Naomba ushauri toka kwenu wataalamu wa taaluma na ufundishaji kutokana na tabia niliyoisikia ktk shule hii. Nina mtoto ninayemsomesha ktk shule hii ya Bendel memorial iliyoko moshi eneo la soweto, ambayo inaendeshwa na shirika la kikatoliki. Kwa ujumla matokeo yao ya mitihani huwa ni mazuri.
Tatizo kubwa ni uhusiano kati ya waalimu na wanafunzi wa shule hii. Ni miaka miwili sasa, mtoto anaporudi hadithi anayoisimulia ni wingi wa viboko unaotokana na maamuzi ya mwalimu yeyote ktk maeneo ya shule. Mshauri wa wanafunzi, yaani Patron hana ushauri anaotoa zaidi ya viboko.
Nilidhani ni utundu wa kijana wangu lakini hata jirani kalazimika kumuhamisha kijana wake kwa sababu hiyo hiyo. Wanafunzi wanapokuwa ktk maandalizi ya usiku, hiyo inayoitwa prep, kila wakati wanakuwa na wasi wasi maana patron akiingia huamua kupiga wanafunzi eti tu wanasoma wameinua vichwa, sic! Hata mlinzi wa shule anapiga wanafunzi viboko, eti tu ni usiku na anawasikia wakiongea.
Imani yangu hawa ni waalimu waliosomea, pamoja na yeyote aliyeko hapa ukumbini, hebu nipeni ushauri juu ya haya machache maana yapo mengi ambayo nadhani yanaharibu maana ya shule na huenda yatawaathili wanafunzi. Je, mtindo huu ni wa kawaida ktk ufundishaji?
Maana labda mimi kama mlezi namkinga sana kijana huyu!