo huu mwaka jana Watanzania wakawajibu kwa kuiongezea chadema wabunge kutoka 5 hadi 48.
idadi siyo ubora na sababu za kupatikana kwa wabunge hutofautiana kati ya Jimbo na Jimbo na na sehemu na sehemu.

Igunga mkatumia propaganda hizohizo wanaIgunga wakawajibu kwa kuwapa kura chadema kutoka kura sifuri hadi elf 23.Hamchoki tu? Tafuteni propaganda nyingine hii imeshindwa.
Wanaigunga tangu mwaka jana walishaikataa CCM na ndiyo maana walimpa Mgombea wa CUF Mahona Kura 11,000 bila ya nguvu kubwa kutumika. Kwa hiyo mwaka huu watu wengi zaidi wamefikiwa na nguvu kubwa zaidi ikatumika kwa pamoja CDM na CUF wameongeza kura 15,000 kutoka zile 11.000 za awali. Wana Igunga walishaikataa CCM hata kama CDM wasingeenda wangewachagua vyama vingine na si CCM.
 
Sielewi ni kwa nini unafikiri ukosoaji wangu ni wa kinafiki wakati kila kitu nimeweka adharani.



Kama utaonyesha kwenye post yoyote nimetaja kabila lolote basi nihukumu,lakini kama utashindwa kuonyesha basi wewe ni MZUSHI


Sijakataa kuwa ndugu yako akiwa mwanasiasa na wewe usiwe mwanasiasa. Julius alikuwa mwanasiasa na Joseph Nyerere naye alikuwa ni mwanasiasa. sioni tatizo katika hilo. Hoja yangu ni kwani nini hayo yakitokea CCM inakuwa ni nongwa kwa CDM ni baraka?


Hata mimi nakusihi wewe usiwe mnafiki kwani hata dini zinakataa wanafiki.


idadi siyo ubora na sababu za kupatikana kwa wabunge hutofautiana kati ya Jimbo na Jimbo na na sehemu na sehemu.


Wanaigunga tangu mwaka jana walishaikataa CCM na ndiyo maana walimpa Mgombea wa CUF Mahona Kura 11,000 bila ya nguvu kubwa kutumika. Kwa hiyo mwaka huu watu wengi zaidi wamefikiwa na nguvu kubwa zaidi ikatumika kwa pamoja CDM na CUF wameongeza kura 15,000 kutoka zile 11.000 za awali. Wana Igunga walishaikataa CCM hata kama CDM wasingeenda wangewachagua vyama vingine na si CCM.

nina swali moja kwako kwanini wanaIgunga hawakuwapa kura hao wasio na undugu katika uongozi kama chadema kwa madai yako? Kwanini kura za cuf ziporomoke ziende chadema? Kwanini wasichague vyama vingine vya upinzani kama SAU,DP,UPDP au Chausta? Kwa nini wakipe kura chadema ilihali wewe unakituhumu ni chama cha kibaguzi? Kama wewe si mnafiki nipe majibu.
 
Kwanza nashukuru ndugu yangu kwamba tumetoka kubishana hadi sasa kujadiliana, hayo ndiyo mabadiliko ya kweli na Uhuru wa Kweli ambao CHADEMA inaupigania.
nina swali moja kwako kwanini wanaIgunga hawakuwapa kura hao wasio na undugu katika uongozi kama chadema kwa madai yako?
Igunga hoja kubwa ilikuwa kama Igunga ni maskini au si maskini na kama ni maskini ni nani kausababisha huo umaskini. Kwa hoja hii CDM walishinda kwani wananchi wenyewe wa Igunga wanajua umaskini wao. Pia Igunga walikuwa hawawachagui hao niliowaorodhesha bali walikuwa wanataka kuchagua Kashindye mwana Igunga mwenzao na mwalimu maarufu anayefahamika na wengi.

CUF hawakuchaguliwa kwa sababu wenyewe waliwekeza kidogo kwenye upelekaji wa ujumbe wao kwa wananchi hadi wakashindwa kujitofautisha wao na CCM ambao wananchi wa Igunga walishaamini ndiyo wezi wa rasirimali zao na ndiyo waliosababisha wao wawe maskini.

Kwanini kura za cuf ziporomoke ziende chadema?
Hakuna anayejua kwenye suala la kura ni za nani zilikwenda CDM. Kwa nini usifikiri kwamba za CUF zilikwenda CCM na CDM wao walichota za CCM?
Kura za CUF zilipungua kwa sababu walikuwa hawana hoja mahsusis inayokubalika kwa wananchi. Halafu kumbuka ndoa ya CCM na CUF ni mzigo unaowatesa CUF huku Tanzania Bara.

Kwanini wasichague vyama vingine vya upinzani kama SAU,DP,UPDP au Chausta? Kwa nini wakipe kura chadema ilihali wewe unakituhumu ni chama cha kibaguzi? Kama wewe si mnafiki nipe majibu.

Hivi vyama vyote ulivyovitaja uwekezaje wake wa kifedha na rasirimali watu huwezi kuufananisha na CCM na CDM. CDM walikuwa na Helkopta moja wenzao wa CCM walikuwa nazo mbili. Igunga kuna kata 26 hivi vyama vingine hata magari walifanya kukodisha au walikuw nayo chakavu. kwa mantiki hiyo utaona ni kwa nini mvutano ulikuwa ni kwa CCM na CDM na CUF kwa Mbaaali.

Wabunge wa CCM na CDM walikuwa wanapishana mbugani na magari yao huku wengine wa vyama hivi hata kuzindua kampeni zao walikuwa na Horn speakers tu. heri yule wa UPDP alituburudisha kwa Mayenu.
 
Back
Top Bottom