Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Ukiona sehemu eneo la ardhi ni cheap kuliko pengine,jua hiyo sehemu pako nyuma kidogo kimaendeleo kulinganisha na hiyo sehemu nyingine.
 
Watu wanaozungumzia mzunguko wa pesa kwenye hii mikoa wanachanganya madesa bila kuwa na uelewa au utafiti wa hali ilivyo kwenye hii mikoa.

Hii mikoa kuna baadhi ya wilaya zina mzunguko wa hela mkubwa kuliko wilaya zingine sababu ziko wazi sana.

Mathalani Tabora wilaya za Nzega na Igunga zina mzunguko mkubwa wa pesa ukilinganisha na wilaya zingine kama urambo, sikonge na Kaliua sababu kubwa ni kuwa wilaya hizo mbili ziko kwenye barabara kuu ya kwenda Mwanza hivyo mwingiliano wa watu ni mkubwa ukilinganisha na wilaya zingine.

Kahama inabebwa na sababu mbili 1 uwepo wa dhahabu 2 kuwepo kwenye barabara kuu inayounganisha Tanzania Rwanda na Burundi do you expect this place to be idle?

Sehemu nyingi zenye wasukuma wengi mzunguko wa pesa lazima uwepo sababu zipo nyingi.
1 Wasukuma wanazaliana sana hivyo population unachangia consumption ya huduma mbali mbali

2 Purchasing power ya wasukuma ni kubwa sana hasa ukizingatia kuwa ni wazalishaji wazuri wa mazao mbali mbali na wafugaji wa kila kitu.

Hivyo hata Tabora sehemu yenye wasukuma wengi biashara huchangamka haraka kuliko maeneo ambayo ni wachache.


Wilaya za urambo sikonge na kaliua zimesthirika na mdororo wa zao la tumbaku ambalo lilikuwa likiingiza pesa nyingi sana kwa wakulima hivyo nakubali kwa sasa kwenye wilaya hizi mzunguko wa pesa umepungua kidogo.
Igunga Luna mzunguko mkubwa kuliko nzega

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shinyanga ardhi ni ghali kwa sababu ya population kuwa kubwa kuliko kawaida.

Wasukuma wanazaliana sana na wameweza kuhamia mikoa ya Tabora ambao kwa sasa 50% ya wakazi ni wasukuma, Katavi almost 30% wakazi ni wasukuma, Sumbawanga 20% wasukuma na Kigoma.

Sasa Shinyanga upatikanaji wa ardhi ni mgumu kwa sababu ya population tu.

Sababu nyingine wasukuma kwa asili yao ya ukulima huwa hawauzi mashamba hovyo hovyo hivyo demand ni kubwa kuliko supply.
Tabora na mikoa jirani wenyeji wanauza maeneo cheaply kwa sababu ya kutokuwa na matumizi nayo.
Ukiona sehemu eneo la ardhi ni cheap kuliko pengine,jua hiyo sehemu pako nyuma kidogo kimaendeleo kulinganisha na hiyo sehemu nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo umezidisha chumvi...nimetoka shinyanga juzi tu, mbona poa sana
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umeongea vema sana, huyo jamaa anitwa Jambo kunaeneo alijenga nyumba yake jirani kabisa a kiwanda chake cha vinywaji baridi, kwa pesa aliokuwa nayo aliweza kupabadilisha sana licha ya kwamba palikuwa pakame kabla hajaweka hiyo nyumba yake, Achana na kitu inaitwa pesa, wapo watu wengi maeneo mbalimbali ya nchi ambayo tunaambiwa yana neema na mizunguko ya pesa lakini ni mafukara wa kutupa, sehemu yeyote mtu unaweza kuishi ilmradi panakidhi na kukupatia kile unachotafuta, sio kweli kwamba ukienda sehemu yenye mzunguko wa hela basi utafika tu na kujazwa mapesa mfukoni, hata huko dar wapo watu ambao kula yao tu ya shida
 
Unataka mji uwe kama kiberiti....utadumaa kwa muda kisha utapanuka na kuamsha tena.
Ni kweli,lazima udumae kwanza baada ya miaka Kama 20 hivi unachangamka,
Kesi Kama Bariadi wao walihamisha stands zao na baada ya miaka 15 kumekaa level
 

Unataka kuharibu uzi wa mwenzio,,,hapo tiari ushaingizi udini. Inamaana waislamu ndio tatizo?? Natamani nikutukane but namuogopa Allah
 
Kati ya shinyanga town na tabora town wapi papo populated zaidi?
 
Nzega kuna future gani si bora useme Igunga utaeleweka.Hata hivyo future na ukuaji wa T
 
Kwenye ishu ya viwanda Shinyanga iko vizuri hii ni kutokana na hali yake ya Tambarare,vingi ya viwanda vilitakiwa kujengwa mwanza sasa jiografia na ufinyu wa ardhi ukatoa faida kwa Shy,is like Pwani na Dar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…