salum bin hassan
Member
- Sep 17, 2014
- 38
- 35
CHADEMA wanakwepa kiini cha tatizo. Tatizo sio SHIBUDA. wameingia ndani ya bunge la katiba bila ya ajenda na walivyotoka nje wameshindwa kushawishi watanzania kujitoa muhanga. Shibuda alikuwa na ajenda ya wakulima na wafugaji. Kura ya maoni itathibitisha alikuwa sahihi pale theluthi mbili ya Tanzania bara itakapo piga kura ya ndio.
Shibuda kipau mbele chake ni masilahi ya wakulima na wafugaji sio kufurahisha CUF kwa kudai serikali tatu.
Sio polisi waliofanya maandamano na migomo ishindwe, bali ni uongozi wa chadema kukosa ushawishi. Unajuwa kabisa kilichofanya maandamano yashindwe kufanikiwa ni viongozi wa chadema kushindwa kushawishi watanzania wasiogope polisi. Viongozi wa chadema wanatakiwa waje na ajenda itakayo gusa hisia na mioyo ya watanzania kiasi cha kuwapa ujasiri wa kupambana na polisi.
Kilichotokea mashariki ya kati (uarabuni) ni watu kuguswa na ushawishi wa wanaharakati; yule mtu aliyejichoma moto mbele ya kituo cha polisi aliwasha moto ambao tayari ulikuwa unangojea kuwaka.
Huwezi kutegemea ajenda ya serikali tatu kumgusa mtanzania wa kawaida ambaye anataabika kupata ugali wake wa kila siku. Mtanzania wa kawaida haelewi serikali tatu itamsaidia vipi au itarahisisha vipi kupata ugali wake wa kila siku. Huwezi kutegemea ajenda ya serikali tatu kumpa ujasiri mtanzania wa kawaida kwenda kupambana na polisi. Na mbaya zaidi pale anapoambiwa kiongozi mwenye ajenda ya serikali tatu kaenda vakesheni nje nchi.
Kama kweli unataka kutoa ushauri wa kusaidia chadema, uongozi unapokosea lazima uwe na ujasiri wa kuwaambia ukweli.
Zaidi ya asilimia 70% ya watanzania ni wakulima na wafugaji, kwahiyo Mh. Shibuda alivyokuwa anawaambia ajenda iwe haki za wakulima na wafugaji alikuwa anatumia uzoefu wake kuwaambia ajenda itakayogusa mioyo ya watanzania ni ile ya wakulima na wafugaji.
Mbowe upeo wake mdogo umeshindwa kuelewa kwamba Tundu Lissu anasifa mbili tu, sifa nyingine muhimu hana, na kumfanya kuwa mshauri mkuu ni makosa. Sifa za Tundu Lissu ni usomi wa sheria na uaminifu. Hana uzoefu wa siasa wala uwezo wa kufanya maamuzi sahihi (He lacks experience and sound judgment).
Unaweza kuona hata humo ndani ya bunge la katiba vipau mbele vya Tundu Lissu au Ukawa vilivyokuwa vinabadilika. Ni kama mtu anayepapasa kwenye giza ambaye hajuwi ashike wapi. Alianza na hati ya muungano haipo, wanaushahidi kutoka umoja wa mataifa kuwa haijapelekwa, wakaamia tunatukanwa ndio maana tunatoka bungeni, baada ya hapo wakasema rasimu inapendekeza serikali tatu lakini CCM wanataka serikali mbili.
Lakini pia ikumbukwe humo ndani ya Bunge ya katiba, kuna wajumbe walihoji utaratibu uliotumika kukusanya maoni ya wananchi kwamba hauwakilishi sura halisi ya matakwa ya wananchi; ukasanyaji maoni ulipuuza baadhi ya maeneo (yaani bad sampling). hivyo hata hayo maoni yaliyoletwa na Warioba yanakosa uhalali kwasababu utaratibu wa ukusanyaji haukuwa sahihi.
Chadema kukosa dira au ajenda inaonekana pia kwenye operesheni zao; ukiangalia operation sangara, movement for change hakuna hata moja tuliyoona imefikia malengo fulani, zinayayuka hewani.
Hapa ndipo unapoona umuhimu wa uzoefu wa watu kama Shibuda. Kama ushauri wao ungekuwa unazingatiwa, sasa hivi CHADEMA ingekuwa inaonekana inapigania haki za wakulima na wafugaji sio serikali tatu ambazo hazi resonate to average Tanzanian. Mtanzania wa kawaida haelewi serikali tatu zitamsaidia vipi kuleta ugali nyumbani.
Msimamo wa kung'ang'ania serikali tatu ni ajenda ya kujenga mahusiano mazuri na CUF lakini sio ajenda ya kumtatulia mtanzania wa kawaida (mkulima, mfugaji, mvuvi) shida zake. Sasa Chadema watuambie watu wa tanzania bara ni masilahi ya kundi gani hayajazingatia katika katiba iliyopendekezwa.
Shibuda kipau mbele chake ni masilahi ya wakulima na wafugaji sio kufurahisha CUF kwa kudai serikali tatu.
Sio polisi waliofanya maandamano na migomo ishindwe, bali ni uongozi wa chadema kukosa ushawishi. Unajuwa kabisa kilichofanya maandamano yashindwe kufanikiwa ni viongozi wa chadema kushindwa kushawishi watanzania wasiogope polisi. Viongozi wa chadema wanatakiwa waje na ajenda itakayo gusa hisia na mioyo ya watanzania kiasi cha kuwapa ujasiri wa kupambana na polisi.
Kilichotokea mashariki ya kati (uarabuni) ni watu kuguswa na ushawishi wa wanaharakati; yule mtu aliyejichoma moto mbele ya kituo cha polisi aliwasha moto ambao tayari ulikuwa unangojea kuwaka.
Huwezi kutegemea ajenda ya serikali tatu kumgusa mtanzania wa kawaida ambaye anataabika kupata ugali wake wa kila siku. Mtanzania wa kawaida haelewi serikali tatu itamsaidia vipi au itarahisisha vipi kupata ugali wake wa kila siku. Huwezi kutegemea ajenda ya serikali tatu kumpa ujasiri mtanzania wa kawaida kwenda kupambana na polisi. Na mbaya zaidi pale anapoambiwa kiongozi mwenye ajenda ya serikali tatu kaenda vakesheni nje nchi.
Kama kweli unataka kutoa ushauri wa kusaidia chadema, uongozi unapokosea lazima uwe na ujasiri wa kuwaambia ukweli.
Zaidi ya asilimia 70% ya watanzania ni wakulima na wafugaji, kwahiyo Mh. Shibuda alivyokuwa anawaambia ajenda iwe haki za wakulima na wafugaji alikuwa anatumia uzoefu wake kuwaambia ajenda itakayogusa mioyo ya watanzania ni ile ya wakulima na wafugaji.
Mbowe upeo wake mdogo umeshindwa kuelewa kwamba Tundu Lissu anasifa mbili tu, sifa nyingine muhimu hana, na kumfanya kuwa mshauri mkuu ni makosa. Sifa za Tundu Lissu ni usomi wa sheria na uaminifu. Hana uzoefu wa siasa wala uwezo wa kufanya maamuzi sahihi (He lacks experience and sound judgment).
Unaweza kuona hata humo ndani ya bunge la katiba vipau mbele vya Tundu Lissu au Ukawa vilivyokuwa vinabadilika. Ni kama mtu anayepapasa kwenye giza ambaye hajuwi ashike wapi. Alianza na hati ya muungano haipo, wanaushahidi kutoka umoja wa mataifa kuwa haijapelekwa, wakaamia tunatukanwa ndio maana tunatoka bungeni, baada ya hapo wakasema rasimu inapendekeza serikali tatu lakini CCM wanataka serikali mbili.
Lakini pia ikumbukwe humo ndani ya Bunge ya katiba, kuna wajumbe walihoji utaratibu uliotumika kukusanya maoni ya wananchi kwamba hauwakilishi sura halisi ya matakwa ya wananchi; ukasanyaji maoni ulipuuza baadhi ya maeneo (yaani bad sampling). hivyo hata hayo maoni yaliyoletwa na Warioba yanakosa uhalali kwasababu utaratibu wa ukusanyaji haukuwa sahihi.
Chadema kukosa dira au ajenda inaonekana pia kwenye operesheni zao; ukiangalia operation sangara, movement for change hakuna hata moja tuliyoona imefikia malengo fulani, zinayayuka hewani.
Hapa ndipo unapoona umuhimu wa uzoefu wa watu kama Shibuda. Kama ushauri wao ungekuwa unazingatiwa, sasa hivi CHADEMA ingekuwa inaonekana inapigania haki za wakulima na wafugaji sio serikali tatu ambazo hazi resonate to average Tanzanian. Mtanzania wa kawaida haelewi serikali tatu zitamsaidia vipi kuleta ugali nyumbani.
Msimamo wa kung'ang'ania serikali tatu ni ajenda ya kujenga mahusiano mazuri na CUF lakini sio ajenda ya kumtatulia mtanzania wa kawaida (mkulima, mfugaji, mvuvi) shida zake. Sasa Chadema watuambie watu wa tanzania bara ni masilahi ya kundi gani hayajazingatia katika katiba iliyopendekezwa.