jockey emmanuel
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 330
- 50
Kwenye msafara wa mamba na kenge lazma wawepo
<br />Mkuu Zitto mwenyewe kathibitisha hilo na kuelezea mbinu anazotumia kukataa posho. Wengine wote wanapokea tena kwa moyo uliokunjuka na mikono miwili. Anayeweza kusema against posho ndani ya CHADEMA ni Zitto tu wengine wote kimya. Regia yupo humu pamoja na Mbunge wangu Ndugu Mnyika mbona hawajatoa kauli kama hawachukui posho za vikao?[/QUOTE<font size="4">]ILE SIO POSHO NI UJIRA WA MWIHA</font>
<br /> Kumbuka kuwa Zitto anaonekana kwa vile ni waziri Kivuli wa Fedha na hiyo ndio sera ya CDM lazima aishikilie hivyo kumbuka hii ni sera ya CDM ni ya chama c ya Zitto,na c kila mbunge atoe kauli yake humu au bungeni, cha msingi SHIBUDA aliingia CDM kwa bahati mbaya hivo kama hafahamu mlango wa kutokea aoneshwe,bora tujue ya kwamba moyo na fikra za SHIBUDA ni za CCM na yeye ni CCM mwenye kadi ya CHADEMA.
Zaidi ya yote yanayosemwa kuhusu Mhe. Shibuda, kwa kuongezea tuu, Mhe. huyu Shibuda ni mtu asiye na shukrani kabisa katika madogo, wala hakumbuki fadhila!.
Aliposhikiliwa kwa kubambikiwa kesi ya mauaji wakati wa kampeni, alisambaza ujumbe mfupi wa sms za kuomba msaada wa fedha kwa marafiki zake na hata kwa wasio marafiki lakini wanaojuana kisiasa. Japo aliwekwa chini ya ulinzi, lakini aliwekwa ki VIP fulani akiwa na simu yake ya mkononi.
Kwenye sms hiyo, alieleza jinsi anavyoteseka mahabusu ya polisi, na kumalizia kuwa amenyanga'nywa kila kitu mpaka kadi zake za ATM, hivyo anaomba msaada kidogo wa tulaki tuwili tutatu kusaidia familia yake kwa chakula. Ujumbe huu, ulimfikia mshirika wangu wa karibu na ikatokea bahati mbaya mshirika huyu naye ujumbe ulimkuta akiwa katika hali mbaya, ndipo akaweka wazi kwa watu wake wa karibu.
Ikapitishwa harambee ya papo kwa papo, kikapatikana kiasi kuliko kilichoombwa, akapigiwa simu kuulizwa zitamfikiaje, hata bila kujibu ile simu au japo kusema asante, alimkatia jamaa sumu sikioni na mara jamaa ilipigwa simu na mtu aliyejhitambulisha katumwa na mheshimiwa kukusanya hicho chochote kitu, na mara alielekezwa zilipo akazipitia.
Yule mjumbe akarudisha ujumbe, mzigo umemeshamfikia mlengwa kwa kuutuma kwa mtu, ambaye amemfikishia rasmi mheshimiwa wetu, jamaa yangu akitegemea japo sms nyingine toka kwa mhishimiwa ya kushukuru, japo aliomba kidogo, amepewa mara dufu ya alichoomba, akitegemea jamaa ange appreciate kwa hilo lililofanyika ndani ya muda wa lisaa limoja tuu, lakini no!. Hakuna cha shukrani, wala asante!.
Hata baadaye walipokutana na Shibuda viwanja vya bunge, alianza kwa kumpongeza kwa ushindi wa ubunge, na kuulizia vipi maendeleo ya kesi, na jee kale kamzigo kalifika na kama kalisaidia kitu, jibu likawa kalifika, akitegemea basi japo kaasante kangetoka, lakini wapi!.
Jamaa alipoturudishia feedback kumbe jamaa hata shukrani hana, sisi tulisisitiza kuwa lengo letu lilikuwa ni kutenda wema tuu na kuendelea na maisha yetu na sio kusubiria shukrani.
Mtu asiyekumbuka fadhila na kushukuru kwa madogo kama Mhe. Shibuda, Chadema isitarajie hisani, fadhila wala shukrani yoyote kutoka kwake, sana sana, isubiri kuambulia matusi ya haja, mara atakaporejea nyumbani CCM baada ya ziara ya kutembelea Chadema!.
Pamoja na kasoro za Shibuda Haya mengine ni majungu na fitna tu, jengeni hoja banaMh. Shibuda, hivi kweli wewe unasema mbele za watu na unajidai kwamba wana-Maswa ni wako! Umesahau vijana tuliokusaidia kwa hali na mali maana ulikuwa huna uwezo wa kushinda. Kwanza Shibuda ulikuwa na doa la kumchezea mchezo mchafu JIDULA MABAMBASE ambaye alikufa mda si mrefu wakati wa kura za maoni za CCM. Sisi vijana wa Maswa tunafahamu hata waganga wako (kamati ya ufundi), ulikuwa na waganga saba, ulienda siku moja kwa mganga wako wa Malampaka na alikutabiria mambo yako kuwa hayakuwa mazuri, vijana wa Kizungu, Dodoma, Kadoto, shishiyu,Mwabayanda wote kwa sasa tunakushangaa na tunakuona huna fadhila. Wananchi wa Maswa tunataka mageuzi na mageuzi yataletwa na CHADEMA hakuna chama mbadala kwa sasa zaidi ya CDM. Kama unajidanganya unamtaji Maswa, sahau wananchi wameshakutoa maana.
Kamtetee Mtatiro anasema CDM hawana nguvu Igunga, halafu anaanza kulalamika kuwa CDM watagawa kura za CUF.....sasa kama CDM hawana nguvu watagawaje kura za chama ngunguri??Ndani ya CDM ukiwa mkweli unajichimbia kaburi!! Wangwe alijichimbia kaburi baada ya kuhoji ruzuku zinatumikaje. Bado kuna wasaliti wengi tu ambao wanachukua posho za vikao ilihali CDM walishakubaliana kwamba posho za vikao ni haramu. Hawa nao wanatakiwa watendewe haki yao.
Kamtetee Mtatiro anasema CDM hawana nguvu Igunga, halafu anaanza kulalamika kuwa CDM watagawa kura za CUF.....sasa kama CDM hawana nguvu watagawaje kura za chama ngunguri??
Ndani ya CDM ukiwa mkweli unajichimbia kaburi!! Wangwe alijichimbia kaburi baada ya kuhoji ruzuku zinatumikaje. Bado kuna wasaliti wengi tu ambao wanachukua posho za vikao ilihali CDM walishakubaliana kwamba posho za vikao ni haramu. Hawa nao wanatakiwa watendewe haki yao.
hacha uhayawani wewekitu ambacho chadema hawawezi kuthubutu ni kumuondoa shibuda, wanajuwa wakifanya hivyo ndio kifo chao, kama wanabisha wamuondoe halafu waone nini kitafata.
Mkuu nimtetee Mtatiro kwa nini? Hilo halihitaji utetezi ni suala la upinzani kukubaliana tu kwamba nani aachiwe baada ya kupima upepo. Lakini CDM walivyo na uroho wa madaraka hata kama hawakubaliki mahala wanaenda tu kugawa kura za wapinzani na matokeo yake: CDM 5, CUF 8, CCM 10!! CCM anatangazwa mshindi kwisha habari.
Mkuu nimtetee Mtatiro kwa nini? Hilo halihitaji utetezi ni suala la upinzani kukubaliana tu kwamba nani aachiwe baada ya kupima upepo. Lakini CDM walivyo na uroho wa madaraka hata kama hawakubaliki mahala wanaenda tu kugawa kura za wapinzani na matokeo yake: CDM 5, CUF 8, CCM 10!! CCM anatangazwa mshindi kwisha habari.
Kitu ambacho CHADEMA hawawezi kuthubutu ni kumuondoa Shibuda, wanajuwa wakifanya hivyo ndio kifo chao, kama wanabisha wamuondoe halafu waone nini kitafata.