Mongoiwe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 524
- 263
Kada maarufu wa CCM na aliyewahi kuwa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki(EALA), ShyRose Bhanji kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram ameandika kuwa Hakubaliani na Utawala wa Rais JPM, na yuko tayari kwenda jela
Ikumbukwe kuwa Mwanasiasa huyo siku kadhaa zilizopia aliandika kupitia ukurasa wake huo kuwa ''Serikali ya chama changu CCM haiwezi kukwepa lawama kwa namna yoyote ile kufuatia kupigwa risasi kwa binti ambaye hakuwa na hatia hata kidogo.
Imekuwa ni siku mbaya sana kwangu; nimeshindwa kula na nashindwa kupata usingizi kutokana na kifo cha huyu binti. Nafsi yangu inanisuta. Mungu wangu naomba unisaidie ''
=====
UPDATES
ShyRose Bhanji ajitokeza na kukanusha taarifa zilizosambaa kuwa hakubaliani na utawala wa Rais Magufuli
Kupitia akaunti yake hiyo ya Instagrama, Shyrose amemuomba radhi Rais Magufuli na watanzania wote kwa ujumbe huo kwani akaunti yake ilidukuliwa
Ikumbukwe kuwa Mwanasiasa huyo siku kadhaa zilizopia aliandika kupitia ukurasa wake huo kuwa ''Serikali ya chama changu CCM haiwezi kukwepa lawama kwa namna yoyote ile kufuatia kupigwa risasi kwa binti ambaye hakuwa na hatia hata kidogo.
Imekuwa ni siku mbaya sana kwangu; nimeshindwa kula na nashindwa kupata usingizi kutokana na kifo cha huyu binti. Nafsi yangu inanisuta. Mungu wangu naomba unisaidie ''
UPDATES
ShyRose Bhanji ajitokeza na kukanusha taarifa zilizosambaa kuwa hakubaliani na utawala wa Rais Magufuli
Kupitia akaunti yake hiyo ya Instagrama, Shyrose amemuomba radhi Rais Magufuli na watanzania wote kwa ujumbe huo kwani akaunti yake ilidukuliwa