NICK2275
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 3,931
- 918
Mwanaharakati wa masuala ya kijamii, Shyrose Bhanji (pichani), ametoa kilio chake kutoka moyoni akilalamika kuchezewa rafu na wabaya wake, Amani Jipya linashuka nayo.
HABARI KAMILI
Shyrose alianza kuandika kwenye ukurasa wake katika ‘netiweki' ya kijamii ya Facebook mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba, kuna kundi limeibuka ambalo kazi yake ni kumsema vibaya hivyo kutaka kujua amewakosea nini.
Katika maelezo yake, mwanaharakati huyo alilitaja kundi hilo kwa jina la Jamiiforum kuwa ndilo lililo mstari wa mbele katika kumharibia sifa yake kila kukicha.
Aliandika: "Naomba kuuliza, nimewakosea nini mpaka mnanisema vibaya sana?
"Jamiiforum ndiyo mko mstari wa mbele kuniharibia kila siku! Nimewakosea nini? Wote mnaoniharibia sifa yangu mnaniumiza moyo wangu sana na hamnitendei haki."
Alimalizia: "Kila mnaponiharibia, Mungu ananisaidia. Watch me (Niangalieni)."
Source-globalpublishertz