MAGAMBA MATATU
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 646
- 1,174
Wakuu mie ni mwajiliwa wa kampuni ya madini hapa bongo , na mshahara wangu kwa mwezi ni laki 7.3,nina miaka miwili nikiwa kazini, nini diploma ya Environmental Engineering nina first class ya GPA ya 4.8 kwa ufupi nina sifa zote za kujiunga na chuo, lakini napenda kujiendeleza zaidi kielimu na kuna wakati nawaza niache kazi ili niende chuo, lakini pia naona nikiacha kazi nikasome nikimaliza nitakuta wigo wa ajira umepungua halafu nikasota mtaani, ila imefikia hatua nikaona kuwa sisi tulio na diploma za vyuo serikali imetunyima mkopo tangia mwaka jana sasa kuacha kazi nikasome naona ada itakuwa mzigo.
sasa naomba ushauli wenu wakuu, niache kazi ili niende chuo au nisome online chuo kikuu huria nikiwa kazini?? na nisomee course gani???
Nawasilisha wakuu.
sasa naomba ushauli wenu wakuu, niache kazi ili niende chuo au nisome online chuo kikuu huria nikiwa kazini?? na nisomee course gani???
Nawasilisha wakuu.