Shukrani kwa wana JF

Shukrani kwa wana JF

Najua kudhiliwa tena najua kufanikiwa katika hali yoyote, na katika mambo yoyote,
Nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Wafilipi 4:12-13

Mungu yupo pamoja nawe katika mambo yote JS.
 
Pole sana mpendwa!!!
Mungu ampumzishe mzee salama!!!
 
Pole sana JS, Mungu ni mwema na anakupenda sana ww kuwa na baba yako hadi umri huu, wengine waliwaona wazazi wao kwenye pichaa tuu. Pole sana
 
pole sana JS.
kazi ya MUNGU haina makosa.
tu mavumbi sisi, na mavumbini tutarudi.

bwana awe kiongozi wenu na mfariji wakati huu wa kipindi cha majonzi.
 
Pole sana mpendwa tunaendelea kuwaombea wote katika familia yenu Mungu awape faraja. Wamtumainio Bwana ni kama mlima sayuni ambao hautatikisika kamwe. Endelea kumtumaini Bwana hata ukiwa katika kipindi kigumu.GOD WILL MAKE A WAY WHERE IT SEEMS TO BE NO WAY HE WORKS IN WAYS WE CAN NOT SEE. Once again pole sana.
 
pole sana bwana ametoa bwana ametwaa jina la bwana libarikiwe
 
pole my dear,nimechelewa kuona hii.
Kweli kuondokewa na mzazi ni jambo gumu sana lakini Mungu atafanya njia na kukupatia faraja.
 
Pole sana....together as one, life has more meaning!
 
Pole sana mpendwa Js, May the comfort of God help you during this difficult time
 
Julito...........aksante kwa shukrani kumbuka Baba yetu ni waridi lililompendeza mwenye bustani hata akaamua kulichuma na ni hakika amelipamba bedroomuni kwake ambako linakuwa la mwisho kuliona kabla ya kulala na la kwanza kuliona aamkapo. Tumshukuru MUNGU kwa hilo

Ni vema tukayatengeneza maisha yetu ili kwamba nasi tukaungane naye katika kumpatia mwenye bustani wetu usiku mwema na habari ya asubuhi kila kukicha

JF inakupenda na iko pamoja nawe
Love you galfriend
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom