Shule ya sifa: Shule ya Sekondari Milambo, Tabora

Shule ya sifa: Shule ya Sekondari Milambo, Tabora

Nipo hapa nyumbani naendelea kuisogeza siku hii ya tarehe 01.01.2017.

Ghafla nikaikumbuka shule hii ya sekondari Milambo iliyopo mjini Tabora,takribani kilomita 2 tu toka kituo kikuu cha mabasi Tabora,na ipo njiani kama unaelekea Urambo,nyumbani kwa marehemu Mh. Samweli Sitta (Mungu amrehemu). Shule hii pia alisoma Mh Edward Ngoyai Lowasa, Waziri Mkuu Mstaafu wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Shule hii haina uzio (kwa sababu ni ya wanaume),na ipo karibu kabisa na mtaa maarufu Tabora uitwao Chemchemu.

Kando ya hiyo shule kuna canteen maarufu sana kwa ajili ya kununulia appetizer au chachandu umapotaka kulia NYALI au POLA.

Ni shule yenye mabweni matatu,mm nilikaa bweni la SOKOINE,floor ya kwanza.

Maji ya ile shule ni ya chumvi sana kiasi cha kuwafanya wanafunzi waende kuchota maji ya kunywa parokiani.

Nyuma ya shule upo uwanja mzuri sana wa mpira.

Waalimu ninaoweza kuwakumbuka n:-

1. Mwl Katondolaa (Marehemu)

2. Mwl Jubwa (Headmaster)

3. Mwl Zoma ( kwa fito balaa)

Nakimbuka pia kuna "Conco room",vyumba ambavyo wanafunzi hupenda kujifungia kama gheto kwa ajili ya kujisomea (hasa viongozi).

Ambavyo sitavisahau:

1. Sikuwahi kuitwa jina kwa miaka miwili

2. T-shirt zake zilikuwa kama blauzi. (ukivaa inasogea kifuani)

3. Foleni siku za nyali au ngema kwa nyama

4. Utamu wa pola (uji).

Milambo acha tu iitwe Milambo
Walambo wamojaa hakunaga kujuanaa ubabee kwa sana kupata nyali ilikua vitaa kati ya hao walimu kabaki zomaa katondoraa na majubwa washa tanguliaa
 
Aisee mimi sitoisahau hii shule. Kwani maisha yangu yote ya Advance hapo milambo hatukuwahi kufanya annual, terminal wala midterm test.

Mtihani wa kwanza kuufanya ulikuwa ni Mock, wa pili NECTA herself.

Hahahaa.
Daah milambo shule yangu naipendaa
 
Nimesoma hapo Advance,nilikaa bweni la Nyerere.
Hadi sasa Milambo iko vizuri,zaidi inazidi kuboreshwa,nilipata fursa ya kupatembelea hapo mwaka 2015 mwishoni.
ulikutana na yule mpishi anaitwa msengi, manake ndio aliyebaki, na kumbukumbu hatari, alinifahamu kwa vile nilikuwa namuibukia mara kwa mara kwa kupata soft manake ngema wakati mwingine ilikuwa ni shida kutafunika
 
Daaah nilikuwepo hapo nikipiga PCB,yan uongoz wa shule hauna habar ni mwendo wa utawala binafsi tuu alaf watu wanapasua pepa kama kawaidaa!!!!!!.
Mkuu ulikimbiaa zaina zaina
 
Mie nilimaliza hapo 1983 combination ya French . Nilikuwa Kennedy no. 10. Nakumbukia Sana maembe ya kule mawiti. Maji tulikuwa tunachota Bwawa la igombe. Nakumbukia father kalumanzira wa parokia ya makokola. Classmates ninaowakumbuka ni kama Shewere, Ben Mwangonda, Felix Lubuva, Revocatus Msokane, Julius Mganga , Philip assey n.k. Mkuu alikuwa ni Mr. Msemakweli.
na kyala akiwa second master ulimumkuta
 
Aisee mimi sitoisahau hii shule. Kwani maisha yangu yote ya Advance hapo milambo hatukuwahi kufanya annual, terminal wala midterm test.

Mtihani wa kwanza kuufanya ulikuwa ni Mock, wa pili NECTA herself.

Hahahaa.
ila ni kweli aisee, mie nimesoma hapo form 1 mpaka 4 sijaona test, na form 5 karibia nusu darasa tukafaulu vizuri tu
 
MILAMBO SHULE YANGU NAIPENDAAAA, IPO TABORA MJINI, MKOANI TABORA KANDA YA MAGHARIBI, MOTTO WETU SIKU ZOTE!!

Nakumbuka huu wimbo kila jumatatu lazima uimbwe wakati wa parade
 
Boyz wakituona wanaume wanakula chochoo
kuna siku alfajiri tukawa tunakimbia mchakamchaka, sasa kufika pale 4 ways karibia na mihayo sekondari, tukakutana na tabora boys nao wanakimbia mchakamchaka, dadadeki, ulitembea mkono hapo, sie tusio na nguvu vinyoya tukalala mbele kurudi shule, wababe wakanyukana, na kuna siku tena tulikutana na tabora boys nadhani lilikuwa ni kombe la mgulunde pale kazima, mechi kwisha tu ngumi zikaanza mpunga wa kazima sec wote ulilazwa chini, na kuna siku wakakosea behewa la treni tukawekwa pa1 na tabora boys, kuingia tunakuta tabora boys wametuna wanapiga story, mkono ulitembea hapo mpaka tabora boys ikabidi warudi kwa station master wakapewa behewa lingine
 
Back
Top Bottom