Pasco,
Kwa kawaida yangu huwa sipendi unafiki na longolongo za kisiasa kama zinavyofanywa na chama chako cha CCM. Umafia na ubabe wa kupora haki za walio wengi na kuzigeuza kuwa kinyume ili zionekana ndiya mawazo ya CCM!!!
BMK tunajua, hata CCM wanajua kabisa kuwa Katiba Inayopendekezwa si MAONI YA WATANZANIA YALIYOKUWEMO KWENYE RASIMU
#2 Iliyotokana na Tume ya Jaji Warioba. Hili ni jambo liko wazi na halina ubishi.
Tunajua namna SS na Andrew Chenge walivyocheza na namba za Wajumbe hasa kutoka Zanziba ili kutengeneza theluthi 2(2/3) ya BANDIA. Tumeshuhudia Mjumbe mmoja mtu mzima akilia mbele ya media kwa jina lake kuingizwa kwa kughushi ili kupata 2/3. Tumeshuhudia SS na Chenge wakihaha kulaghai watu kuwa Wajumbe waliokuwa nje ya Nchi walokuwa wameenda kuhiji na hospitali kuwa walipiga kura kwa FAX na MITANDAO kitu mabacho si kweli na ni kinyume na sheria za BMK!!!!
BMK limekosa maridhiano na hivo limekosa uhalali na utashi wa kisiasa na hivo kupoteza haki ya kuwapatia Watz waliowengi Katiba BORA nayopendekezwa. Twendeni tunavoenda lakini nina hakika kabisa kuna madudu yataenda kuibuka huko mbele hata kabla ya KURA YA MAONI na ndo utakuwa mwisho wa Katiba ya CCM inayopendekezwa.
Tusubiri tu, kwani siku hazigandi. Time gonna tell.