KATIBU NA MTENDAJI MKUU CHADEMA (DR SLAA) TAFADHALI TUPE RIPOTI YA MAREJESHO YA UTENDAJI KAZI BORA WA VIONGOZI WETU ILI TUPATE KUBAINI MBEGU ZA 'VIONGOZI BORA' NA WALE 'BORA VIONGOZI'
Baada ya mapendekezo ya UTARATIBU GANI KUFUATA KUPATA VIONGOZI ndani ya CHADEMA, sasa naomba nichukue fursa hii kumpa changaamoto Katibu Mkuu wetu Dr Slaa kwamba awe anachapisha magazetini ripoti ya MAREJESHO YA VIONGOZI WA CHADEMA NA UBORA WA UTENDAJI WAO KAZI walau mara moja kwa mwaka.
Huko tuendako, endapo CHADEMA tutazingatia mapendekezo kwenye mchango namba 70 ndani ya uzi huu hapa, watu tutaanza kusikia SIASA ZA KOO ZA 'UTENDAJI ULIOTUKUKA' na SIASA ZA UKOO WA 'UADILIFU USIO NA MAWAA' taratibu zikichukua nafasi za SIASA ZA KIZAMANI KULE CCM ambazo siku zote ni SIASA ZA 'KUBAHATIKA KUZALIWA KATIKA KOO TEULE ZA UONGOZI NCHINI' na zile siasa za 'UNAMJUA NANI NEC TAIFA NA UNAYO KILO NGAPI YA KUWEZA KUHONGA' au wakati mwingine tu ni kuzingatia SIASA VIWANGO VYA KUFUZU UPIKAJI MAJUNGU, FITINA, NA KUWAPORA WATANZANIA RASLMALI NA HAKI ZAO ZA MSINGI eti kwa jina na faida ya chama - CCM.
Watu tunakusudia kuondoka huko na kuleta mpambazuko mpwa wa siasa za HAKI, UTENDAJI ULIOTUKUKA na UADILIFU USIO MAWAA kwa kuzingatia njia za kupimika kisayansi na rekodi ambazo kamwe hazitowekwa SIRI KUU kwa macho ya Vikao vya NEC tu jinsi wenzetu CCM wanavyofanya hivi sasa.
Sasa ili Katibu Mkuu wa CHADEMA aweze kuonekana kuwa FAIR katika kutangaza wazi RIPOTI YA MAREJESHO YA UBORA WA UTENDAJI KAZI WA VIONGOZI WETU CHAMANI NA NDANI YA 'SERIKALI YA CHAADEMA', itakua ni vema kwake kuzingatia MIJUMUISHO MITATU ya ripoti za utendaji wa kila kiongozi na kuitengeneza kuwa ripoti moja inayozingatia vipindi 3 tofauti ili ndio picha halisi iweze kujiweka wazi kwetu sisi wanachama wa kawaida na Umma wa Tanzania kwa ujumla wake.
Naam, ninachokisema hapa ni kwamba mathalan tuchukulie kwamba kila kiongozi wa CHADEMA wa hivi sasa ameingia MKATABA WA UTENDAJI KAZI BORA na kwamba tathmini ya utendaji kazi wa afisa huyo husika hupimwa kila baada ya miezi mitatu ofisini kisha RIPOTI YA MAREJESHO YA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI WAKE (CHADEMA Public Officer Quarterly Performance Appraisal Report - inayoainisha vigezo mbalimbali ndani mle) kutolewa na yeye kupewa nakala; itakua ni jukumu la Katibu Mkuu kutoa marejesho pia kwa wenye chama ambao ni sisi wanachama wa kawaida na umma wa Tanzania kwa ujumla wetu ili tupate kujua kama kweli tunaye kiongozi wa kutumainika katika ngazi husika au ni mzigo wa kuni tu.
Kwa namna hii ya chama kuwa na utaratibu wa wazi na unaopimika kisayansi kupiga chekecha maafisa wake, vivyo hivyo serikali itakayozaliwa na chama cha siasa chenye mfumo kama huu itaakua ni serikali yenye watendaji madhubuti na waadilifu wenye dalili zote za kuweza kutufikisha huko tunakodhamiria kwenda KIUCHUMI, KISIASA na KIJAMII. Kwa lugha nyingine, kwa utaratibu kama huu SIASA NCHINI TANZANIA ITAKOMA KUENDELEA KUWA PANGO LA WANYANG'ANYI ambako mfisi wote katika jamii hukimbilia kwa utajiri wa kimapepo.
Great Thinkers, sasa karibu tukosoleane na au kuboreshana mawazo hapa ili na sisi huku CHADEMA tukija kushika dola mnamo 2015 mambo yasije yakawa ni yale yale tunayoyakataa leo endapo utaratibu unaopimika kutekeleza wajibu chamani na ndani ya serikali haitokwepo.
Remember, mine is a real fight for a change of systems and structures on the way we operate as a government that is down-bent to benefit tax-payers at all costs throught varifiable checks and balances,and not merely making aa change of political faces that are heavily armed with lethal streak of arsenals of trendy unrealistic honey-sweet political slogans (Maisha bora kwa kila Mtanzania na kuishia na Bora maisha kwa kila Mtaanzania) that bears no impact to the masses of this country.
Ndio, mine is a brutal fight for a change that face-lifts the way we operate and carry ourselves in public office in a manner that easily predictable to trickle down benefits to citizens and not syphoning public finance from public coffers to a heavenly-safe Swiss bank that only facilitates job creation outside our borders.