Shiranga la Mashoga wa Baa ya Stonewall!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,393

stonewall.jpg

Inadaiwa kwamba tukio la awali la serikali yoyote duniani kupambana na ushoga ni lile lililotokea kule Marekani Julai 6, 1969. Mapambano kati ya Polisi wa nchi hiyo yalitokea kwenye kitongoji cha Greenwich jijini New York, kwenye baa iliyokuwa ikifahamika kama Stonewall. Baada ya kuwepo kwa taarifa ya baa hiyo kuwafuga mashoga, polisi waliandaa shambulizi kwa kisingizio cha kumkamata mwenye baa na wanywaji kwa kuendesha biashara ya pombe bila leseni.

Shambulizi dhidi ya baa hiyo lilifanywa saa 6:00 usiku hadi saa 8:00 ikiwa ni saa mbili za kamata kamata. Polisi wa awali ambao walikuwa ni wachache walikaribia kuzidiwa nguvu na mashoga ambapo ilibidi waombe msaada wa kuongezewa nguvu, vinginevyo mashoga hao huenda wangewaumiza au kuwadhuru zaidi. Katika mpambano huo Polisi wanne walijeruhiwa na mashoga kadhaa pia ambapo 13 walikamatwa. Ndani ya baa hiyo inadaiwa kwamba kulikuwa na zaidi ya mashoga au mashoga na wapenzi wao wapatao 200. Baa hiyo inadaiwa kwamba ilikuwa ikiendeshwa na kundi la kigaidi la Mafia.

Habari za shambulizi hilo iliandikwa kwenye gazeti la New York Daily News, la Julai 6 hiyo hiyo, lilinukuu baadhi ya kauli za mashoga hao. Baadhi ya wale walionukuliwa ni pamoja na Erick na Jackson ambao walikuwa ni wachumba na Bruce na Nan ambao pia walikuwa ni mke na mume. Mashoga hao walinukuliwa na gazeti hilo wakilaani shambulio hilo kwani walisema lilikuwa limevuruga harusi iliyokuwa ifanyike Julai 7, yaani siku inayofuata kati ya Erick na Jackson.

Mama mmoja anayeishi jirani na eneo hilo, Shirley Evans aliliambia gazeti hilo kwamba, mashoga kwenye baa hiyo walikuwa ni watu waungwana sana na kamwe hakuwahi kusikia vurugu au ugomvi ndani ya baa hiyo. Kwa hiyo kuvamiwa kwao na Polisi alikuona kama uonevu tu.

Kumbuka hiyo ilikuwa ni mwaka 1969, wakati huku kwetu hata uchangudoa lilikuwa ni jambo la aibu sana na la kushangaza.
 

Kwani Sodoma na Gomorah ilikuwa ni mwaka gani? Haya mambo yapo tangu zama hizo! Tangu Adam na Hawa walipomuasi Mungu...
NImezungumzia kwa huku kwetu Tanzania, jambo hilo la ushoga lilikuwa ni jambo la kufikirika..........................
 
Mh ulizia mwanayamala kuna movement ya mashoga na inakuja juu

Soon utagundua kuwa TZ kulikuwa na mashoga 2000 kila mkoa mwaka 1969
 
Mh ulizia mwanayamala kuna movement ya mashoga na inakuja juu

Soon utagundua kuwa TZ kulikuwa na mashoga 2000 kila mkoa mwaka 1969
najua walikuwepo lakini ilikuwa ni kimya kimya....................Lakini siku hizi.............Mweh!
 
Asante kwa kutujuza hili.

Naomba unitumie ile ya yule
mwanamke wa kibongo aliyemuua mwenzie
sikuwa nimemaliza kuisoma, niwekee hata kwenye PM.
heshima sana kwako kijana wangu.
 
najua walikuwepo lakini ilikuwa ni kimya kimya....................Lakini siku hizi.............Mweh!

Hii inatokana na kukua kwa njia ya upashana habari kuwa rahisi. Siku hizi tukio linatokea unapata taarifa hai (live story) ila enzi hizo mpaka uwe wa ndani(inner circle) ndo ujue...

Hata hivyo hawa jamaa zako kitambo wapo mbali... Just Imagine Titanic ilizama 14/04/1912, huku Tanganyika hata Nyerere Hajazaliwa... si mambo ya ajabu haya...

Na kwenye hiyo Titanic kulikuwa na mashoga eebboooh!...
 
Ukweli ndio huo first lady hawa watu wapo muda mrefu sana hasa pwani hii ya EA
Kuna stori moja tulikuwa tunasimuliana, eti shoga kamuona mwizi akikimbizwa yeye akam-mwagia shombo ya samaki, wale waliokuwa wakimfukuza mwizi wakamuuliza kwa nini hakumkamata yule mwizi yeye akasema, "Nimemwagia shombo ya samaki, akaliwe na paka huko mbele ya safari......." LOL
Najaribu kujiuliza wakati huku kwetu mashoga walionekana laini laini, lakini hawa wenzetu walimudu kupambana na Polisi kwa mtiti wa nguvu hadi ikabidi Polisi waombe msaada wa vikosi zaidi........kumbuka walikuwa hawana silaha!
 
Hivi kuna hisia ipi hapo kati mwanaume na mwanaume kupaishana? duh.... kinyaa sana aise nashindwa hata kuchangia.
 
NImezungumzia kwa huku kwetu Tanzania, jambo hilo la ushoga lilikuwa ni jambo la kufikirika..........................

Acha kusoma historia za kibongo na za mashariki ya kati..Mombasa na zenj km miji ilianza lini?Mercury alikuwa ndiye shoga maarufu kujitangaza wazi ktk vyombo vya habari na kupata support ya mataifa makubwa.Ila hivi vizee vijavyojisifia kwa ubasha along the coast vina miaka mingapi?
 
Kuna stori moja tulikuwa tunasimuliana, eti shoga kamuona mwizi akikimbizwa yeye akam-mwagia shombo ya samaki, wale waliokuwa wakimfukuza mwizi wakamuuliza kwa nini hakumkamata yule mwizi yeye akasema, "Nimemwagia shombo ya samaki, akaliwe na paka huko mbele ya safari......." LOL
Najaribu kujiuliza wakati huku kwetu mashoga walionekana laini laini, lakini hawa wenzetu walimudu kupambana na Polisi kwa mtiti wa nguvu hadi ikabidi Polisi waombe msaada wa vikosi zaidi........kumbuka walikuwa hawana silaha!

Kati ya mashoga si kunawengine ni madume na mengine majike hapo?
Naona yale madume ndiyo yaliyopambana na maaskali.lol!
 

View attachment 51813

Inadaiwa kwamba tukio la awali la serikali yoyote duniani kupambana na ushoga ni lile lililotokea kule Marekani Julai 6, 1969. Mapambano kati ya Polisi wa nchi hiyo yalitokea kwenye kitongoji cha Greenwich jijini New York, kwenye baa iliyokuwa ikifahamika kama Stonewall. Baada ya kuwepo kwa taarifa ya baa hiyo kuwafuga mashoga, polisi waliandaa shambulizi kwa kisingizio cha kumkamata mwenye baa na wanywaji kwa kuendesha biashara ya pombe bila leseni.

Shambulizi dhidi ya baa hiyo lilifanywa saa 6:00 usiku hadi saa 8:00 ikiwa ni saa mbili za kamata kamata. Polisi wa awali ambao walikuwa ni wachache walikaribia kuzidiwa nguvu na mashoga ambapo ilibidi waombe msaada wa kuongezewa nguvu, vinginevyo mashoga hao huenda wangewaumiza au kuwadhuru zaidi. Katika mpambano huo Polisi wanne walijeruhiwa na mashoga kadhaa pia ambapo 13 walikamatwa. Ndani ya baa hiyo inadaiwa kwamba kulikuwa na zaidi ya mashoga au mashoga na wapenzi wao wapatao 200. Baa hiyo inadaiwa kwamba ilikuwa ikiendeshwa na kundi la kigaidi la Mafia.

Habari za shambulizi hilo iliandikwa kwenye gazeti la New York Daily News, la Julai 6 hiyo hiyo, lilinukuu baadhi ya kauli za mashoga hao. Baadhi ya wale walionukuliwa ni pamoja na Erick na Jackson ambao walikuwa ni wachumba na Bruce na Nan ambao pia walikuwa ni mke na mume. Mashoga hao walinukuliwa na gazeti hilo wakilaani shambulio hilo kwani walisema lilikuwa limevuruga harusi iliyokuwa ifanyike Julai 7, yaani siku inayofuata kati ya Erick na Jackson.

Mama mmoja anayeishi jirani na eneo hilo, Shirley Evans aliliambia gazeti hilo kwamba, mashoga kwenye baa hiyo walikuwa ni watu waungwana sana na kamwe hakuwahi kusikia vurugu au ugomvi ndani ya baa hiyo. Kwa hiyo kuvamiwa kwao na Polisi alikuona kama uonevu tu.

Kumbuka hiyo ilikuwa ni mwaka 1969, wakati huku kwetu hata uchangudoa lilikuwa ni jambo la aibu sana na la kushangaza.
kw hiyo mkuu kwa thread hii unataka kutuambia kuwa unaunga mkono hoja ya barack obama....:ranger:
 
kumbe hawa jamaa wakiungana kinanuka.
Naogopa yasije kutukuta
 
View attachment 51813

Inadaiwa kwamba tukio la awali la serikali yoyote duniani kupambana na ushoga ni lile lililotokea kule Marekani Julai 6, 1969. Mapambano kati ya Polisi wa nchi hiyo yalitokea kwenye kitongoji cha Greenwich jijini New York, kwenye baa iliyokuwa ikifahamika kama Stonewall. Baada ya kuwepo kwa taarifa ya baa hiyo kuwafuga mashoga, polisi waliandaa shambulizi kwa kisingizio cha kumkamata mwenye baa na wanywaji kwa kuendesha biashara ya pombe bila leseni.

Shambulizi dhidi ya baa hiyo lilifanywa saa 6:00 usiku hadi saa 8:00 ikiwa ni saa mbili za kamata kamata. Polisi wa awali ambao walikuwa ni wachache walikaribia kuzidiwa nguvu na mashoga ambapo ilibidi waombe msaada wa kuongezewa nguvu, vinginevyo mashoga hao huenda wangewaumiza au kuwadhuru zaidi. Katika mpambano huo Polisi wanne walijeruhiwa na mashoga kadhaa pia ambapo 13 walikamatwa. Ndani ya baa hiyo inadaiwa kwamba kulikuwa na zaidi ya mashoga au mashoga na wapenzi wao wapatao 200. Baa hiyo inadaiwa kwamba ilikuwa ikiendeshwa na kundi la kigaidi la Mafia.

Habari za shambulizi hilo iliandikwa kwenye gazeti la New York Daily News, la Julai 6 hiyo hiyo, lilinukuu baadhi ya kauli za mashoga hao. Baadhi ya wale walionukuliwa ni pamoja na Erick na Jackson ambao walikuwa ni wachumba na Bruce na Nan ambao pia walikuwa ni mke na mume. Mashoga hao walinukuliwa na gazeti hilo wakilaani shambulio hilo kwani walisema lilikuwa limevuruga harusi iliyokuwa ifanyike Julai 7, yaani siku inayofuata kati ya Erick na Jackson.

Mama mmoja anayeishi jirani na eneo hilo, Shirley Evans aliliambia gazeti hilo kwamba, mashoga kwenye baa hiyo walikuwa ni watu waungwana sana na kamwe hakuwahi kusikia vurugu au ugomvi ndani ya baa hiyo. Kwa hiyo kuvamiwa kwao na Polisi alikuona kama uonevu tu.

Kumbuka hiyo ilikuwa ni mwaka 1969, wakati huku kwetu hata uchangudoa lilikuwa ni jambo la aibu sana na la kushangaza.

Kweli Marekani wametutangulia kwa mengi!
 
Back
Top Bottom