Kichama Shibuda hana nguvu, anaweza kuwekewa mkakati, akafukuzwa uanachama na kupoteza hata ubunge.
Kinachwapa watu maswali hapa ni, Shibuda anathubutu vipi kuwa na kiburi hiki? Je, kashajichukulia siri nzito za CHADEMA kiasi cha kuweza kubwabwaja bila kuogopa huku akijua kwamba inawawia vigumu CHADEMA kumfukuza kwa kuwa wanajua ana siri za uongozi wa juu wa chama?
Mkuu ni kweli jamaa ana kiburi, lakini mimi nakiita si kiburi bali ni kubuni mbinu kuchanganya akili za watu, huyu huyu alitishia kugombea urais apingane na JK watu wakahofu sana, akawachanganya watu kwa muda then akasema Hagombei tena.
Anajua wanaweza kumfukuzwa, sasa anachofanya ni kuwafanya watu wote tuwe attention tuumize vichwa vyetu kujiuliza hizi guts za kusema nifukuzeni muone kazipata wapi? kifupi jamaa hana lolote na nawaambieni kama kuwa fired atakuwa fired tu.
Na endapo ataanza kuitisha mikutano kukiponda chadema yatamkuta ya Mch. Mtikila alipotaka kutafuta umaarufu wa kutumia jina la marehemu Wangwe kujinadi - yaliyomkuta jukwaani Tarime hatakaa ayasahau hadi leo.