Shivji: Tanganyika Siijui, Siihitaji

Shivji: Tanganyika Siijui, Siihitaji

Kwa hiyo unakubali wenzako kubaguliwa?
Mkuu hebu jibu swali jepesi tu. Tanzania ni muungano wa nchi huru mbili amambazo ni Tanganyika na Zanzbar. Zanzbar bado ipo kama nchi na kama serikali. I wapi Tanganyika kama nchi na serikali? Na kama Tanganyika haipo iliyeyukia wapi?
 
Muhindi wa India huyu anaongea Pumba siku hizi naona anazeeka Vibaya.... Dengu zimezidi pilipili ameamua kupumua.... Tanganyika huku akisema haijui... hana tofauti na Nyani anayekata tawi alilokalia.... Akianguka ndio atajua Janja yake...
 
Wazanzibari wanajitambulisha kama wazanzibari kwanza na watanzania baadae na wana hisia kali sana kuhusu utaifa wao,na kwa unafiki wenu na usomi wenu hamkosoi wala kuwalaumu,leo hii watanganyika nao wameonyesha kuwa na hisia za utaifa wao wasomi msioelimika mnawashambulia,kwani zanzibar iliungana na nani? German east african au na hiyo tanzania yenu? Kwa nini mnaiogopa tanganyika?
 
Kwakuwa Nilisha sema na kuandika Mawazo yangu juu ya Muundo Wa Muungano wetu Mara kadha na hasa kuhusu dhana ya utanganyika.

ninaomba kuweka Hapa Sehemu Kati ya yale aliyo ya sema Prof. Idea Shivji wakati wa kongamano la vijana hivi majuzi. Msisitizo Zaidi Hasa kwenye Suala la UTANGANYIKA!!

Nanukuu,

"Juu ya hilo la Utanganyika, ningependa kuongeza maneno machache hasa kwa faida ya vijana wetu. Nimeshangaa kidogo kwamba hata mzee na mwanazuoni mwenzangu Prof. Mpangala ametumia msamiati wa ‘Utaifa wa Tanganyika’ bila kudadisi kihistoria ‘Utaifa wa Tanganyika’.

Kwa muhtasari tu, kabla ya vita vya kwanza, hatukuwa na Tanganyika. Tulikuwa na ‘German East Africa’ ambayo eneo lake lilijumuisha Burundi, Rwanda na eneo hilo la ‘Tanganyika’ chini ya himaya ya ubeberu wa Wajerumani. Baada ya Ujerumani kushindwa katika vita, Rwanda na Burundi ziligawiwa kwa Ubelgiji na Tanganyika kwa Uingereza. Waingereza ndipo wakaunda neno hili ‘Tanganyika’ na iliitwa ‘Tanganyika Territory’, yaani, bustani ya wakoloni, siyo taifa.Mababu zetu waliopigania uhuru walijikita kwenye dhana ya Utaifa wa Kiafrika, kama alivyoeleza vizuri tu Profesa Mpangala. Vyama vya wananchi, kutoka TAA (Tanganyika African Association) mpaka TANU (Tanganyika African National Union), viliweka msisitizo kwenye ‘African’, Uafrika wao. Iliwabidi kuweka neno Tanganyika kwa sababu tu ndilo lililokuwa eneo la utawala wa wakoloni.Tulipopata uhuru mnamo Desemba 1961, hatukuwa taifa kwa sababu mkuu wa nchi bado alikuwa Malkia. Mwezi wa Novemba 1962 ndipo tukawa Jamhuri ya Tanganyika wakati Mwalimu alipochaguliwa kuwa Rais. Na Mwalimu tangu mwanzo alisistiza kwamba sisi hatukuwa taifa bali mkusanyiko wa makabila na lilikuwa jukumu la serikali huru kujenga utaifa (nation-building).

Lakini Mwalimu hakupata muda wa kutosha kujenga utaifa wa Tanganyika kwa sababu mwezi Aprili 1964, yaani baada ya miezi 14 tu, tukaungana na Zanzibar kuwa Tanzania. Na kwa takriban nusu karne tumekuwa tunajenga Utaifa wa Tanzania.

Sasa hii dhana ya Utaifa wa Tanganyika, au Utanganyika, unatoka wapi? Na mantiki na historia yake ni ipi?Ningependa kujua hapa tulipo ni vijana wangapi kati yenu mlizaliwa kama Watanganyika. Nyoosheni mikono juu. Nyinyi wote mlizaliwa mkiwa Watanzania, utaifa wenu ni Utanzania; utambulisho wenu ni Utanzania; mnajitambua kama Watanzania na mnatambuliwa na wengine kama Watanzania.Ukweli ni kwamba mking’ang’ania Utanganyika wenu, ambao wala hamjui kama mtakuwa mnavunja taifa, mtakuwa mnatumikia maslahi na matakwa ya mabeberu na wanasiasa wachache wenye uchu wa madaraka. Na Utanganyika wenu hautadumu kwa sababu mtaanza kudai sasa Jamhuri ya Makonde na Jamhuri ya Sukuma! Mtakuwa vipande vipande. Hivi siyo vitisho; kuna mifano hai mbele yetu. Somalia imesambaratika, Libya pia, Sudan, Afrika ya Kati, na nchi nyingine nje ya Afrika – Afghanistan, Pakistan, Syria, Iraq bila kutaja nchi za Ulaya"

- Prof. Issa Shivji 2014.

Comrades, maneno haya ya mwanazuoni huyu nikama ameyasikia kutoka kwangu ama kuyasoma katika kuta zangu katika mitandao mbali mbali,. Sijilinganishi naye., hapana hata kidogo. Ila ninachosema nikwamba mtu yeyote mwenye nia njema na fikira tulivu anaweza kung'amua nia hasa ya wale wanaotupandikiza hisia za utanganyika na uzanzibari. Walafi wamadaraka!!

Nilisha sema na ninasema tena hapa Tanganyika Siijui, na wala Siihitaji.!!

Comrades ninashukuru sana.

kwani shivji na mtanganyika au mhindi!
 
Kwa hiyo Balali kuzikwa Marekani ndio tuseme alikuwa na ngozi ya ki-"Shivji?" Nilishasema huu utanganyika hautaishia kuwabagua tu Wazanzibari, bali tutaanza kubaguana wenyewe kwa wenyewe! Mungu atuepushie mbali na huu msukule wa Utanganyika!
wewe ulishuhudia balali akizikwa?
 
Ni bora angesema Zanzibar ili ungana na Sii Vuzii manake hataki kukubali uwepo wa Tanganyika, pili hao wakoloni wazungu na waarabu mbona wametuachia mambo mengi kwake jina Tanganyika ndo nongwa. Huyu baniani busara yake inamatege?
 
Ndugu Shivji kama uko humu au wafuasi wake kama mpo humu hebu elezeni japo kwa kifupi kuhusu huu muungano. Je, ni nchi ipi na ipi ziliungana ikazaliwa Tanzania? Kama upande wa pili wameamua kujitambua kama nchi huru, kwa mujibu wa marekebisho ya katiba yao ya mwaka 2010, je, upande unaobaki uendelee kujiita jina gani?
 
Mkuu hebu jibu swali jepesi tu. Tanzania ni muungano wa nchi huru mbili amambazo ni Tanganyika na Zanzbar. Zanzbar bado ipo kama nchi na kama serikali. I wapi Tanganyika kama nchi na serikali? Na kama Tanganyika haipo iliyeyukia wapi?

Tanganyika ipi uitakayo, ya Mwingereza au Mjerumani?
 
Shivji kama kasema hayo basi ni mwongo namba mija wala hajui, basi aache wanaojua wazungumzie wanachokijua.

Kwahiyo Zanzibar haikuungana na nchi ya Tanganyika.. . shame on him
 
nani anabaguliwa?
Angalia Post hii hapa chini ndio utaelewa jinsi washabiki wa Utanganyika walivyopinda:
user-offline.png
Male Gigolo

Today 11:53

MemberArray


Join Date : 20th February 2014
Posts : 38
Rep Power : 314
Likes Received9
Likes Given3


[h=2]
icon1.png
Re: Shivji: Tanganyika Siijui, Siihitaji[/h]
Muhindi wa India huyu anaongea Pumba siku hizi naona anazeeka Vibaya.... Dengu zimezidi pilipili ameamua kupumua.... Tanganyika huku akisema haijui... hana tofauti na Nyani anayekata tawi alilokalia.... Akianguka ndio atajua Janja yake...​



I am a Bongo man Male ''Gigolo'' i give Woman Pleasure
 
Kwa hiyo Balali kuzikwa Marekani ndio tuseme alikuwa na ngozi ya ki-"Shivji?" Nilishasema huu utanganyika hautaishia kuwabagua tu Wazanzibari, bali tutaanza kubaguana wenyewe kwa wenyewe! Mungu atuepushie mbali na huu msukule wa Utanganyika!

ujasiri wakukataa kujiona bora zaidi ya mwenzako, moyo wakuchagua kwamakusudi kuutunza umoja na ndugu yako ndio hasa unaoishikilia jamii hii tukufu. Tukikubali kuipoteza hii basi, Adui yetu hasa atakua ameshinda
 
Ok ok if that is the case, tuwe na serikali moja na sio mbili......!!!!!
naunga mkono hoja kama hakuna haja ya tanganyika na zanzibar nia moja=TAN-ZA-NIA nchi iwe ni tanzania isiyotokana na muungano iwe na serikali moja zanzibar iwe mkoa
 
Kwa wale Walio Karibu na Shivji ni vyema wamshauri mzee huyu aache kuendelea kuharibu reputation yake na sasa ajinyamazie na kupumzika katika maisha yake ya ustaafu. Kwa mfano, katika hili la kutoijua na kutoitambua Tanganyika, amedandanya tena. Tazama yafuatayo:

ISSA SHIVJI (2006): Let the people speak: Tanzania Down the road to neoliberalism, page 117, Paragraph 6:

...Whatever form the new unity takes it ought to observe scrupulously the basic democratic principle of the right of people to self determination. This premise has two sides to it.

A) That between Zanziba and Tanganyika, as a people and nations, we would have to respect the principle of equality on the one hand, and be sensitive to the legitimate culture, history and sentiments of both parts, on the other. This means that THOSE OF US who come from the bigger nation, Tanganyika, and consider OURSELVES progressive and democrats, should be extra responsible and cautious in guiding against big nation Chauvism.


Cc: Nguruvi3, mliberali, FJM, tpaul, Pasco, FaizaFoxy, Mtanganyika, MwanaDiwani, gambalanyoka, Ritz, zomba.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nimeuliza hapa, ni yupi Kati yetu anaeweza kujifisia akisema yeye ni mtanganyika zaidi kuliko alivyokuwa Mwalimu Nyerere??! Ni nani?

Kama weye usingejivunia kuitwa Mtanganyika basi una tatizo kichwani. Kama weye huwezi kujivunia kuzaliwa Tanganyika basi weye ni chizi.
Kw vijineno vyako, inaonesha weye ni double id. Shivji inaonesha si mzawa, anajua alichokifanya akaukwaa huo Utanganyika (Utanzania Bara) sasa anaogopa watamnyang'anya uraia wake.
Kila mnapoleta hoja ya kuikataa Tanganyika ati mnaleta hoja mfu ya vita vya kimbari, ukabila na maneno mbofu mbofu yasio na msingi.
Mbona Kenya wanaishi, mbona Uganda mbona Congo DRC ilikataa Uzaire. Poa tu bro. huo usomi wako ni mashaka sana. Uingereza ilitoa uhuru kwa Tanganyika. Nasi Twaitaka
 
Nimeuliza hapa, ni yupi Kati yetu anaeweza kujifisia akisema yeye ni mtanganyika zaidi kuliko alivyokuwa Mwalimu Nyerere??! Ni nani?

Naomba kwanza unijibu hili swali ili twende sawa, nitajie ni nchi gani iliungana na Zanzibar ikapatikana Tanzania!? Hapa nategemea jibu la nchi tu sitaki porojo nyingi mara ilikuwa hivi mara ikawa vile
 
Kwa hiyo Balali kuzikwa Marekani ndio tuseme alikuwa na ngozi ya ki-"Shivji?" Nilishasema huu utanganyika hautaishia kuwabagua tu Wazanzibari, bali tutaanza kubaguana wenyewe kwa wenyewe! Mungu atuepushie mbali na huu msukule wa Utanganyika!
Kaka fikiri nje ya box! Sijasema kuhusu ubaguzi hapo. Kama ungeelewa, nilikuwa ninamaanisha watu wenye uraia pacha hawawezi kuwa na uchungu na nchi zote lazima moja hataitilia maanani. Kama ni suala la rangi mbona Waziri Leader Stirling baada ya kufariki alichomwa na majivu yake yalitupwa hapa hapa Tanzania! Pamoja na hayo, una uhakika gani kama Balali amezikwa US! (tuwekee death certificate hapa)
 
Back
Top Bottom