Neno la Mungu ktk kitabu cha Mithali 14:12 linasema,ipo njia ionekanayo sahihi machoni pa mwanadamu lakini mwisho wake ni njia ya mauti,mdogo wangu tayari umesahau ulipotoka mara hii tu?
Hivi unapata wapi ujasiri wa kuchukua kalamu na kuandika kuwa Magufuli ndiye suluhisho la matatizo ya watanzania?
Umejuaje wakati hata ikulu hajaingia? Kwanini umekuwa mtu wa kujipendekeza sana kwa serikali? Umesahau kuwa umaskini uliowatesa wazazi wako ulisababishwa na serikali ya CCM?
Hujui kuwa aliyekuinua wewe kiuchumi siyo CCM bali ni Mungu wako? Watanzania wenzako wanaoteseka na maisha magumu yaliyosababishwa na CCM umewasahau na kukumbatia serikali hii isiyo na upendo na watu.
Kwa taarifa yako CCM wanakupenda kwa kuwa unacho, ungekuwa kapuku usingemjua JK wala Pombe, wanakupenda kwa kuwa una media na unawafagilia.
Mtu yeyote mwenye hofu ya Mungu hachangamani na watawala wabovu na wala kunywa divai yao, hebu msome nabii Elia, unajiona uko sahihi sana kumbe unapita katika njia ambazo ni machukizo ya Mungu na hutaikwepa ghadhabu.
Ukiwa mmiliki wa vyombo vya habari ambavyo havifungamani na upande wowote kisiasa si vema kuegemea sehemu moja na ukiegemea upande mf. wa serikali basi tunasema unatafuta favored. Lakini kama comment moja hapo juu kuhusu imani yake kutoka huko nyuma. Ninavyo wafaham #WASABATO wanafundishwa maadili nyumbani, kanisani na popote walipo na mtu akiamua kutanga mbali basi ni yeye mwenyewe ila nafsi yake itaendelea kukumbuka alichopewa.
Halafu hakomi si wakati ule alikatwa huyu!Mkuu upo sahihi kabisa, huyu jamaa amekuwa akijipendekeza ccm muda mrefu kabisa
Ivi shigongo ndio yule muandishi wa riwaya za mapenzi,ngono na udaku. sasa kujipendekeza kote huko kwa ccm alifikiri siasa ni kama tungo za kimapenzi au mahaba niue. alishafanya the same thing uchaguzi wa 2010 na leo anataka kurudia tabia yake ya kidhalimu kwa kupotosha uma wa watz. watanzania wa 2015 hawadanganyiki, wanataka mabadiliko. mwaka huu twende na Lowasa kwa mabadiliko ya kweli, dhamira ya kweli katika kutengeneza tanzania mpya na yenye usawa, serekali sikivu na rafiki kwa kila kada. Ninaimani Lowasa anaweza.