Shule ya sifa: Shule ya Sekondari Milambo, Tabora

Shule ya sifa: Shule ya Sekondari Milambo, Tabora

Alajesembamba.....
Nilikuwa hapo 93/95, KLF mimi ndio nilikuwa golikipa wenu, tukiwafunga Wavulana wa Tabora akina Njohole na Kidau goli 3. Nakimbuka mechi na Uyui iliyoahirishwa na Bro wa Students Center ndani ya uwanja wa vita. Halfu siku iliyofuata tulawapiga goli 3 tukivaa sketi ya rangi ya ugolo ya Uyui.
 
Nipo hapa nyumbani naendelea kuisogeza siku hii ya tarehe 01.01.2017.

Ghafla nikaikumbuka shule hii ya sekondari Milambo iliyopo mjini Tabora,takribani kilomita 2 tu toka kituo kikuu cha mabasi Tabora,na ipo njiani kama unaelekea Urambo,nyumbani kwa marehemu Mh. Samweli Sitta (Mungu amrehemu). Shule hii pia alisoma Mh Edward Ngoyai Lowasa, Waziri Mkuu Mstaafu wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Shule hii haina uzio (kwa sababu ni ya wanaume),na ipo karibu kabisa na mtaa maarufu Tabora uitwao Chemchemu.

Kando ya hiyo shule kuna canteen maarufu sana kwa ajili ya kununulia appetizer au chachandu unapotaka kulia NYALI au POLA.

Ni shule yenye mabweni matatu,mm nilikaa bweni la SOKOINE,floor ya kwanza.

Maji ya ile shule ni ya chumvi sana kiasi cha kuwafanya wanafunzi waende kuchota maji ya kunywa parokiani.

Nyuma ya shule upo uwanja mzuri sana wa mpira.

Waalimu ninaoweza kuwakumbuka n:-

1. Mwl Katondolaa (Marehemu)

2. Mwl Jubwa (Headmaster)

3. Mwl Zoma ( kwa fito balaa)

Nakimbuka pia kuna "Conco room",vyumba ambavyo wanafunzi hupenda kujifungia kama gheto kwa ajili ya kujisomea (hasa viongozi).

Ambavyo sitavisahau:

1. Sikuwahi kuitwa jina kwa miaka miwili

2. T-shirt zake zilikuwa kama blauzi. (ukivaa inasogea kifuani)

3. Foleni siku za nyali au ngema kwa nyama

4. Utamu wa pola (uji).

Milambo acha tu iitwe Milambo
cc kizaz kipya cha milambo tupoo tuko form five mwaka huu mwalimu Zoma yupo Babu wa chakula yupo pia mkuu ni mwl Benny Walter sitaisahau zaina zaina form 6 walivyotutesa ucku kucha na kuambulia kufukuzwa shule baadhi yao ni hayovtu mkuu kuhusu milambo ya sasa WALAMBOOO
 
Aisee mimi sitoisahau hii shule. Kwani maisha yangu yote ya Advance hapo milambo hatukuwahi kufanya annual, terminal wala midterm test.

Mtihani wa kwanza kuufanya ulikuwa ni Mock, wa pili NECTA herself.

Hahahaa.
Be honest ulifaulu?
 
Katika maisha yangu yote niliopitia hakuna kama milambo,

milambo ni shule iliyonifunza jinsi gani kuishi maisha yoyote kwenye dunia hii,bila kuishi kwa umakini na akili ya hali ya juu milambo lazima ufeli

milambo kuna kila aina ya uhuru,unaweza usikaeshuleni hata miaka yote ya masomo

we uwe unafanya mitihani yao tu over,sitamsahau mwalimu wangu KABEJA,alikua anakuja yuko vyombo(kitwanga) asubui ya masterpaled halafu yeye ndo mtoa matangazo utamchek anavyolembua tu,watu wanacheeeeeka


milambo ni shule inayoongozwa na wanafunzi ,kuna SKAUT wanamafunzo ya hali ya juu ukileta ngembe utajuta kuijua milambo

KIMBEMBE ndo mahala pake

mwanafunzi wa milambo tabora anaogopwa kuliko ata police,mwanafunzi wa milambo ni wamoja,akiguswa mwanafunzi mmoja huo msala kuisha kwake lazima FFU wamwagwe ndo watatuliza fujo

wanafunzi wa milambo kusimamiwa chini ya SMG ni kawaida kwao

mtaa wa chemchem kunawatoto wa WALAMBO

Naiheshimu sana milambo,wanafunzi wa milambo nawaheshimu sana

MILAMBO NAIKUBALI SANA KWA KUMFUNZA MWANAFUNZI KUISHI MAISHA YOYOTE,lazima utumie akili ya hali juu kusurvive katika mazingira yoyote,

big up
 
Walambo wamoja mlambo moja sana na waboyzia kumi dah afu kaka maji ya kunywa umekosea yanapatikana kachelema huko uzunguni na mtalaam zoma
 
Tatzo la milambo lengo kuu la kilichowapeleka shule lilipotea... Wao ni wasela nondo hawajali elimu, baadhi waliokua wanajielewa walielekea tabora boys kujisomea.
Bifu la milambo na tabora boys ndio kitu kinachonogesha zaidi...
Milambo washafungwa sana na boys pale ally hasan mwinyi....
Milambo inaongoza kwa zero wakishindana na uyui, st mary na shule za kata nyingine....
 
Wewe kumbe class mate wangu hapo



Basi kama ni huo mwaka utakumbuka yafuatayo


1. Disco vumbi kwa wanyamwezi na akina Nkunu Elisha,
2. Samaki zilizosambazwa katika taasisi za serikali tulikula mpaka basi

3. Mbwa mkali, hapa tunajipatia kila vinavyotuhusu,

4. Safati za kwenda kachelema.

5. Siku ya miss KAMNA warambo walishiriki karibia nusu ya shule.




Wimbo wetu na hasa ukutwapo na magumu popote ukiuimba utapata mrambo tiii


""Warambo mko wapi, warambo mko wapiii.....
Kwa nguvu utasikia yeaaaaaa.....""

Tulifukuzwa siku ya mwenge baada ya kukosa mahali pa kukaaa


Aseeee nakumbuka mengi uramboni jamaniii


Zoma,
Katondolaa
Kabejaa.
Oyooooo unaikumbuka ile siku ngema ilikua mbichi tukaimwagaa na vuruguu hatariiii
 
Choo Yetu Ya Carifonia Bado Ipo Wakuu?
Nakumbuka Kila Siku Mida Ya Saa Mbili Usiku Lazma Ntimbe Pale Aise.
 
hata humu Jf ukiita tu walambo njooni huku njoon huku watamwagika kama maji.
 
Tatzo la milambo lengo kuu la kilichowapeleka shule lilipotea... Wao ni wasela nondo hawajali elimu, baadhi waliokua wanajielewa walielekea tabora boys kujisomea.
Bifu la milambo na tabora boys ndio kitu kinachonogesha zaidi...
Milambo washafungwa sana na boys pale ally hasan mwinyi....
Milambo inaongoza kwa zero wakishindana na uyui, st mary na shule za kata nyingine....

Walambo hawawapendi waboyzia kwa sababu wanazidiwa taaluma
 
boyz mda wote walikuwa wanawaza kusoma wanaingia disco na notes thats y girls walikuwa hawataki kuwaalika disco milambo ndo walikuwa fit angle zote eg kisoka,kutoa vibano kwa boyz nk i remember 2003,
 
Nipo hapa nyumbani naendelea kuisogeza siku hii ya tarehe 01.01.2017.

Ghafla nikaikumbuka shule hii ya sekondari Milambo iliyopo mjini Tabora,takribani kilomita 2 tu toka kituo kikuu cha mabasi Tabora,na ipo njiani kama unaelekea Urambo,nyumbani kwa marehemu Mh. Samweli Sitta (Mungu amrehemu). Shule hii pia alisoma Mh Edward Ngoyai Lowasa, Waziri Mkuu Mstaafu wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Shule hii haina uzio (kwa sababu ni ya wanaume),na ipo karibu kabisa na mtaa maarufu Tabora uitwao Chemchemu.

Kando ya hiyo shule kuna canteen maarufu sana kwa ajili ya kununulia appetizer au chachandu unapotaka kulia NYALI au POLA.

Ni shule yenye mabweni matatu,mm nilikaa bweni la SOKOINE,floor ya kwanza.

Maji ya ile shule ni ya chumvi sana kiasi cha kuwafanya wanafunzi waende kuchota maji ya kunywa parokiani.

Nyuma ya shule upo uwanja mzuri sana wa mpira.

Waalimu ninaoweza kuwakumbuka n:-

1. Mwl Katondolaa (Marehemu)

2. Mwl Jubwa (Headmaster)

3. Mwl Zoma ( kwa fito balaa)

Nakimbuka pia kuna "Conco room",vyumba ambavyo wanafunzi hupenda kujifungia kama gheto kwa ajili ya kujisomea (hasa viongozi).

Ambavyo sitavisahau:

1. Sikuwahi kuitwa jina kwa miaka miwili

2. T-shirt zake zilikuwa kama blauzi. (ukivaa inasogea kifuani)

3. Foleni siku za nyali au ngema kwa nyama

4. Utamu wa pola (uji).

Milambo acha tu iitwe Milambo
Rwabukoba(second master)
 
usinikumbushe enzi za fupa, dadadeki, tulimng'oa mwaka 1994 na mwalimu Mabuye akaja kuwa mwalimu mkuu akitokea kazima, RIP mwalimu Mabuye, mwanakondoo nadhani unamsema mwalimu Mwilu ndio alikuwa mwalimu wa kifaransa, mwalimu Njile yupo Kaliua shule 1 ya kata huko,
Kaliua boy hapa!Njile ndo yule mwalimu wa Kifaransa?Si jembe letu ni Ben Nyandigo(Big Ben)
 
Nafikiri hakuna headmaster mwenye beat kama majubwa katika nchi hii anakupiga beat yaani unajua tayari ushafukuzwa shule. Nakumbuka alimpiga beat headboy mpaka anazimia lakini pia hakujali akasema nisipomfukuza huyu ujue mama yangu amefufuka na kuniambia nimuache la sivyo lazima aondoke. Majubwa ni noma
 
boyz mda wote walikuwa wanawaza kusoma wanaingia disco na notes thats y girls walikuwa hawataki kuwaalika disco milambo ndo walikuwa fit angle zote eg kisoka,kutoa vibano kwa boyz nk i remember 2003,
Mkuu ilikuwa 2004 walipovamia tabora girls usiku mwingi na kutoa kichapo cha kutosha nakumbuka majubwa alimwaga matusi kama hana akili nzuri Assembly
 
Mtoa mada Mwl katondolaa ni marehemu! Duh! Alikuwa anakubalika sana katika kutatua migogoro inapotokea japo alikuwa Mwl wa kifaransa
 
Back
Top Bottom