Sheria ya Umiliki wa Rasilimali na Maliasili iliyotungwa Awamu ya Tano, chini ya Hayati Magufuli

Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Feb 26, 2021
949
2,865
Ikumbukwe wakati sheria ya kulinda rasilimali za taifa inatungwa mwaka 2017 Mh Waziri mkuu alikuwepo,Spika alikuwepo wakati huo alikuwa Naibu Spika,Rais alikuwepo wakati huo alikuwa Makamu wa Rais,Waziri wa fedha alikuwepo wakati huo alikuwa Waziri wa Sheria, na wabunge waliopitisha bungeni ni awa awa wa CCM, watu ni walewale na chama ni kilekile waliotaka na kuona kuna umuhimu wa kutunga sheria ya kulinda rasilimali za taifa lakini sasa ni haohao hawaitaki tena hiyo sheria, wanaona hamna haja ya kuwa na sheria hiyo tena ya kulinda rasilimali za taifa.!

Wananchi wanapiga kelele wanasema ibara ya 20 katika mkataba wa bandari ibadilishwe kwa kuwa inakwenda kinyume na kifungu cha 11 cha sheria ya mamlaka ya nchi kuhusiana na umiliki wa rasilimali na maliasili zetu,sheria ya mwaka 2017 aliyoipitisha Hayati Rais John Pombe Magufuli (The natural wealth and resources permanent sovereignty) act no 5 ya mwaka 2017 inayosema mgogoro wowote wa rasilimali na maliasili ya nchi utatatuliwa hapa hapa Tanzania na kwa sheria za Tanzania, sio kwenda nje ya nchi wakati rasilimali na maliasili ni zetu.

Kama kweli wanataka kufuta sheria hiyo aliyoipitisha Hayati Rais Magufuli, Swali langu ni hili.

Je wakati wanaitunga na kuipitisha hii sheria waliipitisha kwa kuwa walikuwa na uchungu wa rasilimali za taifa kutoka moyoni? Au walipitisha tu kwa sababu tu Rais alikuwa ni Magufuli?

#WatanzaniaTuipendeNchiYetu.
 
Kwa upande wa CCM, mwenyekiti wao ambaye ni rais anaabudiwa zaidi ya Mungu. Anaweza kuamrisha jambo lolote hata kama lipo kinyume na amri za Mungu, kisha wapambe wake ambao ndiyo wateule wa nafasi mbalimbali anazoteua mwenyewe wataimba mapambio na sifa.

Leo ikitokea mwenyekiti wao akitamka tuandike katiba mpya, wote watazunguka nchi nzima kushangilia. Akitamka tena kesho kuwa ameikataa, watanyanyuka na kumwimbia sifa.

Huyu wao ni zaidi ya Mungu. Ndiyo maana wameamua kumjengea masanamu (mabango) nchi nzima ya kumkweza wakiandika Amemzidi mpaka Mwenyezi Mungu (Eti ni nani kama mama).
 
Kwa upande wa CCM, mwenyekiti wao ambaye ni rais anaabudiwa zaidi ya Mungu. Anaweza kuamrisha jambo lolote hata kama lipo kinyume na amri za Mungu.

Leo ikitokea mwenyekiti wao akitamka tuandike katiba mpya, wote watazunguka nchi nzima kushangilia. Akitamka tena kesho kuwa ameikataa, watanyanyuka na kumwimbia sifa.

Huyu wao ni zaidi ya Mungu. Ndiyo maana wameamua kumjengea masanamu (mabango) nchi nzima ya kumkweza wakiandika Amemzidi mpaka Mwenyezi Mungu (Eti ni nani kama mama).
Umepiga mule mule
 
Kwa CCM chochote kinawezekana, msemo wa chini ya jua hakuna kinachoshindikana unafanya kazi kikamilifu ccm.

Katika ccm kipimo cha unafiki kinakamika kwao .
 
Tatizo letu hapa nchini huwa watu wote wanaangalia juu kukoje ni kama vile hatuna mipango ya muda mrefu ya kitaifa wakati ipo imekaa tu kwenye makaratasi.
 
Je wakati wanaitunga na kuipitisha hii sheria waliipitisha kwa kuwa walikuwa na uchungu wa rasilimali za taifa kutoka moyoni? Au walipitisha tu kwa sababu tu Rais alikuwa ni Magufuli?
Same skin, same political party, same people, same strategy, same behaviour!! Usijetegemea uzalendo humo, Never ever and ever!!
 
"Maliasili zetu Watanzania zinachukuliwa bure haya ni maajabu,sitaruhusu hilo" Hayati Rais John Pombe Magufuli.
 

Attachments

  • VID-20230715-WA0734.mp4
    9.5 MB
Back
Top Bottom