Shinyanga: Afariki kwa kupigwa risasi na wanaodaiwa kuwa majambazi

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,828
21,461
Richard Nzumbe mkazi wa mtaa wa Butengwa Manispaa ya Shinyanga amefariki dunia akidaiwa kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wakati anaingia nyumbani kwake.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 1 usiku wakati akitoka kazini kwake alipofika nyumbani kwake ndipo alishambuliwa na watu hao wanaodaiwa kutaka kumpora fedha.

Akieleza undani wa tukio hilo leo Desemba 19, 2022 Shemeji wa marehemu, Salome Dady amesema majira ya saa 1 usiku walikuwa ndani yeye na watoto wa dada yake, ndipo waliposikia gari la shemeji yake likiwa limefika getini.

Amesema, mmoja wa mtoto alitoka nje kumlaki baba yake na ndipo aliposukumwa na watu hao waliomfuata marehemu kisha kumfanyia unyama huo.

"Mtoto wa dada alikwenda kufungua mlango ndipo nikasikia kelele nje ikabidi nitoke nikaone kuna nini nikakuta watu wawili wanampiga risasi shemeji ikabidi nichukue stuli nikampiga mmoja akaanguka, ndipo wakachukuana wakaondoka," amesema Salome Dady.

Naye Mwenyekiti wa mtaa wa Butengwa, Onesmo Mayenda akizungumzia tukio hilo, amesema majira ya saa 1 usiku alipewa taarifa na wakazi wa mtaa huo na alipofika eneo hilo alikuta washambuliaji hao wameshatoweka.

“Kwa kweli tukio hili ni la kikatili sana na tunalilaani kwa sababu majambazi hawa wametoa uhai wa mtu, ambapo ni kosa la jinai, hivyo tunaliomba Jeshi la Polisi kuwakamata waliohusika,” amesema Mayenda.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema Jeshi la polisi linaendelea na msako wa kina kuwabainisha waliohusika na tukio hilo.

Chanzo: Mwananchi
 
Mshukiwa wa kwanza kwenye hiyo kesi hii ni shemeji wa Marehemu,Salome Dady.

Maelezo aliyotoa yana ukakasi mkubwa sana ,kwamba watu wenye silaha anachukua stuli na kuwapiga nayo. Ninachojua wanawake kiasili ni waoga sana, inawezekanaje Salome akapata ujasiri huo?

Kama sio watu wanaofahamiana ,sidhani kama wangemuacha hai ikiwa aliwaona sura zao. Cha kushangaza majambazi hawaonekani kuhofia kuonekana nyuso zao kwa Salome.

Kwanini hakupiga kelele kuomba msaada na badala yake akachukua uamuzi wa kuchukua stuli na kumpiga?

Makisio yangu yananiambia kuwa Marehemu ni mfanyabiashara . Swali ni Nani mwingine alijua Marehemu ana fedha zaidi ya watu wake wa karibu hususani Salome?

Polisi anzeni na Salome Dady anaujua ukweli wote
 
Mshukiwa wa kwanza kwenye hiyo kesi hii ni shemeji wa Marehemu,Salome Dady.

Maelezo aliyotoa yana ukakasi mkubwa sana ,kwamba watu wenye silaha anachukua stuli na kuwapiga nayo. Ninachojua wanawake kiasili ni waoga sana, inawezekanaje Salome akapata ujasiri huo?

Kama sio watu wanaofahamiana ,sidhani kama wangemuacha hai ikiwa aliwaona sura zao. Cha kushangaza majambazi hawaonekani kuhofia kuonekana nyuso zao kwa Salome.

Kwanini hakupiga kelele kuomba msaada na badala yake akachukua uamuzi wa kuchukua stuli na kumpiga?

Makisio yangu yananiambia kuwa Marehemu ni mfanyabiashara . Swali ni Nani mwingine alijua Marehemu ana fedha zaidi ya watu wake wa karibu hususani Salome?

Polisi anzeni na Salome Dady anaujua ukweli wote
Polisi wenyewe wanakula sahani moja na wahalifu
 
Mshukiwa wa kwanza kwenye hiyo kesi hii ni shemeji wa Marehemu,Salome Dady.

Maelezo aliyotoa yana ukakasi mkubwa sana ,kwamba watu wenye silaha anachukua stuli na kuwapiga nayo. Ninachojua wanawake kiasili ni waoga sana, inawezekanaje Salome akapata ujasiri huo?

Kama sio watu wanaofahamiana ,sidhani kama wangemuacha hai ikiwa aliwaona sura zao. Cha kushangaza majambazi hawaonekani kuhofia kuonekana nyuso zao kwa Salome.

Kwanini hakupiga kelele kuomba msaada na badala yake akachukua uamuzi wa kuchukua stuli na kumpiga?

Makisio yangu yananiambia kuwa Marehemu ni mfanyabiashara . Swali ni Nani mwingine alijua Marehemu ana fedha zaidi ya watu wake wa karibu hususani Salome?

Polisi anzeni na Salome Dady anaujua ukweli wote
Unawajua vzuri wanawake wa kisukuma ww
 
Richard Nzumbe mkazi wa mtaa wa Butengwa Manispaa ya Shinyanga amefariki dunia akidaiwa kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wakati anaingia nyumbani kwake.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 1 usiku wakati akitoka kazini kwake alipofika nyumbani kwake ndipo alishambuliwa na watu hao wanaodaiwa kutaka kumpora fedha.

Akieleza undani wa tukio hilo leo Desemba 19, 2022 Shemeji wa marehemu, Salome Dady amesema majira ya saa 1 usiku walikuwa ndani yeye na watoto wa dada yake, ndipo waliposikia gari la shemeji yake likiwa limefika getini.

Amesema, mmoja wa mtoto alitoka nje kumlaki baba yake na ndipo aliposukumwa na watu hao waliomfuata marehemu kisha kumfanyia unyama huo.

"Mtoto wa dada alikwenda kufungua mlango ndipo nikasikia kelele nje ikabidi nitoke nikaone kuna nini nikakuta watu wawili wanampiga risasi shemeji ikabidi nichukue stuli nikampiga mmoja akaanguka, ndipo wakachukuana wakaondoka," amesema Salome Dady.

Naye Mwenyekiti wa mtaa wa Butengwa, Onesmo Mayenda akizungumzia tukio hilo, amesema majira ya saa 1 usiku alipewa taarifa na wakazi wa mtaa huo na alipofika eneo hilo alikuta washambuliaji hao wameshatoweka.

“Kwa kweli tukio hili ni la kikatili sana na tunalilaani kwa sababu majambazi hawa wametoa uhai wa mtu, ambapo ni kosa la jinai, hivyo tunaliomba Jeshi la Polisi kuwakamata waliohusika,” amesema Mayenda.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema Jeshi la polisi linaendelea na msako wa kina kuwabainisha waliohusika na tukio hilo.

Chanzo: Mwananchi
Kwa maelezo ya shemeju, inaonekana hayo ni mauaji ya kupanga na siyo tukio la ujambazi.

Mungu ampokee mja wake
 
Huko alipotoka kuna watu walimsoma,wakamfatilia na kumlia timing....
Mambo ya pesa yanatakiwa siri sana
Sasa kama wewe unabeba pesa huku ukifanya matangazo basi hapo utakuwa unajihatarisha maisha

Ova
 
Planned event,hapo inabidi waanze na chain yote ya watu wa ofic yake adi marafiki waliokuwa wakiongea Kwa cmu kuhusu pesa.
 
Back
Top Bottom