Watoto wako watakaofuata baada yako katika vizazi vya baadaye na wageni ambao watakuja kutoka nchi za mbali, wataona maafa, yaliyoipata nchi na magonjwa ambayo BWANA aliyaleta juu yake. Nchi yote itakuwa jaa linaloungua la chumvi na kiberiti, hakuna kilichopandwa, hakuna kinachochipua, hakuna mimea inayoota juu yake. Itakuwa kama maangamizo ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu ambazo BWANA aliangamiza kwa hasira kali. Mataifa yote yatauliza: "Kwa nini BWANA amefanya hivi juu ya nchi hii? Kwa nini hasira hii kali ikawaka?''
Na jibu litakuwa: "Ni kwa sababu watu hawa waliacha agano la BWANA Mungu wa baba zao, agano alilofanya nao wakati alipowatoa katika nchi ya Misri.Walienda zao na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, miungu wasioijua, miungu ambayo Mungu hakuwapa.Kwa hiyo hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya nchi hii, hivyo Mungu akaleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki. Katika hasira kali na katika ghadhabu kuu BWANA aliwang'oa kutoka nchi yao na kuwasukumia katika nchi nyingine, kama ilivyo sasa.''
KUMBUKUMBU LA TORATI 29: