Shukrani kwa wana JF

Shukrani kwa wana JF

JS

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2009
Posts
2,064
Reaction score
506
Wapendwa, habarini zenu? Kwanza niwatakie heri ya mwaka mpya wa 2011. Sikupata nafasi ya kuwaambia hivyo kutokana na kutingwa na mambo mengi.


Pia, napenda kuchukua fursa hii kuwashukuruni wote mlionipa support kipindi cha msiba wa baba yangu mpendwa. Kwa kweli nilifarijika sana na salamu za pole/rambirambi kutoka kwa WanaJF walioko sehemu mbalimbali ndani na nje ya Tz.


Baba alikuwa mgonjwa kwa muda mrefu kiasi kuanzia mwezi wa saba. Sisi kama familia tulipokea ugonjwa wake kwa mikono miwili na kumpa huduma ipasavyo. Hata hivyo Mungu alimpenda zaidi na akamchukua tarehe 31 Dec. 2010 usiku tukijiandaa kupokea mwaka mpya.You can all imagine how bad it was. Tulimaliza shughuli zote za maziko salama.


Jana jioni nilipata fursa ya kukutana na baadhi ya WanaJF, nilifarijika sana kuwaona. Kwa kweli through JF I have made myself true friends whom I can count on everything. Asanteni sana Teamo, MJ1, the Finest, GY, LD, Asprin, Acid, St. RR, Askofu, Bigirita, Kimey, Maty, FL1, Dark City, Pearl, Lizzy na wengine wote ambao sijawataja. Na namaanisha WanaJF wote whether nakufahamu in person au sikufahamu, nakushukuru sana. Na poleni kwa wale ambao hamkupata taarifa mapema lakini msijali najua deep down in your hearts hamkupenda iwe hivyo.


Mungu awazidishie baraka tele. Tuendelee na moyo huo huo wa kuwa marafiki wa karibu wakati wa shida na raha. Nawapenda sana.



With much love and appreciation,
JS
 
Pooole sana JS! Tunafurahi mmemaliza mazishi salama! Mungu aendelee kuwapeni nguvu!
 
pOLE SANA BEST...Hilo ndilo neno la juu ambalo kwasasa naweza nikatamka kukupa faraja!
Mungu akufariji zaidi!
 
Mshiki...

Kwa mara nyingine tena: Pole kwa pigo ulilolipata, mipango ya Mungu siku zote haina makosa. Naelewa machungu na pengo ulilolipata, lakini hakuna jinsi, maisha ni lazima yasonge mbele. Katangulia mbele ya haki, nasi tutamfuata huko. Jina la Bwana linapaswa kuhimidiwa. Imeandikwa TUSHUKURU KWA KILA JAMBO. Nasi Tumshukuru Mungu kwa uamuzi alioufanya wa kumtanguliza mzee wetu mbele ya haki.

Tunaendelea kumuombea Mzee wetu apumzike kwa amani. Amen

TUTAONANA PARADISO, KWENYE MJI WA RAHA!
 
pole sana JS...ni habari ya kushtua hii.....binafsi nimeguswa sana...kuondokewa na mzazi ni kitu chenye maumivu mno...Mungu akutie nguvu na uvumilivu....bwana alitoa bwana ametwa....jina lake lihimidiwe
 
How sad it is to lose your beloved one,maanini Mungu anakupa nguvu za kuvumilia haya mapito!
Pole sana
 
There we go JS....maisha yanaendelea.....najua kama familia mmeachiwa nyayo zisizofutika....najua mtamkumba na kuishi pamoja nae (kwa njia ya ya aliyowaachia mioyoni)........
Nakupa pole kwa mapito uliyokumbana nayo...
I am more than glad to have you back! I missed you!
 
Tunashukuru kwa kila jambo, Jina la bwana linapaswa kuhimidiwa tunaendelea kumuombea mzee wetu apumzike kwa amani.

GOD IS GREAT
 
JS,
Pole sana rafiki,
Prayin for u and ur family that God gives u strengths all the way,
And may he rest his soul in peace.
Tuko pamoja.
 
Pole Js,binafsi nlishangaa nilipoona taarifa ya kuwani msiba kwa Js hapa kwenye thread flani. Pole sana ndugu,ila baba akiondoka majukumu unayarithi,pole kwa kuongezewa majukumu na mola ayafanye mepesi. Kila kiumbe kitarudi mahala pake,iyo ndo njia ambayo sote tutaipitia kwa nyakati tofauti. Amina.
 
Bwana ndie mchungaji wako hutapungukiwa na kitu,Mungu akutie nguvu na kuwapa faraja ktk mapito mnyayopitia kama familia,Mungu mwenye rehema awe ndie fimbo na muongozo wenu,Tuzidi kumwombea Baba mpendwa apumzike kwa Amani.
 
Kwa mara nyingine tena pole sana Mdada, Mungu awape nguvu mue na amani na upendo.
Pamoja tutashinda yote. Amen
 
Pole sana na ahsante kwa updates.
Baraka & Rehma zake muumba ziwe nawe/nanyi, nguvu KUU iwe nanyi daima.
 
Yeye aliye Mkuu, anayajua machungu yako na anafanya mambo yake kwa kadiri ya matakwa yake.
Yeye aliye Mkuu akakupe nguvu, sisi tutakuonyesha upendo lakini yeye atakupa Upendo na amani.

Akakutie nguvu kuu, ukazione nyayo za baba yako mpendwa katika upendo wake kwako, msimamo wake kwako na ucheshi wake kwako.......Ukaziishi nyayo hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom