Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

After a brief period of relatively moderate rule,Nicolae Ceaușescu's regime became increasingly brutal and repressive. By some accounts, his rule was the most rigidly Stalinist in the Soviet bloc.[4] He maintained controls over speech and the media that were very strict even by Soviet-bloc standards, and internal dissent was not tolerated. His secret police, the Securitate, was one of the most ubiquitous and brutal secret police forces in the world!(Wikipedia).
 
Mkuu Informer ilikuonyesha hapa hakuna dhamira njema sec;50
Huu ni utawala wa Imla.Haiwezekani mtu mmoja eti Mkurugenzi wa Mashitaka awe muamuzi wa mwisho na kusiwe na hata nafasi ya kukata rufaa.


Wapinzani wakishiriki katika kupitisha hili,nadhani nitajifikiria kama kunahaja ya kupiga kura hapo Oct.2015
Kama marekebisho ya msingi yatakataliwa wawaache wapitishe wenyewe wenye Nchi
(CCM)
maana na amini wako watu makini Bungeni watakaoleta maboreho muhimu na yakujenga ,lakini kwa sababu kuletwa kwa msada huu kiuharaka kuna nia ofu ndani yake yatakataliwa.


Kufifilisha kosa

50.-(1) Bila kuathiri sheria nyingine inayotumika Tanzania Bara, Mkurugenzi wa Mashtaka, muda wowote kabla ya mwenendo wa mahakama kuanza na kwa kuzingatia tamko la kukiri kosa kwa hiari la mshitakiwa anaweza kufifilisha kosa na kuamuru mtu huyo alipe kiasi cha pesa atakachokitaja ambacho hakitazidi kiasi cha faini kwa kosa hilo.
(2) Amri ya kufifilisha kosa chini ya kifungu kidogo cha (1) itakuwa -
(a) ya maandishi, ikiainisha kosa lililotendeka, kiasi cha fedha zitakazolipwa na tarehe ya kufanya malipo ikiambatanisha tamko la kukubali kosa lililorejewa chini ya kifungu kidogo cha (1);
(b) ni uamuzi wa mwisho na hautakatiwa rufaa; na

(c) na uwezo wa kutekelezwa katika namna sawa na amri ya Mahakama Kuu.


Suala jingine lenye kuleta mianya na matumizi mabaya ya utawala.Ni hili la Waziri mwenye dhamana kutengeneza Kanuni.
Kanuni hizi ifike mahali zipitie kwenye Kamati ya Uongozi ya Bunge na Kamati ya Katiba na Sheria na ijadiliwe na waipigie kura za wazi.


51. Waziri anaweza kutunga Kanuni kuhusiana na jambo lolote ambalo linatakiwa kuainishwa na Sheria hii au ambalo ni la umuhimu au uharaka kwa ajili ya utekelezaji wa masharti ya Sheria hii.
 
Last edited by a moderator:
Kama Serikali ya ccm ingekuwa inatunga sheria kali kwa mafisadi, asingebaki hata mmoja. sheria zao kandamizi ni kwa walala hoi

Membe na January Makamba wana Wasi wasi wa kusumbuliwa juu ya madhambi yao na Fitna zao juu ya Lowasa kwa mbinu za kimafia kwa kutumia kivuli cha Sauti ya Nyerere na picha wakaweka ya Lowasa, kumbuka Nyerere anakataza pesa kutumika kwenda ikulu,

Lakini hao hao January na Membe wanatumia Pesa nyingi kutengeneza na kusambaza video ya sauti ya Nyerere picha za Lowasa lengo lao kumdhoofisha Lowasa na Wao wajisafishie njia kirahisi kwenda ikulu, Mapesa wanazitumia Membe na lowasa kununua njia ya kuelekea ikulu ni mengi kuliko mtu yeyote hivyo Kauli ya Nyerere tayari imewahukumu wenyewe japo waliamini wanamkomoa Lowasa.

Membe ni mwizi wa pesa za Marehemu Gadafi na ufisadi mwingine mwingi tu ikiwemo kununua Ugeni Rasmi kwa Wasabato na sasa kanunua Ugeni Rasmi Tamasha la Pasaka, na January yeye ana madhambi mengi sana tutayaanika kadri tukipata nafasi.
 
Hii Staili ipo China ambapo kule wao wamepiga marufuku mitandao mikubwa kama Google nk kutumika china wakiwa na lengo la kudhibiti Maadili yao na kulinda mitandao yao lakini kumbuka China ni Nchi Tajiri inajitosheleza kwa kila kitu ina uwezo wa kukataa chochote popote na Maisha yakaendelea.

Hapa Tz kinachotaka kufanywa na January na wenzake ni mbinu za kuwadhibiti watu wasiwaanike Madhambi yao na kupunguza speed ya watu kupata Elimu juu ya mataifa mengine wakiamini kuwa itawasaidia, January huwa ni mtu wa kukurupuka kama baba yake hapendi kutafakari Kabla kasahau kuwa watanzania wa sasa wameamka hawataki kuburuzwa.
 
Ukiwa sio muongo, mdaku sheria ni murua Kabisa...

Itasaidia tusome vitu vya ukweli sasa sio mazagazaga. Sometimes we waste a lot of time kusoma maujinga ambayo mtu Hana hakika naye.

kenya ma-blogger mbalimbali waliingia kwenye mikono ya Pilato kwa kucheza na sheria kama hii.

Ni kweli mkuu, mitandao imekuwa na uongo na upotoshaji sana,

Nashindwa kumuelewa mleta mada anaposema sheria kama hii haiendan na demokrasia. Sijui ni demokrasia ipi inayoruhusu uongo na upotoshaji.
 
January Makamba na Membe wanahaha kila Dk kubuni mbinu za kuwasaidia Kuingia ikulu, huku Membe akiwaza Jinsi ya kupata Pesa za kujenga Magereza makubwa mengi ili endapo atakuwa Rais atawafunga jela Viongozi wote wapinzani wake na hata akihisi wewe ni m'baya wake Mwendo ni Gerezani tu, Sheria za Membe zitakuwa kama za China watu watanyongwa kwa wingi sana, Membe atakuwa kama idd Amini na January Makamba atakuwa kama mali ya mungu. Sasa kazi kwenu mpeni Nchi Membe na Makamba muone Balaa lao.
 
Kuna wanasiasa wanafanya hayo hayo lakini si kupitia mfumo wa komyuta bali hadharani au mbele ya vyombo vya habari. je, hao watafanywaje?
 
Kuna sheria ya ya kukonyeza, kuna sheria inayokataza watu kuvutacsigara hadharani....so usihofu
 
Ni kweli mkuu, mitandao imekuwa na uongo na upotoshaji sana,

Nashindwa kumuelewa mleta mada anaposema sheria kama hii haiendan na demokrasia. Sijui ni demokrasia ipi inayoruhusu uongo na upotoshaji.
hata kama kuna uongo lakini
unadhani inastahili unyama huu wa January ? kama wanapotosha kwanini nyie msiweke ukweli ili kunyoosha mambo ? hivi kwa mfano chenge akiitwa fisadi ni kweli kwamba kuna upotoshaji ?
 
Vigumu kushindana na kizazi cha leo cha utandawazi, ukweli mambo pengine yakawa mabaya zaidi kuanikana na vielelezo tulivozoea kuvionea huruma tutafianiaka na huko serikalini wavujishaji ni wengi sana maana wameshachoshwa na usanii wa serikali yetu.
 
Uzuri ni kwamba hawataweza kutufunga au kutuua wote kabla ya saa ya Ukombozi haijafika.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
hata kama kuna uongo lakini
unadhani inastahili unyama huu wa January ? kama wanapotosha kwanini nyie msiweke ukweli ili kunyoosha mambo ? hivi kwa mfano chenge akiitwa fisadi ni kweli kwamba kuna upotoshaji ?

Ndo maana sheria inasema kama una taarifa basi uwe na ushahidi wa kutetea taarifa yako.

Ninaposema upotoshaji sina maana ya mambo ya aikina chenge mkuu, kuna upotoshaji mwingi sana kwenye mtandao wengine mpaka wanazushiana vofo n.k

Kwa hiyo nadhani sheria ya namna hii itaongeza credibility ya habari na taarifa zote mtandaoni.
 
Inabidi sasa tuanze kuencrypt our internet traffic na kutumia anonymizing proxies na VPN.

Itabidi tuanze kuishi kama hackers kwa kuogopa kufuatiliwa na kukamatwa.

Ndiko tulikofikia. Tunajengewa nidhamu ya woga.
 
Back
Top Bottom